Dkt. Wilbert Kleruu - Utata wa kifo chake, historia na maisha yake

Ktk dunia hii wamepita watu wenye madhambi makubwa na Mwenyezi Mungu atawaadhibu vibaya sana kama hawakutubia madhambi yao. Hebu fikiria hili: watu wametoka huko walikotoka wakahamia sehemu ambayo ni pori (Isimani) lisilo na huduma zozote. Wakavumilia mateso yote huku wakifanya kazi kwa bidii hadi Mwenyezi Mungu akawajaalia kupata riziki zao na kuwa wakulima matajiri wakubwa. Ghafla anatokea mtu mwingine kwa falsafa yake ambayo Muumba haikubali anataifisha mali zao na kuwahamisha ktk majumba yao na kuwapeleka anakotaka yeye kwa sababu ya huo uitwao Ujamaa! Hivi kosa hili halifai kuwa miongoni mwa madhambi makubwa? RIP Mwamwindi ulisimama imara kutetea haki dhidi ya batili na Mwenyezi Mungu siku hiyo ya hukumu ataonyesha ni nani kati yako na wao alikuwa sahihi. Sisi ni wa Mwenyezi Mungu na kwake tutarejea.
 
hi wana JF,
Nimewasili jana jioni toka shamba kwenye shughuri zangu za kujitafutia Riziki, njiani nilinunua Gazeti la Mwananchi. Duh, lina bonge la Makala isomekayo MKULIMA ALIYEMPIGA RISASI,KUMUUA RC KLERUU. Kwa wale wanaopenda kufahamu Histori ya Nchi hii, nawashauri Mtafute gazeti la Mwananchi la tangu Juzi (tar. 20 June, 2016) ili muweze kufahamu ujasiri wa Mzee Mamwindi.

Nawatakia usomaji mwema.

Mkulima 1.png
Mkulima 2.png
 
nilisoma hiyo story, ndio naona kama yanayotokea sasa manake jamaa alishindwa kuvumilia, akaona imekuwa too much akamtwanga risasi, nasikia jamaa alinyongwa na alipoua alienda mwenyewe kituoni kuwaambia tayari keshaua mkuu wa mkoa
 
Hii habari story kuna kipindi Maggid aliisimulia na aliwahoji hadi ndugu zake Mwamwindi waliokuwepo enzi hizo. Tukio lilikuwa kama movie hivi...Wahehe zikiwapanda hawakamatiki.
 
nilisoma hiyo story, ndio naona kama yanayotokea sasa manake jamaa alishindwa kuvumilia, akaona imekuwa too much akamtwanga risasi, nasikia jamaa alinyongwa na alipoua alienda mwenyewe kituoni kuwaambia tayari keshaua mkuu wa mkoa
Mzee alichoka kuzinguliwa, na kudharirishwa. Akajitoa muhanga. Wahehe wanam-treat kama shujaa mmojawapo, ukimuondoa Mkwawa.
 
Hii habari story kuna kipindi Maggid aliisimulia na aliwahoji hadi ndugu zake Mwamwindi waliokuwepo enzi hizo. Tukio lilikuwa kama movie hivi...Wahehe zikiwapanda hawakamatiki.
Sasa hivi inasimuliwa na Tumaini Msowoya, yule bingwa wa kuandika Makala zilizoenda shule.
 
Sasa hivi inasimuliwa na Tumaini Msowoya, yule bingwa wa kuandika Makala zilizoenda shule.
Ukiona mtu yoyote anaandika Historia ya Kuuwa kwa Dr Kreluu basi moja kwa moja anafanya Rejea ya alichokiandika maggid ....Huyu bwana aliandika kila kitu kuhusu huu mkasa mpaka kuongea na Ndugu wa damu kabisa wa Mzee Mwamwindi. Hiyo huyo Tumaini wako yeye anarejea tu au kama sio Copy &Paste.
 
Ukiona mtu yoyote anaandika Historia ya Kuuwa kwa Dr Kreluu basi moja kwa moja anafanya Rejea ya alichokiandika maggid ....Huyu bwana aliandika kila kitu kuhusu huu mkasa mpaka kuongea na Ndugu wa damu kabisa wa Mzee Mwamwindi. Hiyo huyo Tumaini wako yeye anarejea tu au kama sio Copy &Paste.

Mkuu, nae alienda kuwahoji wahusika kulingana na nilivyosoma hio makala, all in all huyo mzee alikua jasiri sana..
 
Ukiona mtu yoyote anaandika Historia ya Kuuwa kwa Dr Kreluu basi moja kwa moja anafanya Rejea ya alichokiandika maggid ....Huyu bwana aliandika kila kitu kuhusu huu mkasa mpaka kuongea na Ndugu wa damu kabisa wa Mzee Mwamwindi. Hiyo huyo Tumaini wako yeye anarejea tu au kama sio Copy &Paste.
Maggid aliandika vizuri na kuwahoji watu mbali mbali. Ila hata huyu Tumaini Mswoya amafanya kazi yake vema. Amewahoji watubmbali mbali akiwemo mtito Mkubwa wa Marehemu Mzee Said Mwamwindi ambaye pia ni diwani. Ameenda mbali zaidi na kuonesha maishs baada ya tukio, baada ya kunyongwa kwa Mwamwindi na uhusiano uliopo kati ya familia ya Kleruu na Mwamwindi na hata mkutano wa kwanza kati mtoto mkubwa wa Mwamwindi na Eva mtoto mkubwa wa Kleruu ili kuondoa hali ya kutoamiana na kufungua ukurasa mpya.
9b34dcd42ea55cf1efce2da81be65fe4.jpg
 
Pia kuna issue ya kuwa Nyerere wakati mwingine alikuwa anatibiwa mambo ya akili, je inawezekana alikuwa "incapacitated" wakati wa kuweka saini hapa? inawezekana personal loss za huyo Dr. Kleruu iliweza kumfanya mzee wa watu akawa katika hali ya kutoweza kutoa maaamuzi akiwa timamu. Naweza nisi-substantiate hizi habari za Nyerere kutibiwa mambo ya akili ila kuna daktari mmoja wa muhimbili kipindi cha nyuma aliwahi kunigusia kuwa alikuwa na tatizo hili na familia yake wana tatizo la akili vile vile.
Aisee jamiiforums kumbe kiboko,ina maana mkuu alikuwa mgonjwa kumbe..!!??
 
Historia huwa zinajirudia.
Watz watakuwa na kumbukumbu za Marehemu Dr. Kleruu aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa aliyeuawa miaka ya 60 baada ya kutangazwa kwa Azimio la Arusha! Kwa utawala huu wa CCM chini ya Magufuli huenda wakaibuka kina Mwamwindi wengine ili kukomesha upuuzi na Ujinga unaofanywa na baadhi ya Wakuu wa Wilaya na Mikoa wanaojifanya ni miungu watu!

Kuna Wakuu wa Mikoa ya Arusha na Dar-es-salaam ambao wanajifanya kindakindaki kwa kuwa- harass Wananchi na Wabunge hasa wa upinzani kwa vile tu wana mtazamo tofauti na Serkali ya CCM. Kibaya zaidi ni kwamba hawa watu wanapewa jeuri na Mamlaka iliyowateua. Baba wa Taifa aliwahi kusema ukianza DHAMBI YA UBAGUZI basi huwezi kuiiacha maana ni sawa na kula nyama ya mtu! Na dhambi hiyo mkiifanya ITAWATAFUNA na mimi nasema IWATAFUNE! Dhambi hiyo imeanza na inakolezwa na utawala huu na ni hatari sana kwa mstakabali wa Taifa letu!
Tafakuri!
 
Na kile chuo cha kreluu iringa ndo moja wapo ya mambo ya kumuenzi naombeni ufafanuzi
 
mimi naona tuamini alichosimulia mwanae amani mwamindi, mana kila mchangiaji anasimulia kiutofauti wa hapa na pale
 
Back
Top Bottom