Maamuzi yameshatolewa ndo hayo kubaliana nayo tu hata kama hukujiandaa kisaikolojia. Japo ulijiapiza kuwa huwezi kukatwa kwa vile eti upo CCM tangu kuanzishwa kwake lakini ndo hivyo tena yamekuwa hata wenzako pia walikuwemo vile vile.
Ulizua misemo mingi kipindi hiki kama vile HAKATWI MTU, PATACHIMBIKA, HUWEZI KUZUIA MAFURIKO, yote hiyo ilikuwa ni mikwara yako ambayo labda kwa namna moja ama nyingine imekuponza kwa vile ulikuwa kama unaitishia CCM na ngazi zote za juu za maamuzi na uteuzi.
Najua imekuuma sana kutokana na jinsi ulivyokuwa umeikamia nafasi hiyo ya juu kabisa kitaifa lakini kumbuka asiyekubali kushindwa si mshindani. Siasa ndo zilivyo hata wewe unazijua.
Kwa heri mzee wa safari ya matumaini amini tu kuwa umeshakatwa na hakuna rufaa.
Pole sana pia wapambe na wafuasi wake wote.
Bado unayo nafasi ya kuondoa umasikini katika nchi kwa vile ulisema unakerwa nao.
Ni mimi mpiga kura wa kawaida nisiyefungamana na chama chochote. Nasubiri October nimkate mmojawapo kati ya CCM au UKAWA.