Dstv ya BURE kupitia Vodacom!

BabaDesi

JF-Expert Member
Jun 30, 2007
6,027
3,941
simu yangu ni Nokia N95 8gb. Toka juzi najaribu kujiunga na ofa ya Dstv kupitia Vodacom ya kuona matangazo ya bure ya TV lakini kila ninapojaribu kujiunga napata maelezo ya 'Not enough Bandwidth'! Wataalamu, Hapo natakiwa kufanya nini?
 
Nimejaribu nikiwa na buku 2 za airtime lakini inaniambiat ya kutokuwa na bandwidth ya kutosha! Tatizo litakuwa ni nini?
 
sasa mkiskia online tv mwajua bureeeezzzz??????? Inakula net kama wataka kuuza sura kitaa bora unune hata cheka internet
 
vodacom dstv mobile service ni bure.nenda kwenye settings-phone-network halafu badilisha kuwa umts.
 
nimejaribu kutumia dstv mobile ila nimekatwa kiasi kikubwa cha hela, nilipouliza customer care wakasema ni free kwa vile hutakiwi kulipa malipo ya mwezi au subscription fees, ila gharama nyingne zinakuwapo
 
Hii huduma inatakiwa na inatangazwa kuwa ni bure, haitakiwi kula data bundle wala hela kwenye simu, ila inaelekea Voda wamechemsha au wanafanya makusudi kuwaibia watu hela inaenda kama kawaida.
 
sio wizi huyo jamaa hapo hapo juu ameeleza ukweli kabisa, dstv mobile inalipiwa kwa mwezi hela hiyo unayolipa ni tofauti na bundle ya internet so kupitia voda hutalipa utalipa tu ya bundle.
 
voda ni majambazi hakuna tofauti na majambazi wanaotumia silaha ya smg ningekuwa nakipato chakumlipa wakili ningewabuluza kotini
 
sio wizi huyo jamaa hapo hapo juu ameeleza ukweli kabisa, dstv mobile inalipiwa kwa mwezi hela hiyo unayolipa ni tofauti na bundle ya internet so kupitia voda hutalipa utalipa tu ya bundle.

Ukienda website yao wenyewe Vodacom Portal ukacheki DsTV FAQ

DStv Mobile is a mobile TV streaming service available exclusively to Vodacom Tanzania customers that allows you to access 5 DStv channels using a 3G and 2.5G video capable cellphone. The service is available to you at no charge.

No data charges apply when using the DStv Mobile service.

Kwa kifupi hawa jamaa ni wezi, na tungekuwa nchi nyingine wangekuwa washachukuliwa hatua na vyombo husika, ila Bongo ili mradi liende.
 
Ukienda website yao wenyewe Vodacom Portal ukacheki DsTV FAQKwa kifupi hawa jamaa ni wezi, na tungekuwa nchi nyingine wangekuwa washachukuliwa hatua na vyombo husika, ila Bongo ili mradi liende.
Selikali imeshikiliwa na majambazi mafisadi nani atakumbuka kuwafatilia huu wizi unao fanyika huko voda
 
hayaa wale wagumu mlokua hamtaki kutumia voda link hiyo nshaichakachua copini kwenye streming link muangalie na bundle ya mb400 airtel rtsp://196.28.65.226/diactus/movie.3gp?weUE9Qdy3GHWo2-5Tpic3b47H(i8afKugOTAdmjZcV1ljArP1641PQ7ee3h-yN20 manake dah wabongo kila kitu siasa hadi huku kwenye science
 
hayaa wale wagumu mlokua hamtaki kutumia voda link hiyo nshaichakachua copini kwenye streming link muangalie na bundle ya mb400 airtel rtsp://196.28.65.226/diactus/movie.3gp?weUE9Qdy3GHWo2-5Tpic3b47H(i8afKugOTAdmjZcV1ljArP1641PQ7ee3h-yN20 manake dah wabongo kila kitu siasa hadi huku kwenye science

Thank u Very much! Hii haiitaji masimu makuuubwa!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom