Dunia sio Salama

Dunia sio Salama

Ndege imefichwa kwenye garage ya mtu, watu wapo bize kuzunguka mabaharini.
 
Dunia ni SALAMA ila NYIE mnaoishi huko ndani yake ndio MMEONDOA huo usalama
 
Mungu anajua kwani huwa wanatabiri hali ya hewa kuwa swari halafu gharika inawakumba kwa hiyo basi ndugu yangu mi namuamini muumba wa vyote na kila analotaka liwe linakuwa asante
Kwa upande wa Kiimani, Ni kweli mkuu Mungu Muumba wa vyote ndiyo mpango mzima..hawa wengine ni ubatili mtupu na kujilisha upepo
 
Shit happens! (kuna jamaa alijibu hivyo tu alivoulizwa, hadi muuliza maswali akabaki kastaajabu)
 
Dunia ni SALAMA ila NYIE mnaoishi huko ndani yake ndio MMEONDOA huo usalama
kwa hiyo waondoke hao waliopo humo ili iwe salama? adhani kuna namna ya kufanya ili waliomo waishi kwa amani na upendo. Tukiweza kuondoa mgawanyiko mkubwa wa kitabaka na maonevu mbalimbali nadhani utakuwa mwanzo mzuri wa kuisaka amani, hata ndege kama hii iliyopotea haitapotea tena kwa kusababishwa na wanadamu
 
sasa wewe unadhani tufanyeje kama watanzania katika kujihakikishia usalama wetu?
unaposema usalama wetu una maanisha nini? Kwasababu kwa mtazamo wangu nazan hii ni ajali kama ajali zingine and there is nothing u can do abt it bcz accident happens, ila kama unazani ni mambo ya kigaidi basi kwa nchi kama yetu tuko hatarini zaidi
 
okey! kwani haya masetelite hayafanyi kazi? mbona wamarekani waliweza kumuua Osama bila Pakistan kujua? yaani kwa dunia ya sasa (kitechnolojia) wenzetu wako mbali sana, sasa sijui setilite zao zilizimwa au ...sipati picha

215798_583783181639734_2023248828_n.jpg Msiumize kichwa wataalam wa anga tushajua hiyo imewekwa kitondocha moja ya jumba bovu kwenye mitaa ya maskini mjini humo sasa ngoja tukalinde heshima ninyi subirien matokeo.
 
Wasiwasi wangu usikute imetekwa kwa ajili ya kuitumia kama silaha.

kama kusudi ndilo hilo itakuwa hatari sana. Hatari itakuwa kubwa kama imetua sehemu na watekaji wakapata nafasi ya kuijaza silaha za maangamizi.

Na wakaiwekea vifaa vingine vya kuondoa utambulisho wa awali na kuibadilisha rangi na kuweza kuruka tena juu.

Ijulikane hawa watekaji hawatakuwa wakiogopa kufa. Na hata kama ni kuizuia kwa kuitungua bado hatari itakuwa kubwa kwani huwezi kujua kuwa itaangukia wapi,

ni kweli kabisa dunia siyo salama kwa sasa. Hofu kubwa ni kama imetekwa , watekaji watakuwa ni wataalamu wa hali ya juu.

Maswali ya kujiuliza bado ni mengi sana, kwani kuna utata mkubwa sana, leo ni siku ya 11 bado haijaonekana baharini au nchi kavu.
 
Sijui ukisema dunia si salama unamaanisha nini.

Ni lini dunia ilikuwa salama 100% kwa "in habitant" wake wote na lini dunia haikuwa 100% salama?

Sasa kama hujui, there is nothing as cruel as mother nature, ikiamua specie fulani i-perish, it will. Haijalishi kwa muda gani lakini lazima wapotee, refer cretaceous-Paleogene Extinction event, how cruel was it? 3/4 of animals and plants perished. Binadamu wana akili ndio, lakini kuna vitu katika nature hawawezi control.

Yaani kama usalama wa dunia unaupima kwa kupotea kwa ndege ya Malaysia tu nitakushangaa. Ni vyombo vingapi vya usafiri vilipotelea Bermud Triange? Na ilikuwachukua muda gani kugundua? Je, tuseme kuwa dunia haijawahi kuwa sehemu salama ya kuishi?

Off course kama tunajilinganisha na mataifa makubwa, huu usalama wa conspiracy za kiteknolojia, the fittest will survive
 
Hiyo ndege imemtisha hata Jk naona ameamua kutulia home kimyaaa
 
unaposema usalama wetu una maanisha nini? Kwasababu kwa mtazamo wangu nazan hii ni ajali kama ajali zingine and there is nothing u can do abt it bcz accident happens, ila kama unazani ni mambo ya kigaidi basi kwa nchi kama yetu tuko hatarini zaidi
nina maanisha ulinzi na usalama wetu kama watanzania, Do you think is normal accidents? mbona hatupata hata baki lolote la hiyo ndege kama ni normal accidents. Ni kweli sisi tupo kwenye hatari zaidi kama ni kweli ugaidi, kwa sababu tunategemea sana mataifa ya nje kwa kila kitu, au unasemaje mrsleo?
 
Wasiwasi wangu usikute imetekwa kwa ajili ya kuitumia kama silaha.

kama kusudi ndilo hilo itakuwa hatari sana. Hatari itakuwa kubwa kama imetua sehemu na watekaji wakapata nafasi ya kuijaza silaha za maangamizi.

Na wakaiwekea vifaa vingine vya kuondoa utambulisho wa awali na kuibadilisha rangi na kuweza kuruka tena juu.

Ijulikane hawa watekaji hawatakuwa wakiogopa kufa. Na hata kama ni kuizuia kwa kuitungua bado hatari itakuwa kubwa kwani huwezi kujua kuwa itaangukia wapi,

ni kweli kabisa dunia siyo salama kwa sasa. Hofu kubwa ni kama imetekwa , watekaji watakuwa ni wataalamu wa hali ya juu.

Maswali ya kujiuliza bado ni mengi sana, kwani kuna utata mkubwa sana, leo ni siku ya 11 bado haijaonekana baharini au nchi kavu.
hiyo ndiyo inayoonyesha wasiwasi duniani, yaani kuitafuta hii ndege imekuwa kama changamoto za kutafuta dawa ya UKIMWI
 
Sijui ukisema dunia si salama unamaanisha nini.

Ni lini dunia ilikuwa salama 100% kwa "in habitant" wake wote na lini dunia haikuwa 100% salama?

Sasa kama hujui, there is nothing as cruel as mother nature, ikiamua specie fulani i-perish, it will. Haijalishi kwa muda gani lakini lazima wapotee, refer cretaceous-Paleogene Extinction event, how cruel was it? 3/4 of animals and plants perished. Binadamu wana akili ndio, lakini kuna vitu katika nature hawawezi control.

Yaani kama usalama wa dunia unaupima kwa kupotea kwa ndege ya Malaysia tu nitakushangaa. Ni vyombo vingapi vya usafiri vilipotelea Bermud Triange? Na ilikuwachukua muda gani kugundua? Je, tuseme kuwa dunia haijawahi kuwa sehemu salama ya kuishi?

Off course kama tunajilinganisha na mataifa makubwa, huu usalama wa conspiracy za kiteknolojia, the fittest will survive
sisi kama binadamu tunafikiri nadhani hata wewe umekiri kuwa binadamu wana akili, lakini linapotokea tatizo kama hili lazima tutumie akili zetu kufikiri, hatuwezi kukaa kimya eti kwa sababu ndege ya Malaysia imepotea.

Kuna changamoto nyingi ambazo zinafanya dunia isiwe salama, mfano magonjwa, terrorism, Vita, Kugombania rasilimali nk.
Nadhani kuzungumza changamoto ni nzuri zaidi kuliko kukaa kimya, au kwa vile Malaysia haituhusu? Au tutabaki tunafikiria tu bila kutoa majibu ya suluhisho....Lets us discuss and see if its relevant to our context especially technologically.
 
Back
Top Bottom