Uwesutanzania
JF-Expert Member
- Feb 9, 2019
- 1,602
- 1,864
Ni mimi wako UWESUTANZANIA 🌍
Kusema ukweli sina siku nyingi sana tokea nimefika katika hii dunia, nina jumla ya wastani wa siku 10,800 sawa na miaka kama 30 hivi au 29.,
Kwenye kipindi chote nimekuwa hapa kuna mambo yameniacha kinywa wazi sana, naamini hata na wewe ndugu msomaji yapo mambo yamekushangaza kama itakupendeza utashiriki na mimi.
Jambo la kwanza (DINI)
Asilimia kubwa ya watu hufata mamlisho na sheria na vikwanzo kutoka kwenye Kiumbe kisichojulikana,.
Wanakiogopa na kukitii.
Wamekijengea majumba na kusema ni yake, wanakusanyika humo na kuzungumza naye aliyakuwa hawamuoni wala hawasikii sauti yake.
Kama wewe ni mgeni hapa duniani unaweza hisi ni wachache wenye kufuata hayo ila cha kushangaza ni wengi ndio wenye kufuata hayo na wachache sana ndio huwa hawafuatishi kwa yalio huko, na wenyewe wakisema huonekana watu wa ajabu sana.
Wanatumaini hupata chakura kutoka kwake, hupata mafanikio na hata pumzi waliyonayo ni kutoka kwake, wengine hufika mbali zaidi na kudai hata wakifa wataenda keti pamoja naye.,
Jambo la pili ujenzi (MAJUMBA)
Nimeona hili la kushangaza pia,
Watu wa duniani wamekuwa ni wenye kujenga majumba makubwa na yenye uimara wa wastani wa miaka 500 aliyakuwa wenyewe huishi miaka 90 na 100,. Wengi wao hufanya hivyo na wachache wasio fanya ujenzi huonekana ni watu wa ajabu na wasio na maana,.
Wengine hujenga kwa kusema ni kwa ajili ya vizazi vyao, ila cha kushangaza hata wasio zaa pia HUJENGA, je wajengea nini sijui.?
Jambo la tatu PESA ( FEDHA)
Hapa kwanza ncheke,
Duniani kuna vitu vyaitwa pesa. Viko vya kama vichuma chuma na viko vya mfananio na makaratasi.
Naam ni makaratasi kabisa, hayana maana yeyote wala faida.
Huwezi fanya andazi ukanywia chai wala huwezi tia kwenye mboga kama kitunguu,.
Ila cha kushangaza watu wamekuwa wakitoa macho mpaka kuuana hili nitaenda kukumbuka sana na nitaenda simulia haya maajabu ikiwa nitaondoka kwenye hii dunia.
Mwisho
Kwangu mimi DUNIA ni kama kisiwa nimeanguka na ndege baada ya ndege kupata ajali.
Jambo langu kubwa nafanya ni kutafuta msaada wa wavuvi na ndege za Hanga iliniweze kuondoka katika kisiwa hiki.
Siwezi kujenga wala kununua ardhi. Maana wakati wowote nikipata msaada basi nitakuwa ni mwenye kuondoka (KIFO)
Kusema ukweli sina siku nyingi sana tokea nimefika katika hii dunia, nina jumla ya wastani wa siku 10,800 sawa na miaka kama 30 hivi au 29.,
Kwenye kipindi chote nimekuwa hapa kuna mambo yameniacha kinywa wazi sana, naamini hata na wewe ndugu msomaji yapo mambo yamekushangaza kama itakupendeza utashiriki na mimi.
Jambo la kwanza (DINI)
Asilimia kubwa ya watu hufata mamlisho na sheria na vikwanzo kutoka kwenye Kiumbe kisichojulikana,.
Wanakiogopa na kukitii.
Wamekijengea majumba na kusema ni yake, wanakusanyika humo na kuzungumza naye aliyakuwa hawamuoni wala hawasikii sauti yake.
Kama wewe ni mgeni hapa duniani unaweza hisi ni wachache wenye kufuata hayo ila cha kushangaza ni wengi ndio wenye kufuata hayo na wachache sana ndio huwa hawafuatishi kwa yalio huko, na wenyewe wakisema huonekana watu wa ajabu sana.
Wanatumaini hupata chakura kutoka kwake, hupata mafanikio na hata pumzi waliyonayo ni kutoka kwake, wengine hufika mbali zaidi na kudai hata wakifa wataenda keti pamoja naye.,
Jambo la pili ujenzi (MAJUMBA)
Nimeona hili la kushangaza pia,
Watu wa duniani wamekuwa ni wenye kujenga majumba makubwa na yenye uimara wa wastani wa miaka 500 aliyakuwa wenyewe huishi miaka 90 na 100,. Wengi wao hufanya hivyo na wachache wasio fanya ujenzi huonekana ni watu wa ajabu na wasio na maana,.
Wengine hujenga kwa kusema ni kwa ajili ya vizazi vyao, ila cha kushangaza hata wasio zaa pia HUJENGA, je wajengea nini sijui.?
Jambo la tatu PESA ( FEDHA)
Hapa kwanza ncheke,
Duniani kuna vitu vyaitwa pesa. Viko vya kama vichuma chuma na viko vya mfananio na makaratasi.
Naam ni makaratasi kabisa, hayana maana yeyote wala faida.
Huwezi fanya andazi ukanywia chai wala huwezi tia kwenye mboga kama kitunguu,.
Ila cha kushangaza watu wamekuwa wakitoa macho mpaka kuuana hili nitaenda kukumbuka sana na nitaenda simulia haya maajabu ikiwa nitaondoka kwenye hii dunia.
Mwisho
Kwangu mimi DUNIA ni kama kisiwa nimeanguka na ndege baada ya ndege kupata ajali.
Jambo langu kubwa nafanya ni kutafuta msaada wa wavuvi na ndege za Hanga iliniweze kuondoka katika kisiwa hiki.
Siwezi kujenga wala kununua ardhi. Maana wakati wowote nikipata msaada basi nitakuwa ni mwenye kuondoka (KIFO)