Eckenford Sekondari,Chuo cha Ualimu na Chuo Kikuu kupigwa mnada na NBC kwa kushindwa kulipa deni

barafu

JF-Expert Member
Apr 28, 2013
6,726
32,818
Chuo kikuu kishiriki cha Eckenford kilichopo mkoani Tanga kinatarajiwa kupigwa mnada pamoja na Taasisi zilizopo chini yake ili kufidia deni wanalodaiwa na Benki ya taifa ya Biashara (NBC).



Kampuni ya udalali ya Bani Investment imetangaza kupiga mnada chuo hicho kilichopo kwenye kiwanja namba 53/2 na 54/2 eneo la Central Tanga. Pia kampuni hiyo itapiga mnada Shule ya sekondari Eckenford na Chuo cha Ualimu Eckenford vilivyopo eneo la Kange, kiwanja namba 12 chenye ukubwa wa Ekari 3.4 za eneo.
 
Dah..

Mwaka huu mgumu sana aiseee, kila sehemu mali zinapigwa mnada.

Ipo siku tutasikia Mukulu kapiga mnada jumba jeupe pale magogoni kufidia deni la Tanesco.
Ni kweli Mkuu ila Magogoni hapauzwi ng'o ni nyie ndio mtauzwa na kuisoma namba
 

Na wanafunzi nao watapigwa mnada au ni majengo tu?
 
da mali za urithi na majanga yake .. lipeni tarimo family
 
NBC kuleni na wenzenu... kama q chillah

Dah huyu nae sijasikia kakamatwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…