ANDIKO LA ZIADA.
Kuna watu hudhani mitetemo humsaidia mtu katika kukabiliana na mambo ya kiroho tu ila kiuhalisia ni kwamba mitetemo huwa inabeba taswira ya maisha kamili ya mtu.
Kwa maana ya kwamba jinsi ambavyo utatengeneza muingiliano na watu wengine, jinsi ambavyo utakwenda kukabiliana na changamoto mbalimbali za kimaisha na kadhalika.
Na kitu ambacho unatakiwa ujue ni kwamba kama unavyoona uwepo wa ndugu wa damu basi pia unapaswa ujue ya kwamba wapo ndugu wa kiroho.
Sasa, ndugu wa damu ni watu mnaotokea ukoo au familia moja ila ndugu wa kiroho ni watu ambao mnatokea kwenye mfumo nyota wa aina moja.
Achana na ile ya ndugu zangu katika imani ya kwamba ndugu zangu katika uislam au ndugu zangu katika ukristo, hiyo ipo kwenye upande huo wa kuamini ustaarabu mfanano wa namna ya kufanya ibada.
Ila ninaposema ndugu wa kiroho namaanisha utimilifu zaidi uliopo upande wa pili wa mtu kwa maana ya upande ule wa kiroho ukiachana na huu wa damu na nyama.
Okay, ndugu zako wa kiimani utawajua kwakua wote huwa mnashiriki ibada kwa pamoja kwa maana ya msikitini, kanisani au kilingeni na hata kwenye mahekalu mbalimbali lakini pia ndugu zako wa damu utawajua kupitia vinasaba mfanano vilivyopo kwenye damu zenu.
Ila ndugu zako wa kiroho huwezi kuwajua kwa njia hizo au kwa kuwaangalia bali kwa ishara za ndani ambazo huwa zinakawaida ya kubadili sifa ya mtu iliyozoeleka kwa watu wanaomzunguka kwenda kwenye sifa nyingine ambayo haijazoeleka sana kutoka kwake.
Na hili ni wewe mwenyewe unaweza kulisoma au watu wanaokujua wanaweza kulisoma ya kwamba kuna hali isiyo ya kawaida ya kitabia imeanza kujionyesha kwako juu ya mtu mwingine.
Labda ukiwa nae unajikuta unakua dhaifu sana kihisia au unajikuta unamjali isivyo kawaida na mambo kama hayo.
Angalia, kuna watu ambao wanasifika kuwa na roho ya kutokujali wengine na watu wenye utata mwingi kwa wengine kwa maana si watu wenye kunyenyekea watu ila ni watu fulani hivi ambao ni wakali wakali or wenye kutokuzoeleka sana kwa wengine.
Lakini utashangaa baada ya muda fulani anatokea mtu mmoja ambae anakuja hapo mtaani au nyumbani kwenu na anamfanya huyo jamaa mtata abadilike isivyo kawaida, kwahiyo utakuta anakua mnyenyekevu na mtu mwenye kusikiliza Kila neno analoambiwa na huyo mtu mpya hapo mtaani na unakuta ni watu ambao wakikaa wanapiga story na kufurahi isivyozoeleka (kwa hali hii watu husemaga Kila shetani na mbuyu wake)
Sasa hii ni ishara ya kwamba watu hao wanatokea kwenye mfumo nyota unaofanana na kinachofanya mmoja awe anasikiliza au mnyenyekevu sana kutoka kwa mwenzie ni utimilifu uliopo kwenye mitetemo yao.
Mtu aliye na utimilifu wa juu kwenye mitetemo huwa anakua na uwezo wa kuwacontrol wengine wote waliochini yake kiutimilifu kutoka kwenye huo mfumo nyota unaofanana kama vile ilivyo wewe na kaka yako au dada yako kwa maana yule mkubwa ndio anaeweza kuwacontrol wadogo zake.
Na hii huwa ni mbaya sana au nzuri sana hasa inapoingia kwenye upande wa mahusiano ya kimapenzi kwa maana watu wa namna hii wanapokutana ili kuanzisha mahusiano ya kimapenzi huwa muunganiko wao unakua ni wa kudumu.
Na atakaekua anamuendesha mwenzake kwenye hayo mahusiano ni yule ambae anakiwango kizuri cha utimilifu kwenye mitetemo yake.
Kwahiyo kama huyu mwenye utimilifu atakua ni mtu asiyejali basi huyu mwingine ndie ambae ataumia sana kimapenzi.
Anaweza akalia na kuapa miungu yote ya kwamba ataachana na huyo mtu wake ila once wakionana ana kwa ana anakua hana usemi na anajikuta tu anapoa isivyo kawaida na anasahau yote aliyotaka kuyafanya na badala yake ataanza kuskiliza tena na kufuata hizo orders anazopewa.
Hii hata kwa wale magwiji wa mapenzi yaani wale ambao hawajawahi kuumia kimapenzi au hawajawahi kupenda kihivyo wanapokutana na watu wa namna hiyo huwa wanaweza hata kujiua ikitokea wameachwa, kwa maana unajikuta unampenda mtu isivyo kawaida na hata kama ulikua hauongi ila unajikuta unahonga na unajikuta uko ladhi kufanya jambo lolote ili mahusiano yenu yaendelee kudumu.
Na ikitokea watu wa hivi wameachana basi sababu ni yule ambae mitetemo yake iko na utimilifu na siku akisema arudi basi penzi linarudi upya bila kujali chochote.
Kwahiyo ikiwa umeoa au kuolewa na mtu ambae alishawahi kukutana na mtu anaetokea kwenye mfumo nyota unaolingana na yeye na ikatokea wametengana kwasababu za hapa na pale Kaa ukijua hao wakikutana wanayafanya yote yale ambayo walizoea kuyafanya.
Na aliyerudi akiamua kutangaza ndoa basi wewe utaachwa kwenye mataa umetulia zako.
Kwa maana kimsingi na kiutaratibu hawa ndio watu ambao waliumbwa kuja kulifanya hilo agano la ndoa pamoja duniani, ule utimilifu unapatikana kwa watu wa namna hiyo hasa ikitokea ule utimilifu wao wa kimitetemo haujaachana sana.
Kwa maana hiyo basi, watu wa hatima yako huwa mara nyingi wanatokea kwenye hili kundi.
Katika namna yoyote ya kimaisha, iwe kirafiki, kimahusiano ya ndoa au kazi au kusaidiana na kadhalika.
(Si Kila mtu anaweza akakusaidia au si Kila mtu anaweza akasaidiwa na wewe, unaweza ukawiwa kumsaidia mtu mwenye uafadhali wa maisha na ukashindwa kumsaidia mtu ambae hana uafadhali wowote wa maisha, mtu ambae aliwahi kumsaidia rafiki yako kwa tatizo mfanano na lile ulilonalo wewe hivi sasa anaweza akashindwa kukusaidia wewe hata kama anao huo uwezo wa kukusaidia, kwahiyo usinune au kulalamika kwa maana huo ni utaratibu wa kawaida wa ulimwengu).
Kwahiyo ukiwa vizuri kimitetemo na ikatokea umepata changamoto au umekwama kwenye eneo fulani wakati unaendelea kupiga hatua za kuelekea kwenye hatima yako, hizo hisia zako za kuwaza Kila siku jambo hilo kinamna chanya itamuibua mtu fulani mnaetokea mfumo nyota unaofanana na ambae anaouwezo wa kukutatulia hiyo changamoto.
Na hii itakua kinamna ile ile ya kimawimbi kama ilivyo kwa mawimbi ya redio au simu inavyozingatia network ili iweze kuunganisha mawasiliano.
Kwahiyo kupitia hiyo changamoto yako ambayo huwa unaiwaza au kuimeditate kinamna chanya sana huwa inapelekea mtu mmoja aweze kutoka kwenye comfort zone yake au wewe mwenyewe uweze kutoka kwenye comfort zone yako ili aweze kukutana na wewe au wewe kukutana na yeye kwa lengo la kutatua hiyo changamoto yako.
Kuna hali fulani zisizotarajiwa huwa zinatokea kwa watu ya kwamba mtu anajikuta ghafla tu anaanzisha safari ambayo haina umuhimu wowote kwake, yaani unaweza ukajikuta uko nyumbani umetulia mara ghafla unajiwa na hisia za kwenda eneo ambalo hukuliwazia hapo kabla na hata ukiulizwa kwa nini unaenda au umeenda hapo huwi na jibu la kueleweka zaidi ya lile la kutembea tu.
Na unapokua kwenye hayo maeneo ghafla unaweza ukakutana na mtu ambae ako na changamoto fulani ambayo iko ndani ya uwezo wako na kweli unajikuta unawiwa kuitatua na ukishaitatua basi unakaa Kaa na unarudi ulikotoka.
Au yule mtu ambae ako na changamoto inayohitaji kutatuliwa anaweza akakaa na ghafla akapata hamasa ya kujianzishia safari au kuna jambo linatokea kwenye mazingira yake na kujikuta anakua kwenye safari fulani na anapokua kwenye hiyo safari anakutana na mtu ambae wanaconnect kwa haraka sana na kupitia huyo mtu changamoto zake zinapata utatuzi.
Kuna watu wamelia sana juu ya kuoa au kuolewa ila siku isiyojulikana wakajikuta tu ghafla wanaanzisha safari na kwenye hiyo safari wanakutana na watu ambao pengine waliwachukulia kuwa kama watu wakawida kama walivyokua wengine ila mwisho wa siku katika hali isiyotarajiwa wanajikuta vile vilio vyao vya kuoa au kuolewa vinapata ufumbuzi kupitia watu hao.
Kwahiyo kuna nyakati ambazo vitendo hivi huwa vinapendeza ila pia kuna nyakati ambazo vitendo hivi havipendezi kwa maana kuna nyakati ambazo wewe na ndugu yako wa kiroho mnajikuta mnatimiza hatima zenu kwa pamoja ila kuna nyakati mmoja anajikuta anatumika kutimiza hatima ya mwingine bila kupenda au kujua.
Kuna watu ambao wako na utimilifu imara sana kwenye mfumo nyota wao, hawa watu wamekua wakiwatumia sana watu wengine ili wao waweze kusonga mbele pasipo wao wenyewe kujua.
Kwa mfano, kuna watu walikua na maisha mazuri, kazi nzuri au biashara iliyosimama ila kuna sintofaham ikatokea kwenye maeneo yao ya kazi au biashara iliyowafanya wao wenyewe waichukie hiyo kazi au biashara na kujikuta wanakimbia kwenda kwenye mji mwingine na huko wanaenda kukutana na mtu fulani atakae watumia kutekeleza hatima yake.
Na mambo haya yote huwa yanatokea kwenye msimu wa mabadiliko ya kihatima ambayo mtu hukutana nayo pale anapohama kutoka kwenye stage moja kwenda kwenye stage nyingine itakayomsogeza karibu ya hatima yake zaidi au kumrudisha nyuma zaidi.
Sasa, kuna watu ambao wanatoka kwenye comfort zone zao na kwenda kwenye maeneo mengine wasiyoyatarajia kwasababu hatima zao zinahitaji njia za namna hiyo ili ziweze kutokea ila kuna watu ambao wanahama kwa kutoka kwenye comfort zone zao na kwenda kwenye maeneo wasiyo yatarajia kwasababu kuna mtu kwenye hilo eneo hatima yake inamuhitaji huyo aliyetoka kwenye comfort zone yake na kwenda kwenye hilo eneo, kwahiyo yeye amepatikana wakati mitetemo inatafutana kiasi cha kumfanya aweze kutoka kwenye eneo lake la kujidai kwenda kwenye eneo asilolitegemea ili mtu fulani kwenye eneo hilo aweze kupiga hatua kupitia yeye.
Na unapoingia kwenye kipindi hiko cha mabadiliko ya kihatima, huwa hasi na chanya zinakua karibu sana.
Na ikiwa lengo ni kukutoa kwenye eneo lako la kujidai basi lazima sababu iwepo itakayosababisha wewe uweze kutoka kwenye hilo eneo bila kulazimishwa na mtu yeyote yule.
Na kwenye hizo sababu huwa zinaweza zikatokea upande chanya au upande hasi kutegemeana na nguvu ya usababishi itakua ipo upande gani kati ya pande hizo mbili.
Sababu hizo za kukufanya utoke kwenye eneo lako la kujidai kwanza zitaanza kutafutwa ndani yako kisha nje yako kwa maana kwa watu ambao wamekuzunguka au vitu ambavyo vimekuzunguka na ile ambayo iliandaliwa au wewe mwenyewe uliiandaa kwaajiri ya hayo mabadiliko pasipo wewe kujua basi itatumika kukufanya utoke kwenye hiyo comfort zone yako bila kupenda.
Nilisema hatima ni kama puzzle na puzzle hii ya hatima huwa inatatuliwa kwa mambo madogo madogo ambayo mtu anakabiliana nayo Kila siku.
Na ndio maana nikasema haupaswi kuchukulia mambo poa poa kwasababu duniani hakuna jambo linalompata au kukabiliana na mtu kibahati mbaya.
Kila jambo ambalo linakutokea Kila siku huwa linaathari fulani kwenye puzzle yako ya kuelekea kwenye hatima.
Inawezekana ikaja kuwa athari chanya au athari hasi na ndio maana swala la uhuiswaji si swala ambalo ni rahisi kuweza kulifikia.
Haijalishi unataka uhuishwe kinamna chanya au kinamna hasi ila kwenye namna zote hizo huwa uhuiswaji haupatikani kirahisi.
Kwahiyo, mambo yote ambayo umeyatunza ndani yako kama siri kwa maana mengine ni mambo ya aibu na siku yakija kujulikana basi unaweza kuonekana mtu wa hovyo kuwahi kutokea kuna siku moja hayo mambo yanaweza kuja kutumika kama chambo ya kukutoa kwenye eneo lako la kujidai ili uweze kwenda kwenye eneo lingine kwaajiri ya kupiga hatua zaidi ya kihatima au kwenda kumpigisha mtu mwingine hatua za hatima yake.
Kwenye misimu ya namna hiyo huwa hakuna kubembelezana, bila kujali ni hatua yenye faida kwako au yenye faida kwa mwingine ni kwamba universe ikisema unatakiwa utoke kwenye comfort zone yako ni unatoka tu tena bila hata kubembelezwa ila ni wewe mwenyewe utahaha sana ili uweze kutoka hapo kwa maana kutoka hapo ndio unafuu wako.
Ingawa kuna wengine huwa wanapitia hizo hatua kiugumu ugumu sana kutokana na ukosefu wa visababishi vingi ambavyo viko ndani yao kwahiyo mazingira ya nje huwa yanalazimishwa kuingilia kati ili visababishi viweze kupatikana kwaajiri ya kuwafanya watoke hapo.
Na mazingira ya nje yanapolazimishwa ili yaweze kuleta visababishi yanaweza yakaleta kwa namna yenye kuleta maumivu au ya kumfanya mtu akose uhuru wa kuishi kwenye hayo mazingira aliyoyazoea.
Ila kama uko na siri zako nzito za aibu ambazo umezitunza humo ndani yako na ikiwa zinafaa kutumika kukuondoa hilo eneo basi haraka sana siri inafichuka unajikuta uchi mtaa mzima au ofisi nzima na unaanza kuhaha na kujikuta unapata wazo la kuhama hapo uende eneo fulani ambalo litakua hapo kichwani mwako na hilo ndio litakua eneo lengwa kwako.
Yes, najua ni mambo yanayoshangaza ila huu ni utaratibu wa kawaida wa dunia kwasababu Dunia ni uwanja wa vita vya hatima kwahiyo ni lazima ubongo wako uwe active muda wote kwa maana tupo hapa kwaajiri ya mission maalumu kwahiyo Kila siku unapaswa ukabiliane nayo ukiwa ubongo wako unafanya kazi kwa utimamu wa juu sana.
Kuna hadithi za kihatima kwenye maandiko, ile ya Yakobo(Yakubu), ile ya Yusufu, ile ya Ayubu na hata ile ya Musa.
Ukiangalia hadithi ya Yakobo au Yakubu utaona kwamba ni mtu ambae hakuwa na exposure yoyote na ulimwengu uliomzunguka kwa maana alikua ni mtoto wa mama sana, ila msimu wa mabadiliko ya upigaji hatua kuelekea hatima yake uliposogea na kutakiwa atoke kwenye comfort zone yake basi ile hali ya uongo iliyopo ndani mwake ikatumika kuweza kumtoa kwenye hilo eneo baada ya kuzuka ugomvi wa kutaka kuuana kwa mapanga yeye na kaka yake kwahiyo ikabidi akambilie kwa mjomba wake na huko alienda kutumika kwaajiri ya hatima ya mjomba wake lakini pia na yeye hatima yake ilihitaji njia hiyo.
Yusufu alijikuta kwenye nchi ya mbali bila yeye kutarajia na hii yote ni kutokana na ule msimu wa hatima yake ulipohitaji mabadiliko ya kutoka kwenye comfort zone yake ulipofika, basi ndugu zake wakatumika ili yeye hatima yake itimie.
Musa alifanya jambo jema kutoa msaada baada ya kuua mtu aliyekua akimuonea mwingine na hilo likawa ni agano la siri baina yake na yule aliyemsaidia ila mabadiliko ya kihatima yalipofika ile siri ikafichuka na kujikuta anakwenda eneo la mbali bila kupenda ila huko ndiko ambako hatima yake ilienda kuanza.
Ayubu, mtu tajiri ambae ilitakiwa atolewe kwenye comfort zone yake ili ile hatima ya unyenyekevu iliyo ndani yake iweze kufikiwa.
Kwahiyo jitahidi sana uwe chanya siku zote ili uendelee kuimarisha mitetemo yako kwa maana bila hivyo unaweza ukatumika sana kutimiza hatima za watu wengine bila ya wewe mwenyewe kujua au kupenda.
Lakini pia usisahau ya kwamba msimu wa mabadiliko unapokuja huwa hauchagui siraha kwahiyo jitahidi kubalance hizo siri unazozirundika ndani yako kwa maana kuna siku moja usiyoijua zitatumika kwaajiri yako wewe mwenyewe.
NITARUDI…