Dunia ina mambo...

The Donchop

JF-Expert Member
Jan 10, 2014
294
376
Habarini wadau?
Nimeshuhudia tukio la kusikitisha sana na kila mara ninalifikiria.
Iko hivi, mimi ni mpangaji mmoja wapo kati ya wapangaji watatu.
Kisa hiki ni juu ya mpangaji mwenzangu anayoyafanya wajameni.

Kuna binti mlemavu na pia ni yatima (baada ya kujua story yake ndipo nikajua kuwa ni yatima) Binti huyu mara kadhaa nilimkuta mlangoni kwa mshikaji. Ni sehemu yenye mbu kutokana na mazingira yalivyo lakini binti anamvumilia mshikaji hata saa sita usiku.

Ipo siku ambayo aliwahi kulala hapo nje mshikaji akiwa amelala ndani bila kumjali.
Katika kudodosa ni kwamba msichana alikuwa ni mpenzi wa huyu jamaa kabla ya huyu jamaa kuhamia kwake.

Mwanzo wa mapenzi yao, binti anadai jamaa alimpenda kweli na kumjali kwa kila hali. Kwa kuonyesha mapenzi yake, binti akawa akipata pesa kidogo anagawana sawa na mshikaji. Binti pamoja na ulemavu wake ni shupavu wa kutafuta pesa. Hana wazazi wala walezi wanaojua kula yake.

Huyu jamaa kwao yupo njema lakini bado alimkandamiza binti kwa maneno matamu na kuna muda alimpokonya kila senti aliyokuwa nayo huku yeye akitumia kwa starehe zake. Binti alivumilia na hata kushinda njaa ili huyu jamaa aweze kufurahi.

Jamaa alipotaka kuhama, alimuomba binti pesa za kulipia chumba kwa miezi sita. Binti akahangaika akijua wanayapanga. Jamaa alipopata pesa hizo, alipanga na hakutaka kumwonyesha binti wapi anaishi. Ilipita muda mrefu hadi binti alipopelekwa nyumbani kwa mshikaji tena kwa masimango.

Hapo ndipo akajua wapi mshikaji anaishi. Baada ya muda mfupi tu, mshikaji akamtema binti kwa maneno ya kejeli kuwa "yeye ni mlemavu na hakuna mwanaume atakayemuhitaji. Pia alikuwa nae kipindi ana shida na sio sasa. Hakuwahi kumpenda wala kuwa na ndoto nae." Binti sasa anatia huruma kwani anadai alikuwa akimpenda mshikaji kwa dhati.

Ndugu zangu, kuna watu wa kufanyiwa mabaya na kuchezewa, lakini kwa hawa mabinti ambao wanakuwa na mapenzi ya dhati na kuwasimanga kwa maneno makali, binafsi inaniuma sana. Mkimuona mshikaji ni kama mtu vile.

Kumbe ndani ni shetani. Nae anatuambiaga binti analazimisha upendo naye hamtaki. Hana sababu ya maana ambayo mnaweza kuielewa. Mungu yupo...
 
Hapo sielewi niwe upande upi kwakweli manake wote wana makosa.
Anyway, mpe pole sana huyo binti, then mwambie anyanyuke hapo apanguse makalio then arudi kwao(alikokuwa anaishi mwanzo) ili asiendelee kudhalilika
 
Kwa hiyo umekuja kumkandia kijana humu jf?? Nasema hivi; Huyo binti sio wa kwanza kujirahisisha kwa kijana. Acha huyu mlemavu, wapo wenye kwao na sura ka uji wa mbege lakini bado huji dhalilisha.
Mwambiye binti aende alikokuwa anakaa. aendelee na maisha kama siku zake zote. Atafute fedha yake ila achunge kwani muda sio mwingi jamaa atakuja akilia kwa yatakayo mpata. Dhulumu kila mtu ila usimdhulumu mwenye ulemavu kwa sababu yaulemavu wake. Hakuuomba kwa aliye muumba. Lazima jamaa apate balaa la kumfanya arudi kwa binti kwa machozi.
 
Sweet Dreams

Eurythmics

Sweet dreams are made of this
Who am I to disagree?
I travel the world
And the seven seas,
Everybody's looking for something.
Some of them want to use you
Some of them want to get used by you
Some of them want to abuse you
Some of them want to be abused.
Sweet dreams are made of this
Who am I to disagree?
I travel the world
And the seven seas
Everybody's looking for something
Hold your head up
Keep your head up, movin' on
Hold your head up, movin' on
Keep your head up, movin' on
Hold your head up
Keep your head up, movin' on
Hold your head up, movin' on
Keep your head up, movin' on
Some of them want to use you
Some of them want to get used by you
Some of them want to abuse you
Some of them want to be abused.
Sweet dreams are made of this
Who am I to disagree?
 
KARMA IS A BITCH

Things will turn over.
Mwambie aendelee kumuonea binti wa watu.
 
Ila kuna watu wana dhambi pia hajajua kwamba kuna usemi usemao hujafa hujaumbika ndio mana akawa na dharau kwa huyo dada wa watu.

Nadhani huyo mwanaume kashindwa kuwaza mbali ndio sababu, hivyo ni bora huyo mdada akafanya mambo yake ipo siku atapata anayempenda kwa dhati na kumthamini pia kwani siku zote mapenzi yapo na yataendelea kuwepo.
 
Kwa hiyo umekuja kumkandia kijana humu jf?? Nasema hivi; Huyo binti sio wa kwanza kujirahisisha kwa kijana. Acha huyu mlemavu, wapo wenye kwao na sura ka uji wa mbege lakini bado huji dhalilisha.
Mwambiye binti aende alikokuwa anakaa. aendelee na maisha kama siku zake zote. Atafute fedha yake ila achunge kwani muda sio mwingi jamaa atakuja akilia kwa yatakayo mpata. Dhulumu kila mtu ila usimdhulumu mwenye ulemavu kwa sababu yaulemavu wake. Hakuuomba kwa aliye muumba. Lazima jamaa apate balaa la kumfanya arudi kwa binti kwa machozi.
Nimejisikia huruma tu kwa anayotendewa. Kumvumilia mtu kwa miaka miwili, siku anapata neema anakimbiwa kwa maneno ya kejeli
 
Yaani wanawake wengi ambao ni yatima au kwao maisha magumu mno wananyanyaswa sana tena sana, vipigo nk. toka kwa waume zao. Inauma sana aisee!.
 
Kwa maekezo yako nimegundua unampenda uyo binti nami nakushauri mchukue tu si kaachwa
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom