Edward Lowassa on ITV!-Dakika 45 Part II!.

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
57,214
Reaction score
128,976
Wanabodi,
Wale wenye access na ITV, lets watch part II ya Mahojiano ya Waziri Mkuu wetu mstaafu kwa kujiuzulu, Edward Lowassa kwenye kipindi cha Dakika 45 kinachorushwa na ITV kuanzia saa 3:00 usiku huu!.

Its expected EL pia atazungumzia his presidential bid kwa uchaguzi wa 2015!.

Nawaombeni tumsikilize kwa makini sana haswa kwa kuzingatia siasa za nchi hii, hazitabiriki sana, haswa kipengele cha "Umdhanie Siye kumbe Ndiye" na pia uwezekano wa "Jiwe walilolikataa waashi, kufanywa kuwa jiwe kuu la pembeni"!.

Kipindi kimekwisha.

My Take.

Nimemsikiliza kwa makini sana, kiukweli namkubali huyu jamaa kwa 100%!.
Wale wenzangu na mimi, wenye mategemeo ya ukombozi wa kweli wa pili wa Mtanzania, kwa mwaka 2015, lazima wamshukuru sana JK, kwa sababu ni kupitia JK, uwezekano wa kuwezekanika kwa ukombozi huo, kunawezekanika!.

Wale mnaolalamika kuwa miongoni mwa makosa makubwa Watanzania, waliofanya, ni kumchagua JK kuwa rais wetu!, kiukweli, uchaguzi wa JK ndio kichecheo cha ukombozi wa pili wa Mtanzania, vinginevyo kama ni Lowassa ndie angekuwa rais, Tanzania isingekuwa hapa ilipo, na kusingalikuwepo hata hilo hitaji la ukombozi wa pili wa Mtanzania maana Tanzania ingeshakuwa peponi!.

Hivyo wale wote wenye kulitakia mema taifa hili, mshukuruni sana EL na JK, vingenevyo 2015, ingekuwa ni hadithi ile ile tulioizoea!.

Asanteni.

Pasco.
 
dah, hajielewi, hata kumsikiliza inakuwa ngumu mno.

Bora awe fundi mchundo!
 

Pasco Heshima mbele!
Naomba unijuze kama kweli CCM watakuwa tayari kumsimamisha EL kuwa mgombea wao wa nafasi ya urais!
 
Kipindi kimeanza, anaanza na repeat ya hoja yake ya gesi kuwa vitalu vilivyoshagawiwa vinatosha, tusiendelee kugawa vitalu. Mtaniona mjinga, ' I'm not a fool"!.
 
Lowassa alistaafu lini..??
 
Anaendelea kuzungumzia tena gesi, nimeisha note some "inconsistance" na unnecesarry repitition, kama alipozungumzia gesi, akarukia tatizo la ajira kwa vijana, sasa amerudi gesi!, inawezekana ni mtangazaji au ni edditing!.
 
ELK hakubaliani na Kilimo Kwanza, amesema hapingi sera, bali "Elimu Kabla Kilimo Kwanza", elimu ndio msingi wa maendeleo, tuwekeze kwanza katika elimu ndipo tuje kwenye mapinduzi ya kilimo, viwanda etc!.
 
ELK hakubaliani na Kilimo Kwanza, amesema hapingi sera, bali "Elimu Kabla Kilimo Kwanza", elimu ndio msingi wa maendeleo, tuwekeze kwanza katika elimu ndipo tuje kwenye mapinduzi ya kilimo, viwanda etc!.

mpaka hapa bado yuko sahihi kabisa, naendelea kusubiri kitu hapa aropoke...
 
Kwa kweli leo Lowassa anatoa points,sijawahi kuona,mi si mshabiki wake lakini nakiri he is far 1000times better than any other person in ccm
 
El, gavana aanzishe mjadala wa kitaifa kwa nini inflation haijashuka, aeleze kwa kina....
 
Lowassa alistaafu lini..??
Alistaafu kwa kujiuzulu, na analipwa mafao yake yote kama mstaafu!. Kwa vile bado hatuna msamiati wa "mjiuzulu", then ni staafu kwa kujiuzulu!.
 
huyu jamaa ni.mpinzani wa kikwete na ccm kwani anaenda kinyume na sera yao ya kilimo kwanza
 
Anasema Angekuwa Rais angechukua mamia ya wanajeshi apande mahecta ya michikichi tungepata mafuta mengi tungejenga kiwanda Iyo ni mbinu moja na anazo Mia moja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…