Mkuu Nguruvi, kuongezea mada yako sababu nyingine ya msingi kutaka kuungana ilikuwa kuepusha vita. Katika makubaliano ya awali the six members waliafiki iwapo kuna mgogoro wa kisiasa baina yao.........
Eric , ahsante sana kwa mchango wako
Kuhusu Brexit, tunaweza kusema kuna layers za sababu.
Hata hivyo, kama tulivyoonyesha hapo awali UK haikuwa na interest na EU kwa muda mrefu. Tulionyesha kuwa ilichukua miaka 10 kwa UK kutuma maombi ya kujiunga (1960), kukataliwa na kisha kuomba tena na tena.
Hata baada ya kukubaliwa bado wananchi walilazimika kupiga kura ya maoni 1975
Katika bandiko lako umesema 'issue ni uhuru wa kujiamulia na suala la immigration'
Ni kweli kuwa UK inaona nguvu za parliament na judicial system zinapokwa na EU.
Lakini hapa kuna suala jingine limejificha 'national identity'
Kujiunga na Eurozone inamaanisha kufikia mwisho kwa pound sterling, pesa inayoaminika kuwa ya zamani katika Ulaya tangu miaka 1600.
Wengine wanaona ni kupoteza identity
Ingawa wachumi wamefanya test nyingi kuhusiana na Eurozone, hakuna matokeo yanayoonyesha atahri kubwa kiuchumi
Kwa Wasomaji, Eurozone haina maana ya EU, ni muungano wa nchi za EU zinazotumia mfumo mmoja wa fedha 'monetary system' ambao si wanachama wote ni Eurozone
UK ilijitoa kufuatia kifungu cha mkataba wa Masaachtrit unayoipa UK op-out
Sababu kubwa ni uchumi wakidai mabadiliko ya Pound kwenda Euro yata destabilize uchumi wa ndani na kubebesha walipa kodi mzigo mzito unaotokana na washirika hasa katika mambo ya madeni ya mifuko ya jamii
Schengen: Ni ushirika wa wanachama wa EU kuhusu visa, kwamba EU iwe ni eneo huru kwa wanachama. Kama ilivyo Eurozone, Schengen si kila mwanachama, wapo wasio!
Na hakika hili ndilo limekuwa sababu kubwa, kwamba UK inataka iwe na uwezo wa kudhibiti mipaka yake (Border protection) ili kuzuia wahamiaji wa kiuchumi.
Wengi wanadhani wahamiaji ni kutoka Asia na Afrika. Gazeti la the Guradian limeripoti katika kipindi cha miezi mitatu wahamiaji takribani 300,000 wameingia na kutoka UK na wengi wakitokea nchi za Ulaya na hasa Ulaya Mashariki.
EU inawapa fursa za kushiriki shughuli zote za kiuchumi bila kuwa na ruhusu ya nchi husika. Hilo ndilo UK wanaona linaathiri soko la ajira.
Kwamba walio na ajira zisizo na uhakika wanaathirika kwa ushindani na pia mapato. Waajiri wamepata soko rahisi la waajiriwa na hivyo kukwaza kiwango cha mishahara.
Na mwisho ni social change , kwamba wahamiaji wengi watapoteza utamaduni wa UK kwa kuchagnayika, linawatisha wahafidhina wanaoona national identity itapotea na athari kwa culture and tradition
Hivyo ukiangalia kwa haraka ni ngumu sana kujua nini kinawakwaza UK katika EU
Hata baada ya majadiliano ya Brussels yaliyoongeza 'opt-out' bado sehemu ya UK haikubaliani na uwepo ndani ya EU.
Ukipitia maoni ya wachambuzi wengi hakuna kukubaliana kwa sababu moja kuu ya kwanini kuwe na Brexit.
Isipokuwa, kuna sababu nyingi zinazoorodheshwa ambazo ni Economy, social change na national identy zote zikichagizwa kwa nguvu na suala la immigration
Itaendelea..