Hii ndio hasara ya kufanyia majaribio damu za watu! Kwangu mimi ni upumbavu kutoa damu yako kwa ajili ya kutafuta, kuitetea ama kuilinda Demokrasia-Afrika! Wengi wanaojua wasichokitaka, pia ni wengi wanaojua wanachokitaka, lakini ni wachache sana wanaojua gharama sahihi na njia ya kufikia kile wanachokitaka!
Ni MANTIKI tu ndiyo iliyopewa uhalali wa kumwaga damu za watu kwa idadi yoyote, sio mifumo wala sera zaliwa na hulka za watu wapumbavu! Ni MANTIKI tu ndiyo ipasayo kufiwa! Nayo tuweza kuipata hvi, je kuna uhalali wa kuondoa kilichopo? Je, kuna uhalali wa kuleta tutakacho? Je, kuna uhalali wa namna ya kuleta kile tutakacho? (uhalali ni kwa mazingira na nyakati zetu mahususi) Kama jibu ni ndio kote, basi DAMU yangu i radhi hata leo, maana huo ni UTU! Lakini kama hata moja tu ni hapana, ni dhambi kubwa kutumia hisia zako na zangu kumwaga damu yangu, ni DHAMBI na ULAANIWE, kwa maana kamwe damu haitakauka aridhini kila uchao na hautaota mmea! Hakuna mzazi atakayekataa kuwekewa kisu shingoni kwa kukitoa kwenye shingo ya mwanae, ILA TU ASIWE MFU maana haitakuwa na maana tena bali ni ULIMBUKENI!
Serikali mfu ni zetu, wahanga wa kwanza ni watoto wetu, ndani ya aridhi yetu. TUSIPENDE KUKURUPUKA! Kila kitu ni HESABU, zikisukwa vizuri hakutakuwa na kujutia hata ikigharimu damu nusu ya watoto wetu! Alaaniwe anayesabisha damu ya mtu mweusi kumwagika, ati kwa ajili ya Demokrasia! Alaaniwe kwa kumwaga damu za watu bure! Alaaniwe kwa upunguani na ulimbukeni wake! TUSIFANYIE MAJARIBIO DAMU ZA WATU, KILA KITU KINAWEZEKANA ILA NI HESABU.
a4afrika. Mungu wetu yu tayari kutushindia vitani. Anaita sasa!