Mr_S
Senior Member
- Apr 2, 2022
- 108
- 88
Habari za muda huu wanachama wa jukwaa la Biashara.
Nimekuja kwenu leo hii nikihitaji dira ya wapi ni pazuri zaidi kwa biashara ya duka la mangi kati ya Kahama au Tunduma.
Kwa kifupi nimefanya ajira Arusha kwa muda mrefu sana, takribani miaka miwili nikaacha na kuanza kuuza duka la Mangi hapa Usariver. Kwa ujumla biashara ilikuwa ya kawaida, ilikuwa na siku nzuri na siku zilizokwenda tofauti. Lakini nimefikia mkataa wa kwamba nataka kutafuta changamoto MPYA na kubadili mazingira. Nataka kuondoka hapa Arusha na kwendA KAHAMA au TUNDUMA.
Nimechagua hizo sehemu mbili kutokana na kusifika kuwa na mzunguko wa biashara. Hata hivyo ni ngumu kwangu kuamua wapi HASA pa kwenda kutokana na ukweli kwamba SIJAWAHI kufika popote kati ya sehemu hizo, sijui gharama za maisha na aina za biashara ambazo zinakubali sana huko. Lakini pia maamuzi yangu yanatiwa ukakasi na mambo yafuatayo ambayo yamesemwa sana na watu kuhusu sehemu hizo.
1. Nikisema ntaamua kwenda Tunduma basi napata ukakasi kila nikikumbuka mambo ambayo watu wanasema kuhusu mahali hapo kwamba kwanza hakuna maji, miundombinu duni na ni "sehemu ambayo biashara pekee inayokubali ni MAGENDO tu! eti biashara nyingine zote zinafeli labda uwe na mtaji mkubwa".
2. Nikisema niende Kahama basi wazo langu litatiwa ukakasi na uvumi kwamba eneo hilo lina mzunguko kutokana na mgodi wa buzwagi. Kwamba siku ambayo mgodi huo utafungwa sehemu hiyo itapoteza kila kitu kutia ndani watu na mzunguko uliopo hapo. Ukizingatia hivi karibuni kumekuwa na seke seke la kwamba siku inakuja ambapo wachimbaji wadogo wataondolewa na migodi itafungwa. Nawaza vipi nikifika pale nikajiwekeza na kabla biashara haijachanganya "migodi ikafungwa ?", Ntakuwa nimeangukia pua.
Wataalamu, wenyeji na wajuzi wa haya maeneo naomba muongozo wenu ili nifanye maamuzi yenye 'low risk', nataka nifanye shughuli ya duka la mangi na mipango yote ya kuhama ilishaanza, nipo mbioni kukata tiketi pia.
Special request kwa moderators, tafadhali msiunganishe uzi huu na ule uzi wa Kahama vs Tunduma. Nimeusoma ule uzi na nimekosa maelezo ya msingi ninayoyahitaji.
Natanguliza shukrani kwa yeyote atakaejitoa kunipa dira.
Nimekuja kwenu leo hii nikihitaji dira ya wapi ni pazuri zaidi kwa biashara ya duka la mangi kati ya Kahama au Tunduma.
Kwa kifupi nimefanya ajira Arusha kwa muda mrefu sana, takribani miaka miwili nikaacha na kuanza kuuza duka la Mangi hapa Usariver. Kwa ujumla biashara ilikuwa ya kawaida, ilikuwa na siku nzuri na siku zilizokwenda tofauti. Lakini nimefikia mkataa wa kwamba nataka kutafuta changamoto MPYA na kubadili mazingira. Nataka kuondoka hapa Arusha na kwendA KAHAMA au TUNDUMA.
Nimechagua hizo sehemu mbili kutokana na kusifika kuwa na mzunguko wa biashara. Hata hivyo ni ngumu kwangu kuamua wapi HASA pa kwenda kutokana na ukweli kwamba SIJAWAHI kufika popote kati ya sehemu hizo, sijui gharama za maisha na aina za biashara ambazo zinakubali sana huko. Lakini pia maamuzi yangu yanatiwa ukakasi na mambo yafuatayo ambayo yamesemwa sana na watu kuhusu sehemu hizo.
1. Nikisema ntaamua kwenda Tunduma basi napata ukakasi kila nikikumbuka mambo ambayo watu wanasema kuhusu mahali hapo kwamba kwanza hakuna maji, miundombinu duni na ni "sehemu ambayo biashara pekee inayokubali ni MAGENDO tu! eti biashara nyingine zote zinafeli labda uwe na mtaji mkubwa".
2. Nikisema niende Kahama basi wazo langu litatiwa ukakasi na uvumi kwamba eneo hilo lina mzunguko kutokana na mgodi wa buzwagi. Kwamba siku ambayo mgodi huo utafungwa sehemu hiyo itapoteza kila kitu kutia ndani watu na mzunguko uliopo hapo. Ukizingatia hivi karibuni kumekuwa na seke seke la kwamba siku inakuja ambapo wachimbaji wadogo wataondolewa na migodi itafungwa. Nawaza vipi nikifika pale nikajiwekeza na kabla biashara haijachanganya "migodi ikafungwa ?", Ntakuwa nimeangukia pua.
Wataalamu, wenyeji na wajuzi wa haya maeneo naomba muongozo wenu ili nifanye maamuzi yenye 'low risk', nataka nifanye shughuli ya duka la mangi na mipango yote ya kuhama ilishaanza, nipo mbioni kukata tiketi pia.
Special request kwa moderators, tafadhali msiunganishe uzi huu na ule uzi wa Kahama vs Tunduma. Nimeusoma ule uzi na nimekosa maelezo ya msingi ninayoyahitaji.
Natanguliza shukrani kwa yeyote atakaejitoa kunipa dira.