"Alinda, post: 32292022, member: 11140"]
Kabla Mwenyezi Mungu hajanichukua nilitamani kuona tunazalisha taifa la vijana wa kuhoji, vijana ambao si wa ndio mzee, vijana ambao si wapiga goti kwa watawala bali vijana ambao wanaheshima, busara na hekima lakini hapo hapo vijana ambao wanaweza kuhoji, kujenga hoja za msingi kwa manufaa ya taifa lao.