Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,401
- 31,364
DHANA YA 'DAMAGE CONTROL'
Kwa mara ya mwisho tuligusia namna ambayo siku 14 zilipita bila uongozi wa Chadema kutoa ufafanuzi , maelezo au majibu sakata la AR.
Siku 14 ni nyingi sana kuachia mada ijieleze na kujijibu yenyewe. Ndipo tulisema dhana ya damage control haikutumika kwa gharama kubwa kisiasa.
Hili halikuwa tukio la kipekee kwa Chadema, vyama kama CUF, NCCR vimepita katika majaribu kama hayo na vimeumia sana.
Kwa ukongwe wa kisiasa, CCM wameweza kufanya damage control ingawa kutokana na siasa za chuki na makundi kazi hiyo inakuwa ngumu. Mfano, waliunda kamati ya mzee ruksa kutafuta muafaka wa chuki baada ya mashambulizi yenye hasira kutoka pande zinazohasimiana.
Ilifika mahali siri za chama na viongozi zinamwagwa hovyo na kukidhalilisha Chama, ndipo kamati ikaundwa kuepusha malumbano.
CCM imekuwa ikijitenga haraka na watu au mtu wenye kashfa, ndiyo maana mara zote wanatoa matamko kama yale yasemayo chama si fisadi ila ufisadi ni wa watu binafsi, wakati mwingine kufikia hatua hata za kuwachachafya watuhumiwa ili kupata 'damage control' mapema kabisa.
Damage control inatumika katika serikali, taasisi na mashirika katika ngazi zote za kitaifa hadi kimataifa. Inafanyika kwa njia nyingi.
Kwa mfano Obama alipoandamwa na tuhuma za mchungaji 'Right' ilimchukua muda mrefu kujibu tuhuma kiasi kwamba kampeni yake iliyumba sana. Bahati nzuri Obama ni Orator mzuri aliugeuza uharibIfu kwa manufaa katika hotuba yake Pennyslavania.
Hata hivyo kuzembea kujibu shutuma, tuhuma au kauli umekuwa ni udhaifu mkubwa sana wa kampeni za Obama na humgharimu.
Tofauti na Obama, Hillary alizusha yake aliposema akiwa Bosnia alipokewa uwanja wa ndege risasi zikivuma angani.
Ukweli ni kuwa alipokelewa na maua na ilionekana kuwa kama kashfa kubwa ya uongo. Hillary alikwenda kwenye vyombo vya habari na kutetea kauli zake na kuhudhuria vipindi 'talk show' ambapo aligeuza tuhuma kuwa mzaha akiwa na comedians na kupoteza nguvu.
Wakati hayo yakiendelea watu wanaojulikana kama Political pundits walikuwa wanatafuta hoja mbadala itakayokuwa na nguvu.
Waziri mkuu wa zamani wa Uingereza bw.Godon Brown alinaswa na vipaza sauti kabla hajavivua vikimkariri akimwita mwanamke mmoja Bigots.
Ilipotokea katika vyombo vya habari asubuhi akaenda nyumbani kwa yule mama kumtaka radhi. Alifahamu uharibifu utakaotokana na maelezo au malumbano yasiyoisha ni mkubwa sana kuliko kusema samahani.
Tunakumbuka mwandishi aliyemwagiwa tindikali, baada ya minong'ono iliyohusishwa na habari za ufisadi, siku iliyofuata Rais aliagiza serikali igharamie matibabu je! hii ilifanyika ili kuua minong'ono kwani ni wakati huo shauri la marehemu Bilali lilikuwa moto.
Mwandishi alipokuwa anakaribia kurudi alisema ataweka wazi waliohusika akifika Dar. Baada ya muda wakakamatwa vibakwa kwa kubambikiwa shitaka. Hapo shitaka likawa mahakamani na hakukuwa na uhalali wa kuliongelea.Baada ya miaka 3 nguvu yake ikapungua vibaka wakaachiliwa.
Hii ilikuwa ni sehemu ya mkakati wa damage control kwasababu ni kipindi hicho EL alikuwa na Richmond na hili la mwandishi lingefunua mambo makubwa kama lingeachiwa kuongelewa hovyo.
Katika taasisi au mashirika nayo hujikuta katika gharma kubwa ima za kuwalinda au kuwaweka sawa watumishi wao ili pamoja na mambo mengine wasijehusishwa na uharibifu wa heshima (reputation). Hakuna shirika litakalofurahi kusikia manager au CEO ameokotwa chakari mitaani, au CEO anahusishwa na biashara chafu kama za madawa au umalaya. Taasisi na mashirika huchukua hatua za awali kuzuia kama njia ya awali ili wasifikie hatua ya damage control ambayo si njema na ni ghali.
Nimelitolea mfano hili kwasababu gharama zake zilikuwa kubwa kwa chama cha CUF kilichokuwa na wafuasi wengi wa ukanda wa pwani.
CUF waliposhutumiwa kuwa chama cha Kidini (Kiislamu) badala ya kufanya damage control (hata kama haikuwa kosa lao) wao wakaacha kwanza jambo hilo likaaminishwa vichwani mwa watu kwa muda mrefu sana. Walipotakiwa kujibu walichofanya ni kuchochea uharibifu kwa kusema CCM nayo ina viongozi wengi wakristo, ni chama cha Kikirsto. Hawakuwa na political strategists, pundits, observers au analysts kwasababu chama kilijengwa kwa personality hasa ya maalimu Seif na si idara au wanachama.
Kwa kukosa watu muhimu kama Pundits, Observers, commentators n.k katika idara za CUF, makosa yakaendelea kufanyika na kuharibu zaidi.
Chama kikawa kinafanya mikutano siku ya Ijumaa baada ya swala! Hii ikashadidia hoja iliyokuwepo awali hata kama ilikuwa ni ya uongo. Uharibifu huo ukawa mkubwa sana na damage control haikuwezekana na kupelekea chama kubaki katika vitabu vya historia.
Chadema, chama cha upinzania ni makini sana lakini bado hawajajifunza kutoka CUF au NCCR kwa undani. Nasema hivi kwasababu chama kimekuwa kama mtu au watu na si idara. Haiwezekani Dr Slaa awepo kila mahali kutoa kauli hata kwa mambo madogo.
Ni mara chache kumsikia msemaji wa chama, au watu wanaolinda maslahi ya chama (pundits, strategists etc) wakitoa ufafanuzi au kauli. Matokeo yake siku zote watu husema Dr mbona hajasema au kasemaje! Hiki ni chama na idara zake ni lazima zifanye kazi kikamilifu.
Kwani tatizo la Chadema ni ukosefu wa watu wenye sifa au kutokuwa tayari kuajiri wenye sifa au kutoona umuhimu tu!!!
Chadema wapo Slow katika ku-seize opportunity hasa CCM wanapobofoa. Ni slow katika kujibu tuhuma, na ni slow katika ufuatiliaji.
Inawezekana kuwa ni mkakati wao ndio maana wapo makini sana, lakini in politics timing is very important.
Ndio maana nasema haiwezekani damage control ifanyike baada ya siku 14 halafu useme huo ni mkakati na sio mapungufu.
Hitimisho:
CCM wanaijua vema dhana ya damage control, timimg and who is to say what.
Vyama vya upinzania bado dhana hii haieleweki. Hoja ya Nape haijibiwi na Katibu mkuu wa Chadema inajibiwa na 'counterpart wa Chadema'.
Upinzani ujue ku react promptly with precisions na ikitokea kuna dalali li za uharibifu damage control ifanyike mapema sana kuepuka gharma zisizo za lazima kisiasa. Lakini pia wawe innovative si kila jambo wafanye kwa 'template ya CCM'.
Ni wakati tusemezane ili kuviimarisha vyama vya siasa tusijerudi kule kule kwa NCCR au CUF.
Hatuna muda wa kulelea vyama vipya kila msimu, tulee vilivyopo ili tuwe na demokrasi ya nguvu na kweli.
Kwa mara ya mwisho tuligusia namna ambayo siku 14 zilipita bila uongozi wa Chadema kutoa ufafanuzi , maelezo au majibu sakata la AR.
Siku 14 ni nyingi sana kuachia mada ijieleze na kujijibu yenyewe. Ndipo tulisema dhana ya damage control haikutumika kwa gharama kubwa kisiasa.
Hili halikuwa tukio la kipekee kwa Chadema, vyama kama CUF, NCCR vimepita katika majaribu kama hayo na vimeumia sana.
Kwa ukongwe wa kisiasa, CCM wameweza kufanya damage control ingawa kutokana na siasa za chuki na makundi kazi hiyo inakuwa ngumu. Mfano, waliunda kamati ya mzee ruksa kutafuta muafaka wa chuki baada ya mashambulizi yenye hasira kutoka pande zinazohasimiana.
Ilifika mahali siri za chama na viongozi zinamwagwa hovyo na kukidhalilisha Chama, ndipo kamati ikaundwa kuepusha malumbano.
CCM imekuwa ikijitenga haraka na watu au mtu wenye kashfa, ndiyo maana mara zote wanatoa matamko kama yale yasemayo chama si fisadi ila ufisadi ni wa watu binafsi, wakati mwingine kufikia hatua hata za kuwachachafya watuhumiwa ili kupata 'damage control' mapema kabisa.
Damage control inatumika katika serikali, taasisi na mashirika katika ngazi zote za kitaifa hadi kimataifa. Inafanyika kwa njia nyingi.
Kwa mfano Obama alipoandamwa na tuhuma za mchungaji 'Right' ilimchukua muda mrefu kujibu tuhuma kiasi kwamba kampeni yake iliyumba sana. Bahati nzuri Obama ni Orator mzuri aliugeuza uharibIfu kwa manufaa katika hotuba yake Pennyslavania.
Hata hivyo kuzembea kujibu shutuma, tuhuma au kauli umekuwa ni udhaifu mkubwa sana wa kampeni za Obama na humgharimu.
Tofauti na Obama, Hillary alizusha yake aliposema akiwa Bosnia alipokewa uwanja wa ndege risasi zikivuma angani.
Ukweli ni kuwa alipokelewa na maua na ilionekana kuwa kama kashfa kubwa ya uongo. Hillary alikwenda kwenye vyombo vya habari na kutetea kauli zake na kuhudhuria vipindi 'talk show' ambapo aligeuza tuhuma kuwa mzaha akiwa na comedians na kupoteza nguvu.
Wakati hayo yakiendelea watu wanaojulikana kama Political pundits walikuwa wanatafuta hoja mbadala itakayokuwa na nguvu.
Waziri mkuu wa zamani wa Uingereza bw.Godon Brown alinaswa na vipaza sauti kabla hajavivua vikimkariri akimwita mwanamke mmoja Bigots.
Ilipotokea katika vyombo vya habari asubuhi akaenda nyumbani kwa yule mama kumtaka radhi. Alifahamu uharibifu utakaotokana na maelezo au malumbano yasiyoisha ni mkubwa sana kuliko kusema samahani.
Tunakumbuka mwandishi aliyemwagiwa tindikali, baada ya minong'ono iliyohusishwa na habari za ufisadi, siku iliyofuata Rais aliagiza serikali igharamie matibabu je! hii ilifanyika ili kuua minong'ono kwani ni wakati huo shauri la marehemu Bilali lilikuwa moto.
Mwandishi alipokuwa anakaribia kurudi alisema ataweka wazi waliohusika akifika Dar. Baada ya muda wakakamatwa vibakwa kwa kubambikiwa shitaka. Hapo shitaka likawa mahakamani na hakukuwa na uhalali wa kuliongelea.Baada ya miaka 3 nguvu yake ikapungua vibaka wakaachiliwa.
Hii ilikuwa ni sehemu ya mkakati wa damage control kwasababu ni kipindi hicho EL alikuwa na Richmond na hili la mwandishi lingefunua mambo makubwa kama lingeachiwa kuongelewa hovyo.
Katika taasisi au mashirika nayo hujikuta katika gharma kubwa ima za kuwalinda au kuwaweka sawa watumishi wao ili pamoja na mambo mengine wasijehusishwa na uharibifu wa heshima (reputation). Hakuna shirika litakalofurahi kusikia manager au CEO ameokotwa chakari mitaani, au CEO anahusishwa na biashara chafu kama za madawa au umalaya. Taasisi na mashirika huchukua hatua za awali kuzuia kama njia ya awali ili wasifikie hatua ya damage control ambayo si njema na ni ghali.
Nimelitolea mfano hili kwasababu gharama zake zilikuwa kubwa kwa chama cha CUF kilichokuwa na wafuasi wengi wa ukanda wa pwani.
CUF waliposhutumiwa kuwa chama cha Kidini (Kiislamu) badala ya kufanya damage control (hata kama haikuwa kosa lao) wao wakaacha kwanza jambo hilo likaaminishwa vichwani mwa watu kwa muda mrefu sana. Walipotakiwa kujibu walichofanya ni kuchochea uharibifu kwa kusema CCM nayo ina viongozi wengi wakristo, ni chama cha Kikirsto. Hawakuwa na political strategists, pundits, observers au analysts kwasababu chama kilijengwa kwa personality hasa ya maalimu Seif na si idara au wanachama.
Kwa kukosa watu muhimu kama Pundits, Observers, commentators n.k katika idara za CUF, makosa yakaendelea kufanyika na kuharibu zaidi.
Chama kikawa kinafanya mikutano siku ya Ijumaa baada ya swala! Hii ikashadidia hoja iliyokuwepo awali hata kama ilikuwa ni ya uongo. Uharibifu huo ukawa mkubwa sana na damage control haikuwezekana na kupelekea chama kubaki katika vitabu vya historia.
Chadema, chama cha upinzania ni makini sana lakini bado hawajajifunza kutoka CUF au NCCR kwa undani. Nasema hivi kwasababu chama kimekuwa kama mtu au watu na si idara. Haiwezekani Dr Slaa awepo kila mahali kutoa kauli hata kwa mambo madogo.
Ni mara chache kumsikia msemaji wa chama, au watu wanaolinda maslahi ya chama (pundits, strategists etc) wakitoa ufafanuzi au kauli. Matokeo yake siku zote watu husema Dr mbona hajasema au kasemaje! Hiki ni chama na idara zake ni lazima zifanye kazi kikamilifu.
Kwani tatizo la Chadema ni ukosefu wa watu wenye sifa au kutokuwa tayari kuajiri wenye sifa au kutoona umuhimu tu!!!
Chadema wapo Slow katika ku-seize opportunity hasa CCM wanapobofoa. Ni slow katika kujibu tuhuma, na ni slow katika ufuatiliaji.
Inawezekana kuwa ni mkakati wao ndio maana wapo makini sana, lakini in politics timing is very important.
Ndio maana nasema haiwezekani damage control ifanyike baada ya siku 14 halafu useme huo ni mkakati na sio mapungufu.
Hitimisho:
CCM wanaijua vema dhana ya damage control, timimg and who is to say what.
Vyama vya upinzania bado dhana hii haieleweki. Hoja ya Nape haijibiwi na Katibu mkuu wa Chadema inajibiwa na 'counterpart wa Chadema'.
Upinzani ujue ku react promptly with precisions na ikitokea kuna dalali li za uharibifu damage control ifanyike mapema sana kuepuka gharma zisizo za lazima kisiasa. Lakini pia wawe innovative si kila jambo wafanye kwa 'template ya CCM'.
Ni wakati tusemezane ili kuviimarisha vyama vya siasa tusijerudi kule kule kwa NCCR au CUF.
Hatuna muda wa kulelea vyama vipya kila msimu, tulee vilivyopo ili tuwe na demokrasi ya nguvu na kweli.