Dunia ni zaidi ya tuijuavyo, cheza salama

Dunia ni zaidi ya tuijuavyo, cheza salama

Myahudi Jr II

JF-Expert Member
Joined
Jan 7, 2016
Posts
6,988
Reaction score
9,213
Habarini ndugu zanguni, poleni sana na mahangaiko ya dunia hii siku zote kumbuka mpaji ni MUNGU pekee.

Leo katika pita pita zangu za vijiweni na story za hapa na pale kulingana na story tulizokua tunapiga nikaikuta nimeseama “…..nikioa na mke wangu akiwa mjamzito nitampeleka akajifungulie kwao, maana siku hizi nasikia wadada wengi hawana Uhuru na nyumbani kwa mama mke…..” Mzee mmoja akanisikiliza sana kwa makini akasema “……kijana usijaribu huo mchezo, Mkeo ajifungulie kwako, tena ikiwezekana mtoto asionekane na mtu hadi zipite siku 40 akiwa ameshakua kila mahali kwa mwili na kitovu kitakua kimekauka……..”

Ndugu zanguni, nimeshangaa sana sana sana, mzee akaendelea kusema, kuna watu na viatu dunia hii akaongezea dunia tambara bovu, akasema unapompeleka mke kule kwao/kwenu watu wengi wanaokuja kumuona mtoto si wote wenye nia nzuri na mtoto, wengine wanakuja kutazama nyota ya mtoto afu wanamchukua wewe unaachiwa roboti linalopelekwa tuu, NIMEBISHA SANA

Mzee akaendelea akasema kijana wangu ulimwengu wa roho ni mmoja, akatoa mfano unakuta mtu ana akili sana lakini maisha yake utamuonea huruma n.k,n.k akaendelea akasema watu wanaoenda kwa mganga kupata kitu Fulani usidhani ni kwamba mganga anavyo hivyo vitu HANA, kwakua ulimwengu wa roho ni mmoja acnachofanya anaita mapepo/majini. How?

Ni hivi amesema, daily routine ya mwanadamu inakua recorded kila kitu (chochote unachofanya kinarekidiwa) upande wa shetani kivyake na MUNGU kivyake, so shetani anajua kila kitu kuhusu wewe hadi vipawa ulivyopewa na Mungu anajua hivyo ni rahisi kwake kujua wewe ni nani wa baaadae na unafaa kwa kipi na nyota yako ni ipi.

Sasa mapepo/majini yale yanakua na taarifa za kila mtu, mganga yule yeye anamsikiliza mteja wake anataka kitu gani, sio kwamba mganga anavyo, hata yeye HANA HATA KIMOJA anachofanya yeye anaingia kwenye ulimwengu huo wa roho anaangaza huyu mteja anataka nini anaita mapepo/majini yale yanajua kitu Fulani kipo kwa mtu Fulani so kinachofanyika ni kupokonywa nyota yako na kupewa yule mtu na wewe utabaki ukihangaika na kusumbuka chini ya jua hili kumbe umeibiwa zamani sana, mzee alikiri NI MUNGU TU ANAEWEZA KUIRUDISHA HAKUNA MWINGINE

Sasa unakuta mtu ni Inperation speaker mzuri san asana sana, asee kumbe amepokonya nyota ya mtu huko na anajua kabisa kuwa hii si yangu, mzee akasema wanailinda kuliko ulinzi wa raisi ikulu, wengine wanaenda hata kuzifungia nje ya nchi, wengine wanazitumia tu pale wanapokua na shughuli hiyo huiska wakimaliza tu wanairudisha kwenye ulinzi.

Mzee akasema, unakuta mtu ameenda kutafuta nyota za watu hata 5 anazo anazitumia tu.sasa kinachotokea watu siku hizi wanaiba nyota za watoto wanaozaliwa kwa kuwa watu wengii sana chini ya jua hili wameshaibiwa ko wakienda kuanganza wanakuta wengii wamechukuliwa nyota zao, akamaliza kwa kuniasa MKEO AZALIE KWAKO MWANANGU.

HAKIKA DUNIA NI ZAIDI YA TUIJUAVYO

Cc: Mshana Jr
 
Kwa dunia ya sasa ni bora mkeo akikalibia kujifungua mama yako ndo atoke kijijini aje kumuhudumia mzazi akiwa kwako. That might be a wise decision vinginevyo hayo uliyotaja yanaweza kukuta.
 
Hapo kwako watu wenye nia mbaya hawawezi kuja mkuu??..

Wanaweza ila si rahisi kama kwenu, umekulia home kila mtu anakujua wenye chuki na wenye kinyongo na wewe wanaweza kuja kwa wema kumbe ndani ni mbwa mwitu
 
Marekebisho kidogo, ni vema “azalie” kituo cha afya (kama unamaanisha kujifungua).... mnaweza kuendelea.

Yaani anaenda kujifungulia nyumbani, sijui kama naeleweka, yaani akizaa huduma zile anapewa nyumbani sio kwa mume wake
 
Hao watu wakitaka si hata hapo kwako watakuja kuichukua kama kweli? Au akijifungulia kwako utawafukuza watu wasije muuona mwanao?
 
Back
Top Bottom