Duka la Dawa Muhimu za Binadamu (Pharmacy): Utaratibu wa Kufuata na Mtaji wa Kuanzisha Biashara

mjasiria

JF-Expert Member
Jan 10, 2011
4,156
1,850

Wakuu nina maswali kadhaa kuhusu hii biashara.
  1. Je, ninahitaji vibali gani? Na vinapatikana katika ofisi zipi na pia itakuwa msaada sana kama itawezekana kuweka gharama zinazolipwa kwa kila kibali.
  2. Je, mtaji kiasi unatosha kufungua biashara hii.
Natanguliza shukrani zangu.


WADAU WENGINE WANAOHITAJI MUONGOZO WA BIASHARA HII


MICHANGO YA WANA JF


KUTOKA TFDA


USHUHUDA BAADA YA KUFUATA USHAURI WA WANAJF
 
Mkuu kila kitu kinawezekana na kwa mtaji wa kiasi ulichosema, naamini lengo litatimia.

Wahusika wakuu wa hii kitu ni TFDA ambao ofisi zao zinapatikana mabibo external.

Nenda katika ofisi zao watakupa majibu ya maswali yako yote na mengine ambayo haukuuliza hapa.

Naogopa kukupa majibu hapa kutokana na mapinduzi makubwa yaliyofanywa na TFDA katika biashara hii ya dawa baridi ambayo kwa sasa wanaziita dawa muhimu.

Make sure you have all the details before jumping into it, si vibaya ukajaribu kuonana na watu ambao tayari wanafanya hii biashara, uhakika nilionao ni kwamba hii biashara inalipa, unachohitaji ni umakini na subira kwa siku za mwanzo za biashara.
 
Kwa ufupi maeneo ya mijini huwezi kuanzisha tena duka la dawa baridi. TFDA ilishatoa tamko. Unatakiwa kuanzisha duka la dawa muhimu vijijini na pembezoni mwa mji ambapo inaelekeana na rural settings.

Kwa maelezo zaidi wasiliana na TFDA, email info@tfda.or.tz . Pia kumbuka kuwa vibali vya maduka ya dawa baridi vinashughuliiwa na Halmashauri ya wilaya/mji/manispaa husika.

Kama upo Kinondoni basi unawasiliana na mfamasia wa manispaa (Kinondoni anaitwa mabonesho) ila kama mdau aliyetangulia alivyosema nenda TFDA kaonane nao.

Specifically kutana na Kitengo kinachohusika na Maduka ya Dawa muhimu (kwa Kiingereza wanayaita ADDO).

Upo hapo kama unataka namba zao ni-PM
 
NISAIDIN JINSI YA KUPATA LESSEN YA DUKA LA MADAWA. Nataka kufungua duka la madawa ya binadamu mkoa songea naomba jamani anayefahamu njia za kupita ili nifanikiwe lengo langu anisaidie nawatakia siku njema.
 
Mkuu hapo kwenye hospitali ya wilaya kuna mfamasia wa wilaya, nenda ukamwone atakupa utaratibu wote.
 
Nenda kwa mfamasia wa mkoa au TFDA. TFDA wana ofisi ya Kanda pale Mbeya. ila kumbuka kwa Songea kuna maduka ya dawa aina mbili:
  1. Duka la dawa muhimu- ADDO
  2. Pharmacy
Sasa wewe unataka kuanzisha lipi mana requirements zinatofautiana.
 
Habari za asubuhi wana JF.

Wakuu kunasehemu nimeona naweza kufungua duka la dawa, naomba watalaam wanisaidie mahitaji yanayohitajika na gharama zake. Ningependelea kuweka dawa nyingi coz mi dr, kama kuna mtu anifafanulie madaraja ya maduka ya dawa. Natarajia ushirikiano wenu wakuu. Asante.
 
Nenda kamwone mfamasia wa wilaya ya eneo husika atakupa imput zote lakini kwa sasa tuna madaraja wa2 tu ya duka la dawa.
Duka la dawa Muhimu na Pharmacy inayohitaji uwe na mfamasia wa degree.
Mahitaji mengine ni vyumba viwili.
 
Naomba mwenye uzoefu na utaalamu wa biashara ya duka la dawa anisaidie, nataka kuanzisha hii biashara.
 
Sio ya kulevya

Nataka kufanya biashara ya kuingiza dawa za binadamu toka nje je nahitaji kibali gani.

Pia, kama nataka kuingiza solution ya unga wa maziwa ya watoto je nayo nahitaji vibali vipi?

Vitu kama pedi za wanawake na pampers za watoto pia nataka kuingiza je zaidi ya TBS nahitaji vibali toka wapi? Na process ikoje?
 
Ndugu wanajamii forum,

Nahitaji kujua taarifa kuhusu biashara ya dawa baridi. Naomba msaada wa kujua mawazo yenu kuhusu hio biashara, walau mtaji kiasi cha chini ni kiasi gani inatakiwa, namna gani ya kuendesha na taratibu zote za kufungua hadi kuweza isimamisha. n

Asante.
 
Milioni mbili hadi tatu, pia tafuta mfanyakazi mzoefu kidogo usije nunua madawa mengine yaka-expire store kukosa wtj.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…