Ebola imeingia Tanzania?

Ebola imeingia Tanzania?

Aisee nimepata hofu sana maana kwa jinsi nilivyopata maelezo inaonekana kuna kitu. Naendelea kufuatilia
 
Wakuu tetesi nilizozipata ni kuwa hofu ya kuingia kwa homa ya ebola imezidi kusambaa baada mgonjwa alielazwa hospital moja ya mkoa huko kusini mwa tz kufariki usiku wa kuamkia leo na kuamriwa kuzikwa haraka leo hii hii.. Najua kuna wenye taarifa sahihi ya hizi tetesi anaweza kutuwekea hapa.. Mungu ibariki Tanzania
Nyanda za juu kusini nako inasemekana kuna client
 
Nimefuatilia michango ya watu wengi hapa
na kujiridhisha kuwa; kama hawa wanaochangia hapa wanawakilisha uelewa wa vijana wetu walio wengi; BADO TUNA MUDA MREFU WAKUJENGEA VIJANA MAARIFA. Yaani watu wanaliona Gonjwa la Ebola ni issue ya kuchezea???
Hawajui kuwa kauli moja tu ya mlipuko isiyo sahihi (hasa kupitia kwa makanjanja) inaweza kuletea taifa hasara ya Mabilioni ?
Vijana tuwe makini na masuala ya Kitaifa; SIO KILA KITU KINAHITAJI USHABIKI KAMA WA YANGA NA SIMBA
Lakini muhimu zaidi mambo ya kitaifa yanasemwa na Msemaji wa Taifa/idara husika na sio kila mtu kujiona yeye ndiye msemajii..
 
Tanzania not sharing information on suspected Ebola cases: WHO
East African country yet to comment on WHO rebuke, but had previously told UN health agency it had no cases of Ebola.
David Child6 minutes ago
Tanzania not sharing information on suspected Ebola cases: WHO

The current Ebola outbreak, the second deadliest in history, has claimed the lives of more than 2,000 people [File: Samuel Mambo/Reuters]
The World Health Organization (WHO) has issued a rare public rebuke to Tanzania over its failure to provide detailed information on suspected Ebola cases.

In a statement on Saturday, the UN health agency said it had learned of one suspected fatal case of the virus in Tanzania's commercial capital, Dar es Salaam, and two others but, despite repeated requests, was provided with no information from the country's authorities.


"To date, clinical data, results of the investigations, possible contacts and potential laboratory tests performed ... have not been communicated to WHO," the statement said.
 
Jana nilienda kanisani maeneo ya kimara.
baada ya ibada alisimama mama mmoja aliyejitambulisha kama mtaalamu kutoka wizara ya Afya. yule mama alitutahadharisha tuchukue tahadhari na ugonjwa wa ebola.miongoni mwa sababu alizosema ni kwamba ugonwa ule waweza kuwepo nchini kwa maana tunazungukwa na walioathirika
Swali mama yle alitumwa nanani na kwanini alifika pale? aliongea kama muumini au mtaalamu wa afya?
serikali kuweni wawazi ugonjwa upo nchini
wasalaam
Hiyo ni tahadhari
Huwezi kusubiri hadi ugonjwa uingie ndio uanze kufundisha unakuwa umesha chelewa
 
Ebola si utani, kama ipo dawa ni kuitangaza na kuhakikisha kila mtu anajua akiwa na mgonjwa afanye nini. Bila hivyo itainua tu kichwa chake. Kwanini watu wanazikwa na serikali??
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Aisee...sasa kwa nini wizara ya Afya haitoi angalizo?? Hili gonjwa ni hatari sana....tutakwisha.
 
Hata sielewi sababu za hii Serikali kufanya siri kubwa kiasi hiki hata kujichafulia jina kule WHO.

Tuna Rais wa ajabu sana na Serikali ya ajabu sana ambayo haijali maslahi ya Tanzania na Watanzania.



Wakuu tetesi nilizozipata ni kuwa hofu ya kuingia kwa homa ya ebola imezidi kusambaa baada mgonjwa alielazwa hospital moja ya mkoa huko kusini mwa tz kufariki usiku wa kuamkia leo na kuamriwa kuzikwa haraka leo hii hii.. Najua kuna wenye taarifa sahihi ya hizi tetesi anaweza kutuwekea hapa.. Mungu ibariki Tanzania
 
Ebola ipo Tanzania na serikali inafanya siri. Sijui kwa faida ya nani.
Wamekataa kutoa za sample za vipimo kwa WHO kama sheria/makubaliano ya kimataifa yanavyotaka. Ni aibu kubwa. Kama ni negative, wanaogopa nini?
Kama vikatuni serikali imeomba US$ 9M huko huko WHO huku ikitangaza kununua ndege zenye thamani ya US$90M kila moja. Tumerogwa.
 
Serikali Imetoa Ufafanuzi Kuhusu Ebola
Tanzania Hakuna
 
Mficha maradhi kifo humuumbua, hii kitu ikishavamia kariakoo na mawasiliano TUMEKWISHA!
 
Waziri kusema hakuna EBOLA siyo ushahidi kuwa hakuna EBOLA
Tunataka Waziri aje na Paneli ya Madkatari waongee kitalamu, Watuonyeshe na ripoti za vipimo vya maabara, wathibitishe kuwa kweli EBOLA haipo ili baadae kama ipo tuweze kuwashitaki kwa kuvunja viapo vyao!

Kwa hali ya sasa simuamini Waziri maana kama ni matamko mawaziri tumeshaona mawaziri wa wizara mbalimbali wakitoa matamko amabayo wakati mwingine yanakuwa ya kisiasa.

Maelezo ya Waziri hayatoshi!

Serikali isilete Siasa kabisa katika hili suala hatutaielewa kabisa!

View attachment 1207655


View attachment 1207657

View attachment 1207675

View attachment 1207692
Hivi hii habari ya ebola iliyoenezwa na wapinzani imefikia wapi? Sijawahi kuona upinzani wa hovyo kama huu wa sasa wa kueneza habari za uongo katika nchi yetu na si ule upinzani wa enzi ya Dr. Slaa wa kufichua ufisadi.
 
Hivi hii habari ya ebola iliyoenezwa na wapinzani imefikia wapi? Sijawahi kuona upinzani wa hovyo kama huu wa sasa wa kueneza habari za uongo katika nchi yetu na si ule upinzani wa enzi ya Dr. Slaa wa kufichua ufisadi.
Ama kweli kuna siku wake zenu wakikosa uzao mtasema ni hao hao wapinzani wamechukua vizazi vyao.
 
Back
Top Bottom