Dr. Ulimboka hatukuelewi ! ! !

Dr. Ulimboka hatukuelewi ! ! !

watanzania wenzangu tuwe hivi hata lini?
Tunakubali kudanganywa na kudaganyika hata lini?

Wewe unayesema Dr Ulimboka aite press conference, kwani unataka kusikia yepi tofauti ya liyokwishasema na video kuwa uploaded kwenye YouTube? Au ni kipi zaidi ya aliyoyaandika Said Kubenea?

Taarifa zote mbili ulizifanyia kazi gani? Je ulichukua hatua gani? Unabaki kuwa mtaalamu wa kuandika kwenye keyboard lakini action iko zero halafu unathubutu kuwaita wengine waoga, wanafiki.

Kaka/dada acha hizo mkuu, haisaidii hata kidogo. Muacheni Dr Ulimboka apumzike na akijiskia kusema lolote au hata kukaa kimya tutauheshimu uamuzi wake. Aliyotufanyia ni makubwa sana katika harakati za haki nchini mwetu

otherwise mtoa thread acha unafiiki, chuki, umbea na uzabizabina. Sioni nikuite neno gani zaidi ya hivyo as it fit your description
 
Nime kutmia pm.

Kwa nini usitaje hapa hadharani mkuu, mimi binafsi siwezi kwa kuwa sina ujasiri huo, Ulimboka is right to keep a low profile for the sake of his life and the lives of those dear to him!
 
watanzania wenzangu tuwe hivi hata lini?
Tunakubali kudanganywa na kudaganyika hata lini?

Wewe unayesema Dr Ulimboka aite press conference, kwani unataka kusikia yepi tofauti ya liyokwishasema na video kuwa uploaded kwenye YouTube? Au ni kipi zaidi ya aliyoyaandika Said Kubenea?

Taarifa zote mbili ulizifanyia kazi gani? Je ulichukua hatua gani? Unabaki kuwa mtaalamu wa kuandika kwenye keyboard lakini action iko zero halafu unathubutu kuwaita wengine waoga, wanafiki.

Kaka/dada acha hizo mkuu, haisaidii hata kidogo. Muacheni Dr Ulimboka apumzike na akijiskia kusema lolote au hata kukaa kimya tutauheshimu uamuzi wake. Aliyotufanyia ni makubwa sana katika harakati za haki nchini mwetu

otherwise mtoa thread acha unafiiki, chuki, umbea na uzabizabina. Sioni nikuite neno gani zaidi ya hivyo as it fit your description

Kama ulikuwa akilini kwangu mkuu!
 
hahahahaha,et kompyuta ya kizamani! Watu wagomvi! Lool, hata kama umechapia spellings kidogo,but well said mkuu!

kuna watu wanapenda kuona wenzao wanatangulia mbele na ku risk maisha yao af wao wanashangilia kwa nyumaaaaa
 
Enzi zetu chuoni wakati wa migomo/kunji tulikuwa tunawajaza watu jazba kwa kutumia ule wimbo maarufu wa solidarity 4 ever af wakikolea wewe unarudi nyuma kule,mabomu na virungu vinawahusu,ndio tabia za baadhi ya watu hapa jf.
 
Enzi zetu chuoni wakati wa migomo/kunji tulikuwa tunawajaza watu jazba kwa kutumia ule wimbo maarufu wa solidarity 4 ever af wakikolea wewe unarudi nyuma kule,mabomu na virungu vinawahusu,ndio tabia za baadhi ya watu hapa jf.

Mkuu tulikuwa wote nini UDSM kati ya 2002-2006 nini? Kunji lilikuwa linahusu sana wakati huo
 
Dr. Ulimboka sema ; hakuna cha ku-risk zaidi ya uliyofanyiwa. Utakufa hata kwa kitu kingine hata ukikwepa kumaliziwa na serikali.
NIELEWEKE:
Mimi siyo usalama , kwahiyo eti nataka jamaa aseme kwanza ili usalama wapate yakutaarifu bila mkanganyiko tena, NO. nataka ukweli uwe 'naked' ila watanzania wafahamu mwanzo mwisho. Tunaposema viongozi wa serikali wanakalia damu iwe na 'sound' zaidi.
 
Kwa hiyo ujasiri wako umeishia kwenye ku-pm, lakini Ulimboka unademand lazima awe na ujasiri wa kuita press!!! interesting...

Watu waoga kutaja majina yao lkn tunataka ulimboka aongee na yeye kashateswa sisi hatujateswa... Good point.. Mi nasemaga uli achukue pesa aendelee na maisha yake coz huwezi cheza na serikali atashindwa tu
 
Ukajha kanunu munntu ughwe!, mbona naye amekudharaau wewe kwa kushindwa kufanyia kazi taarifa alizozitoa!?? tuacheni unafiki jamani
Nibhibhwe ikinyakyusa but nilitaka niseme unamtetea Dr. Ulimboka watakuja kumuua Mwakyembe style. Na kama wewe ni usalama wa taifa njooni mnikamate, nasema hivi Dr. Mwakyembe kategewa kwenye vyakula sumu ya arsenic
 
Mnataka aongee nini mbona alishaongea yote kabla hajaondoka.
Ambae haeleweki ni serikali kwakutochukua hatua juu ya watu waliomwita ulimboka na hatimaye kutekwa!
 
Mbona alishasema jinsi alivyotekwa na kuteswa wakati yuko Muhimbili!!! Mwacheni kijana wa watu apumzike. Sidhani kama ana jipya zaidi ya alichotuambia watanganyika!!!
Huyu ndugu yetu alikumbwa na machungu yaliyomgusa kila mmoja wetu! Nchi nzima ilizizima, na kuamini (nakuweka msisitizo kwenye tunacho fahamu) kua vyombo vya dola ni wabaya. Tukajitolea kwa matibabu yake, hadi kufikishwa hosiptali SA ambapo hata huko tulihisi serikakali ya Tz bado ingaliweza kumfuatilia na kummalizia !. Mimi kama mimi iliniuma sana.

Tunashukuru Mungu, kwa uwezo wake kapona na karejea nchini. Watu walitoa maoni mengi mitandaoni ambayo naamini ilimfikia kua akija aibukie press conference na kuyasema yote. Hataivyo, kutokusema siku ileile hatukushangaa sana maana jamaa lazima apumzike japo kidogo! Na akusanye kumbukumbu vizuri hata kukumbuka simu yake ilipo! .

MY TAKE:
1. Huu muda uliotumia kukusanya kumbukumbu ni mrefu sana,
2. Unajaza wasiwasi.
3. Hicho unacho subiri kwanini usieleze uma?
4. Hukumbuki kua wewe ungalikwisha 'decompose' (inaniuma sana)
5. Unaumiza vichwa vya watanzania wengine wapenda haki.
6. Vikao na kamati za serikali ni vyanini tena wakati walipopanda gari kukuacha Msituni usiku walijua wamekuua?
7. Utakayo yasema hata sasahivi, bado kutakua na hojaji tofauti kisa kutokuaminika tena.
8. Kumbuka ulishasema watu waachane na familia yako , wewe ndio ufahamuye ukweli.
9. Kumbuka kuna mengi yaliyo wakumba wanao kutetea
10. Mods naombeni msichanganye hii thread na ile inayosema " polisi leo kufunguka. . . . "
 
Nakupongeza dr ulimboka kwa kukaa kimya maana umegundua kuwa madaktari uliowapigania wamekusaliti, kupigwa kwako wakati mgomo ukiwa umepamba moto ilipaswa iwe chachu na moto wa kugoma mpaka kieleweke ktk madai uliyokuwa unadai kwa niaba yao. Nakumbuka uliwaachia usia kuwa DAMU YAKO ISIMWAGIKE BURE,,lakini madaktari wa bongo baada ya kutishwa kidogo wakarudi kazini na wengine hawakugoma kabisa!!

my take: 1:umejitoa vya kutosha na asiyeona kujitoa kwako achana nae, maana pamoja na kuwa si mfanyakazi wa serikali lakini uliwapiganiama dr wa serikali na mazingira yao lakini mwishowe wamekutosa na kuungana na baba yao serikali.
3: rafiki yako wa kweli si deo ,ila ni wanaharakati na gazeti la mwanahalisi, kwa hiyo siku ukiamua kusema basi bora usemee mwanahalisi lifunguliwe maana tunaoathilika ni wengi kwa kukosa habari.
 
Mwacheni Ulimboka atulie yaliyomkuta si haba jitokezeni mashujaa wengine; yeye sio chizi ana familia inamtegema; wale mashujaa waliokufa Arusha hivi mnahudumia familia zao? Huu ni wakati muafaka kwa shujaa mwengine kujitokeza; msipige porojo ndani ya JF jitokezeni; ushujaa ni kama mbio za vijiti watu hukimbia kwa kupokezana yeye amemaliza ngwe yake!

Chama
Puerto Vallarta enroute to Gongo la mboto.
 
Wabongo mnapenda kuskia stori tu..hamna lolote nyie..unataka akishatoa press conference upost hapa jf "haya movie hiyo, season II, wapi pop corns"...garbage tu..alisema mtu juzi hapa, ni kipi ambacho ulimboka hajakisema hata sasa?? na wewe kama mtanzania mwenye mapenzi mema naye umeyafanyia kazi gani?..Pengine Ulimboka amegundua kuwa anapigania haki za watu waoga sana wasiotaka kusimama dhidi ya udhalimu wa serikali yao kwa hivyo ameamua kuachilia mbali mapambano.

Wale madokta waliorudi kazini tu walikuwa alama tosha ya kushindwa kuuenzi upambanaji wake..mwatakani???
 
Tatizo sio ulimboka tatizo ni nyinyi madaktari mliokubali kurudi kazini wakati mwenzenu akiwa maututi. Na sasa hivi mnaendelea na kazi lakini mnataka yeye andelee na libeneke.
 
Mwacheni Doctor apate muda wa kupumzika kwani bado hajawa fit kiasi hicho... kuanza misukosuko tena licha yeye kusema yupo fit pale airport siku alipowasili... lkn kwa nilivyomuona...bado anahitaji mapumziko.
 
Back
Top Bottom