Pamoja na nguvu kubwa ya mazingaombwe aliyokua nayo ya kucheza na media pamoja na fedha chafu hizi ndo sababu maalum hawezi kupita hata mchujo wa kwanza wa NEC(5 bora).
1. Ana tuhuma nzito za ufisadi wa richmond uliosababisha kujiuzulu na kutikisika kwa serikali 2008.Tuhuma hizi hakuweza kusafishwa mahakamani(walimbeba ) jambo linalopelekea tuhuma kusimama palepale kisheria.
2. Operation VUA GAMBA, target ya hii kauli mbiu ilikua ni lowassa,Mara baada ya kujeruhiwa bungeni 2008 chama chake kiliona ufisadi ni tatizo kikaanzisha operation ambayo ilipanga kumwangamiza kabisa kisiasa ndugu Ngoyayi alikwepaje tumuulize NAPE ,hapa maana yake chama chake chama chake HAKIMTAKI.
kumbuka kauli ambayo aliitoa katibu mkuu pale mwanza wakati anamaliza ziara za cha,a namnukuu "Tunairudisha misingi ya chama cha mapinduzi ,kiwe chama cha wakulima na wafanyakazi kama alama zinavyoonyesha, CCM sio chama cha wafanya biashara tena ,hawa wafanya biashara ndo wanatuletea ESCROW,RICHMOND,EPA ect" ni nani hajui kama manywele ni businesman?nani hajui kama hela anazogawa kama njugu kuna support kubwa ya business influence?
3. Amekiuka sheria ya gharama za uchaguzi ya mwaka 2011 kifungu Namba 14(1_2)mma kifungu namba 20(1-4) sambamba na kifungu namba 24 cha sheria hiyo ambayo inakataza mgombea yoyote wa nafasi ya urais,ubunge au udiwani .Ikumbukwe hadi sasa Lowassa ametumia zaidi ya billioni 50 kwa ajili ya kuwahonga waandishi wahabari,wenyeviti wa CCM wa mikoa,wabunge,waandesha bodaboda,maaskofu,mashekhe na hivi juzi ametumia zaidi ya shilingi billion 35.5 kuwahonga REDET.
4. Lowassa amezungukwa na wapambe ambao wana criminal records za kifisadi baadhi ni Rostam,Andrew chenge,Nazir Karamagi,Anna Tibaijuka,Kingunge etc.
5. Ugonjwa wake ,mzee ana mgogoro wa Afya si vizuri kuweka details zote hapa lakini hata nyie wenyewe mmeshajionea ameanguka mara kadhaa katika safari tu za kutafuta wazamini kutkana na power ya media manipulation hamkutangaziwa.
6. Alianza kampeni kabla ya wakati ,hamna asiyetambua yeye na wenzake walianza kampeni mapema hadi ikasababishia adhabu ,hata hivyo kipindo cha adhabu alikua bado anaendelea na kampeni hii tafsiri yake ni UTOVU WA NIDHAMU .
7.Visasi hapa nadhani mnanisoma mnakijua akina mwakyembe kiliwapata nini na wengine wakakoswakoswa
8.Makundi -Huyu ndo muasisi wa ccm ya walikua nacho na have nots ,NEC hawawezi wakafanya kosa la ku hype matabaka
9.Kashfa ya tuhuma ya kutaka kuutenganisha uenyekiti wa chama na urais hii siyo ndogo ipo bado kwenye records
Ni hayo tu