DRC Congo: Jenerali wa Jeshi ampa Rais Kabila siku 45 aachie Urais, asambaza video

Itzmusacmb

JF-Expert Member
Jun 22, 2016
1,531
1,132
Haijapita hata miezi mitatu toka tushuhudie Jeshi likiingilia kati na kumuondoa madarakani Rais aliekaa muda mrefu madarakani, Robert Mugabe wa Zimbabwe….. leo tena tunasikia huko Congo DRC Mwanajeshi mmoja ampa Rais Kabila siku 45 awe ameachia madaraka.

Tunafahamu kwamba Rais Kabila alimaliza muhula wake wa pili na wa mwisho kikatiba kuwa Rais mwezi December 2016 lakini hajaachia madaraka, mengi yamesemwa na Serikali ikiwemo “hatuna pesa za kutosha kufanya Uchaguzi Mkuu”

January 19 2018 Mwandishi wa habari Byobe Malenga alieko Congo DRC amesema kwamba Jenerali mmoja wa Jeshi aitwae John Tshibangu ameasi na kutangaza vita na Rais Kabila, amempa siku 45 aachie madaraka.


Asubuhi ya Ijumaa January 19 2018 Wanajeshi walionekana kuizingira kwa wingi IKULU ya Kinshasa huku video iliyorekodiwa na Jenerali Tshibangu ikiendelea kusambaa ambapo ndani yake ameonekana kazingirwa na Wanajeshi wenye silaha.

Kwenye video hiyo Tshibangu amenukuliwa akisema “Nafahamu siri ya Rais Kabila, sasa ni muda wa kuondoa Serikali ya Mabeberu na Udikteta, na ni lazima Rais Kabila aombe msamaha kwa Wakongo kuanzia Makanisani, Shuleni na hata Raia wa kawaida kwa kosa la kushindwa kuiongoza Nchi”

“Mimi kama Mwananchi mwenye msimamo na huruma kwa mateso yenu, niliamua kujitokeza ili kumfukuza Joseph Kabila kwa nguvu za vita na kijeshi, nawahakikishia kwamba tutamuwinda na atakimbia. ” – John Tshibangu.


6de220b68b123a97309a7bccd13a2293.jpg


Tshibangu amelitaja kundi lake la Waasi kwamba linaitwa Forces Nouvel du Congo ikimaanisha NGUVU MPYA KWA AJILI YA CONGO ambapo Taarifa za uhakika zinaeleza kuwa kumekuwa na majaribio ya mapinduzi katika Serekali ya Congo ambapo IKULU ya Taifa imezungukwa na Wanajeshi wengi wanaoonekana kama Wageni, yaani sio Wanajeshi wa congo.

Raisi Kabila amekabiliwa na upinzani mkali kutokana na nia yake ya kutaka kugombea Urais kwa muhula wa tatu baada ya muhula wake wapili kumalizika mwezi December 2016.


Patamu Hapo
 
Nimesikiliza na kutizama vyombo mbalimbali vya habari vya kimataifa hii habari sijaisikia hata chembe.
 
Back
Top Bottom