Dudu baya atao povu baada ya kuambiwa amepigika na anakunywa viroba!

Nucky Thompson

JF-Expert Member
Sep 20, 2016
1,817
4,058
Dudu Baya alisema watu hao ni Kenge na hawawezi kumtishia mamba



Pia kusema kuwa watu wanapoona yupo kimya wanadhani huenda amefulia na kusema yeye yupo busy na biashara nyingine na muda mwingi anakuwa hayuko Dar es Salaam lakini yuko poa na maisha yanakwenda safi.

"Mimi hakuna mtu wa kunipangia kunywa viroba, iwe asubuhi saa mbili, iwe saa tano asubuhi au muda wowote nitakunywa tu, Mimi siyo mwajiriwa kusema niogope kunywa nitakunywa muda nao taka mimi" Amesema

Amesema kwa sasa maisha yake yako Mwanza na Kampala akija Dar anakuja kufanya kazi za kisanaa japo alishaamua kupotezea muziki na kufanya biashara zake mbalimbali kwa kuwa haishi kwa kutegemea mziki pekee.

"Dudu Baya sijafulia kama watu wanavyodhani mimi na biashara zangu nyingine na muda mwingi sipo Dar es Salaam. Watanzania ndiyo tabia yao hiyo wakiona msanii haonekani wanadhani amefulia mfano watu walipoona King Crazy GK amepotea walidhani amefulia kumbe alikuwa chimbo anapiga kitabu na saizi tayari ana masters yake" alisema Dudu Baya

Pia Dudu amesema kauli ya Darasa kuimba kwamba 'siyo chui, simba wala mamba ngozi yake inamtosha kujigamba' haijamsumbua kwa kuwa Darasa ni kijana wake na ni msanii ambaye amepambana kwa muda mrefu ila kwa sasa kafanikiwa hivyo anampongeza kwa mafanikio.
 
Safi sana nimependa apo mwisho alipompongeza darassa kumpongeza aliefanikiwa ni vizuri sio kuleta chuki na wivu wa kijinga
 
Back
Top Bottom