Dual citizenship

Rudi nyumbani uwasaidie watanzania wenzako,uraia wa nchi mbili kwangu ni upuuzi mtupu,tutaiga wazungu kila kitu? wao wanafanya hivyo ili wapate nafasi ya kuhujumu.
Dongeee hilo, hamna lolote. Swali limeulizwa sula la Dual citizenship limefikia wapi. Unachojibu ni nje ya mada husika kabisa. Yaonyesha elimu haikusidii wewe hata tonye. Ndio nyie nyie!
 
Chill out guys. Hivi mnafikiri Tanzania wakisema hakuna DC ndio basi? Nendeni Upanga na Osterbay muwapekue wakaazi wa huko mtakuta wana passport za nje ingawaje wao ni WTZ. Hata mkuu wa kaya mwenyewe ana passport ya nje hapa ni siasa tu hakuna lolote.

Wenye moyo wa kubadili mwelekeo wa maisha ya Watanzania kuwa maisha ya hali ya juu watafanya lakini tena sio kwa kusema bali vitendo. Ni WTZ wachache sana ambao wanakwenda nje na hawapendi kurudi Tanzania sio kwa kupenda bali circumstances zinawazuia lakini ni afadhali ya wao kwani wametumia pesa zao binafsi kuliko Vasco Da gama ambaye anatumia pesa ya walipa kodi na hakuna matokeo yoyote.

Ni aibu kwa kweli miaka 49 ya uhuru bado tunabangaiza kama viichi majirani zetu wakati tungekuwa kwenye level ya Malasyia au Singapore ambazo ni nchi tulizopata uhuru almost same years na economy yetu na wao almost the same wakati ule. (nafahamu kuna more than that but at least we would have been better) Nilikuwa naangalia kideo wakati wa uhuru Dar waliokuwa wamevaa ndala ni wa kuhesabu majority peku peku, Waliovaa viatu unatafuta.

Chama Cha Majambazi kimepoteza mwelekeo na nina imani watakaoweza kuikomboa Tanzania ni hawa wenzetu waliokuwa wamezamia na kujielimisha kwenye nchi za wenzetu. Wakirudi wote hawa bongo moto utawaka kweli! Si mnaona wanavyolalamika hawapendi kabisa input ya mawazo kutoka kwa wabongo walio nje kwa sababu wanajua hawawezi kuwababaisha na biskuti. Wamewateka walipa kodi kwa kofia, kanga, biskuti, na mikokoteni kutoka Japan. Haiingii akilini kuona viongozi wa CCM na serkali wanaishi kama wako peponi wakati walipa kodi wako ICU.
 
Lakini nimemuona Mhe Bernard Membe akisema kuwa uraia wa kuzaliwa hakuna anaeweza kuufuta na hivyo ndivyo inavyotambulika na hao dunia ya kwanza, sasa wale wenzetu waliochukua uraia wa nchi nyengine kwa kuandikisha si raia wa Tanzania kwa kuzaliwa? Moja na moja ni mbili au vipi?
Asante sana Kiongozi, ila huyu Mhe. Membe naye haelewi hata tonye. Kuwa na uraia wa nchi mbili haimanishi kuwa umeusaliti mwingine haswa ule wako wa kuzaliwa. kila nchi ina masharti yake na ndio maana ukiwana dual citizenship kama wewe si mzawa wa hiyo nchi basi kuna nafasi fulani fulani za serikali huwezi kugombania au kupewa. Mfano wewe ni mzaliwa wa Tanzania na una dual citizenship ya Tanzania na Uturuki ina maana huwezi kuwa katika nafasi fulani fulani za nchi ya Uturuki ila kwa Tanzania unaweza kwa sababu wewe ni mzaliwa wa nchi hiyo.
 
safi sana mkuu, umenikuna mpaka natoka unga. itabidi nikugongee thanks.

mtu mzima hataki kurudi nyumbani anabangaiza apate uraia wa nchi nyoingine utadhani hana nchi yake. hawa ndio wanaotutia aibu huku ng'ambo. nikipata nafasi ya maamuzi siku moja msahau kabisa huyo punda anayeitwa uraia wa nchi mbili.

mi niko ng'ambo kwa sasa naingia na kutoka karibu kila nchi ninayotaka bila matatizo ya kunyimwa au kucheleweshewa viza na nina uhakika wa kuendelea kukaa huku niliko (kama nitataka) ng'ambo kwa muda wote nitakaopenda. lakini uraia wa nchi tofauti na tanzania hata ukiniletea bure kwenye karai sichukui. upuuuzi mtupu.

nimetembea sana dunia sijaona nchi nzuri kama tanzania! jamani watanzania turudi nyumbani tujenge nchi yetu, sio mkae huku mkiuliza tanzania imewafanyia nini mje kula.

mimi narudi februari mwakani.

jamani kila anyetaka kurudi aandike hapa anarudi lini sio huu upuuzi wa dual citizenship!.
Hongera sana kwa hilo. Kila mtu ana mawazo yake na nadhani hapo ndipo mwisho yalipofikia yako ktk suala zima la dual citizenship. Kabla hata ya kuondokaga Tanzania nilishaonaga kuwa curriculum ya Tanzania inahitaji kubadilisha ili iboreshwe zaidi na pia iwe na michezo ndani yake. hii yote ni baada ya kuona wenzetu Uganda na kenya wakati nasoma katika nchi hizo miaka tofauti ya nyuma. Kiongozi husikurupuke kuchangia bila kuhoji baadhi ya mambo muhimu kwa undani zaidi.
 
Tulikuwa kwenye kikao cha moja moto na moja baridi na mtangazaji mmoja maarufu sana tena wa siku nyingi. Kuna jamaa mmoja ndiyo kwanza alikuwa ameshuka toka majuu. Katika mazungumzo yule Mtangazaji maarufu akamtwanga swali yule jamaa wa majuu "umeshachukua uraia wa huko uliko?" jamaa akasema bado, sijui kama alikuwa anavunga au anasema kweli.. Mtangazaji akaendelea "unangoja nini?" jamaa akajibu kishatimiza masharti yote ya kuomba uraia lakini hakuwa na haraka nao. Mtangazaji akaendelea "uchangamkie mapema kabla ya sheria hazijawa ngumu zaidi, Utanzania haukusaidii chochote." hii kauli ya "Utanzania haukusaidii chochote ilinishtua sana lakini ukweli wa mambo ni kwamba Watanzania wanaoishi nchi za nje wameshafungua macho kwamba kuchukua uraia wa nchi nyingine si kuisaliti au kuikana Tanzania bali ni kujiweka sawa na wawe na uhuru wa mambo mbali mbali katika nchi hizo ikiwemo za kupata kazi ambazo wasio raia hawaruhusiwi kuapply. Na Watanzania wanaopata nafasi za kuishi nchi za nje hawalazi damu wanapopata nafasi hizo. Nyie wenye roho za korosho kaeni na roho zenu mbaya na kudhani kuwapa uDC Watanzania wazaliwa wa Tanzania eti ni kuhatarisha amani ya nchi. Muda si mrefu Tanzania itakuwa nchi pekee katika Afrika ambayo hairuhusu uDC.
 
Unafikiri kuwa Tanzania ndiyo kuipenda Tanzania?

I wish Lowassa na kundi lake la Mafisadi wangelikuwa wanaishi nje.

Anyway, Utanzania uko moyoni mwa mtu na siyo kwenye JF au kurudi Tanzania. Hata Boss wa Marks and Spencer aitwaye Stuart Rose ambaye alishawahi kuishi zamani Dodoma, alirudi huko na kusaidia shule ambapo zamani walikuwa wanakaa. Huyu ingawa si Raia wa Tanzania (na wala hahitaji) anaweza kuwa Mtanzania zaidi ya akina Lowassa, Mkapa, Liyumba, Mgonja, Mramba na wengine wengi tu.

Mwisho niseme kimoja. Nashindwa kufahamu unachokisema hapa wewe ni kuipenda Tanzania au Uraia wa nchi mbili? Je mtu mwenye uraia wa nchi mbili, ina maana haipendi Tanzania? Mwenye wa nchi moja na anaishi Tanzania ina maana anaipenda sana Tanzania?

Kwangu mie kuipenda Tanzania ni kama ule mfano wa tembo na vipofu 7. Kila mtu anagusa kipande fulani na anaonyesha mapenzi yake. Ukianza kuwacheka wanzako kwa kuonyesha mapenzi kwa Tanzania kwa njia nyingine tofauti na unazotaka wewe ndiyo hiyo ninasema kuwa Mkuu wewe una UMIMI SANA. Kwa nini unapoteza muda kwenye nchi za watu? Kaa Tanzania hadi uje ufie hapa. Una Passport yenye kukuruhusu kutembea dunia nzima na mwisho unakuja kudai watu WARUDI Tanzania. Wewe hiyo Passport na hizo VISA zilizomo ndani za nini?
http://www.youtube.com/watch?v=t3vJ...E50EFE27A&playnext=1&playnext_from=PL&index=6

ndugu hizo ulizosema ndiyo changamoto za siasa. na tayari tumo kwenye mapambano. wito wangu sote tuingie kwenye mapambano

kikamilifu. nimesikitika sana kwa mfano wako wa msaada wa mzungu kule dodoma! nimepata picha halisi wewe ni mtu wa aina gani na kwa nini huamini kuwa moja ya matendo ya mzalendo ni kupenda kuishi kwao. unaamini kuwa kuhangaika kutafuta uzalendo wa nchi nyingine wakati unayo nchi yako nzuri kama tanzania si utumwa! kisa eti siku moja uaweza kuja kuwasaidia watanzania zaidi ya akina lowasa wanavyowasaidia! nani kakwambia watnzania ni wa kusaidiwa tuu?

njoo kama uko nje, au kama uko nyumbani na una safari ya kwenda nje, nenda na urudi tujenge nchi yetu.
 
Hongera sana kwa hilo. Kila mtu ana mawazo yake na nadhani hapo ndipo mwisho yalipofikia yako ktk suala zima la dual citizenship. Kabla hata ya kuondokaga Tanzania nilishaonaga kuwa curriculum ya Tanzania inahitaji kubadilisha ili iboreshwe zaidi na pia iwe na michezo ndani yake. hii yote ni baada ya kuona wenzetu Uganda na kenya wakati nasoma katika nchi hizo miaka tofauti ya nyuma. Kiongozi husikurupuke kuchangia bila kuhoji baadhi ya mambo muhimu kwa undani zaidi.

hapo unadhihirisha kuwa wewe ulishakuwa mtumwa kabisa wa maisha ya ng'ambo, ulilamba asali sasa hutaki kunawa mikono! unataka kuchonga mzinga kabisa.

pia umedhihirisha vizuri ukomo wa mawazo uliyonayo katika cariculum na DC. nakuhakkikishi kuwa hata DC itakaporuhusiwa kisheria (najua hatimaye itaruhusiwa) haitakuwa suluhisho la matatizo ya uhamiaji yaliyopp sasa. haya ni mambo ya kisera tu, na sera suri si lazima iruhusu DC, ipo mibadala mingi

hebu tukae chini, tujenge nchi yetu, duniani tutembee na kutafuta maisha, lakini kwetu ibaki kuwa tanzania, vinginevyo tunaigeuza nchi yetu nzui kuwa shamba la bibi ambapo wenye meno makali tu ndio watakaofaidi matunda yake
 
Back
Top Bottom