Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,346
- 26,138
Natamani sana kuwa kama yeye. Kwa juma zima hili, Dr.Slaa amekuwa akifanya ziara katika Kanda ya Ziwa Magharibi ukiwemo mkoa wa Kigoma.Katika ziara hiyo,kuna taarifa mbalimbali. Kuna zinazosema kuwa Dr.Slaa amefanyiwa/anafanyiwa/atafanyiwa vurugu na hivyo ziara zake zimedorora. Kuna taarifa toka Kurugenzi ya Habari ya CHADEMA kuwa ziara zake zinafana na kuendelea vyema.
Dr.W.Slaa,pamoja na kusemwa tofautitofauti,anasonga mbele.Hajawahi kukimbilia mitandaoni kukanusha au kupambisha ziara zake na kinachoendelea. Wangekuwa akina fulani hapa pangejaa mabandiko yao. Dr.W.Slaa ni mfano wa kuigwa wa wanasiasa. Yeye anajali zaidi kujenga hoja na kuacha mengine kupita bila ya yeye kuhusika. Mwanasiasa huyu kiboko!
Ziara za Kigoma zinasemwa kama kupambana na Zitto. Lakini si kweli. Dr.Slaa anajua fika kuhusu hilo.Ndiyo maana yeye anaendelea na ziara za kukagua na kuimarisha chama chake huku akiyaacha mambo mazito ya Zitto yaendelee kujadiliwa kichama.Hakuna hata hotuba moja iliyoripotiwa humu au kwingineko ambapo Dr.W.Slaa amemzungumzia Zitto. Huu ni ukomavu.
Wote wanaopanga kuvuruga mikutanoya Dr.W.Slaa wanashindwa.Watashindwa kwakuwa yeye si mkorofi na hajibu mapigo.Yuko tofauti sana mwanasiasa huyu. Hakuna haja ya kukodi au kusafirisha watu wa kuvuruga mikutano yake. Wavurugaji watavurugwa wao. Busara za Dr.W.Slaa ni ulinzi wake tosha.
Kila la kheri Dr.Wilbrod Peter Slaa. Mungu atakutangulia!
Muhimu: Mimi si mwanachama wa chama chochote cha siasa hapa Tanzania au kwingineko duniani. Nasema ukweli tu
Dr.W.Slaa,pamoja na kusemwa tofautitofauti,anasonga mbele.Hajawahi kukimbilia mitandaoni kukanusha au kupambisha ziara zake na kinachoendelea. Wangekuwa akina fulani hapa pangejaa mabandiko yao. Dr.W.Slaa ni mfano wa kuigwa wa wanasiasa. Yeye anajali zaidi kujenga hoja na kuacha mengine kupita bila ya yeye kuhusika. Mwanasiasa huyu kiboko!
Ziara za Kigoma zinasemwa kama kupambana na Zitto. Lakini si kweli. Dr.Slaa anajua fika kuhusu hilo.Ndiyo maana yeye anaendelea na ziara za kukagua na kuimarisha chama chake huku akiyaacha mambo mazito ya Zitto yaendelee kujadiliwa kichama.Hakuna hata hotuba moja iliyoripotiwa humu au kwingineko ambapo Dr.W.Slaa amemzungumzia Zitto. Huu ni ukomavu.
Wote wanaopanga kuvuruga mikutanoya Dr.W.Slaa wanashindwa.Watashindwa kwakuwa yeye si mkorofi na hajibu mapigo.Yuko tofauti sana mwanasiasa huyu. Hakuna haja ya kukodi au kusafirisha watu wa kuvuruga mikutano yake. Wavurugaji watavurugwa wao. Busara za Dr.W.Slaa ni ulinzi wake tosha.
Kila la kheri Dr.Wilbrod Peter Slaa. Mungu atakutangulia!
Muhimu: Mimi si mwanachama wa chama chochote cha siasa hapa Tanzania au kwingineko duniani. Nasema ukweli tu
Last edited by a moderator: