Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,054
- 463,870
SEHEMU YA 01 -Erick Shigongo
“Mume wangu! Naomba unisamehe!”
“Nikusamehe! Mara ngapi? Nahisi hunijui! Sasa subiri.”
“Mume wangu naomba unisamehe! Sitorudia tena!”
“Eti hutorudia! Unanifanya mimi mjinga! Leo nataka nikuonyeshee, utajua kwa nini Mungu alianza kumuumba Adamu kabla ya Hawa.”
Zilikuwa ni kelele kutoka katika nyumba moja chakavu iliyokuwa katika Mtaa wa Tandale kwa Tumbo jijini Dar es Salaam. Watu waliokuwa wakipita nje ya nyumba hiyo, walisimama na kusikiliza kile kilichokuwa kikiendelea.
Hiyo haikuwa mara ya kwanza, kila siku kulikuwa na fujo ndani ya nyumba hiyo waliyokuwa wakiishi watu wawili tu, Godwin Mapoto na mwanamke mrembo aliyewahi kutikisa kutokana na urembo wake, Winfrida Michael.
Kelele zile ziliendelea kuwakusanya watu wengi nje ya nyumba hiyo. Wale waliokuwa ndani ya nyumba zao, wakatoka na kwenda kusimama karibu kabisa na nyumba hiyo.
Hakukuwa na mtu aliyediriki kuingia ndani kugombelezea kwani walimfahamu Mapoto, japokuwa alionekana kuwa mwanaume dhaifu, mwenye mwili mwembamba lakini alivuma kutokana na ubabe wake mtaani hapo.
Alikuwa mwanaume wa fujo, aliyetikisa kuanzia Kwa Tumbo, Kwa Mtogole, Yemen mpaka Mwananyamala kwa Manjunju. Watu wengi walikuwa wakimuogopa, jina lake lilikuwa likivuma sehemu kubwa kuanzia Tandale, Mwananyamala mpaka Magomeni Kondoa.
Alikuwa mbabe wa mtaa kiasi kwamba watu walihisi kwamba asingekuja kuwa na mwanamke mrembo kutokana na ubabe wake, lakini kitu kilichowashangaza ni kwamba alifanikiwa kumnasa msichana aliyekuwa na sura nzuri, ya kipole, umbo matata, Winfrida Michael, msichana aliyekuwa akikubalika katika Chuo cha St. Joseph alipokuwa akisomea biashara.
Chuoni hapo, Winfrida alitingisha kwa uzuri, kila mwanaume alikuwa akimzungumzia yeye, alipokuwa akitembea, watu walimfananisha na twiga huku macho yake yakiwa na mvuto mithili ya mwanamke aliyekula kungu.
Hakuwa msichana mwepesi, alikuwa mgumu, wanaume walimfuata na kumtaka kimapenzi lakini Winfrida hakukubaliana nao hata kidogo.
Kila walipokuwa wakizungumza naye, alionyesha tabasamu kubwa kiasi kwamba liliwapa matumaini wanaume wengi lakini jibu lake halikufanana na tabasamu alilokuwa akilitoa usoni mwake.
“Nimekuelewa,” alisema Winfrida.
“Mume wangu! Naomba unisamehe!”
“Nikusamehe! Mara ngapi? Nahisi hunijui! Sasa subiri.”
“Mume wangu naomba unisamehe! Sitorudia tena!”
“Eti hutorudia! Unanifanya mimi mjinga! Leo nataka nikuonyeshee, utajua kwa nini Mungu alianza kumuumba Adamu kabla ya Hawa.”
Zilikuwa ni kelele kutoka katika nyumba moja chakavu iliyokuwa katika Mtaa wa Tandale kwa Tumbo jijini Dar es Salaam. Watu waliokuwa wakipita nje ya nyumba hiyo, walisimama na kusikiliza kile kilichokuwa kikiendelea.
Hiyo haikuwa mara ya kwanza, kila siku kulikuwa na fujo ndani ya nyumba hiyo waliyokuwa wakiishi watu wawili tu, Godwin Mapoto na mwanamke mrembo aliyewahi kutikisa kutokana na urembo wake, Winfrida Michael.
Kelele zile ziliendelea kuwakusanya watu wengi nje ya nyumba hiyo. Wale waliokuwa ndani ya nyumba zao, wakatoka na kwenda kusimama karibu kabisa na nyumba hiyo.
Hakukuwa na mtu aliyediriki kuingia ndani kugombelezea kwani walimfahamu Mapoto, japokuwa alionekana kuwa mwanaume dhaifu, mwenye mwili mwembamba lakini alivuma kutokana na ubabe wake mtaani hapo.
Alikuwa mwanaume wa fujo, aliyetikisa kuanzia Kwa Tumbo, Kwa Mtogole, Yemen mpaka Mwananyamala kwa Manjunju. Watu wengi walikuwa wakimuogopa, jina lake lilikuwa likivuma sehemu kubwa kuanzia Tandale, Mwananyamala mpaka Magomeni Kondoa.
Alikuwa mbabe wa mtaa kiasi kwamba watu walihisi kwamba asingekuja kuwa na mwanamke mrembo kutokana na ubabe wake, lakini kitu kilichowashangaza ni kwamba alifanikiwa kumnasa msichana aliyekuwa na sura nzuri, ya kipole, umbo matata, Winfrida Michael, msichana aliyekuwa akikubalika katika Chuo cha St. Joseph alipokuwa akisomea biashara.
Chuoni hapo, Winfrida alitingisha kwa uzuri, kila mwanaume alikuwa akimzungumzia yeye, alipokuwa akitembea, watu walimfananisha na twiga huku macho yake yakiwa na mvuto mithili ya mwanamke aliyekula kungu.
Hakuwa msichana mwepesi, alikuwa mgumu, wanaume walimfuata na kumtaka kimapenzi lakini Winfrida hakukubaliana nao hata kidogo.
Kila walipokuwa wakizungumza naye, alionyesha tabasamu kubwa kiasi kwamba liliwapa matumaini wanaume wengi lakini jibu lake halikufanana na tabasamu alilokuwa akilitoa usoni mwake.
“Nimekuelewa,” alisema Winfrida.

