Katika kuthibitisha kwamba Dk. Ulimboka hayuko tayari kusema chochote, juzi gazeti hili lilikutana nae katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Ubungo ambapo alisema kuwa kitendo cha kinyama alichofanyiwa, anamwachia Mungu.
Source: Tanzania Daima
teh teh teh..imekaa vibaya, hii bado haijatulia! Sijui ule wimbo aliuimba nani. In short, kutulia ni muhimu sana maana papara na haraka haraka bila kuwa na matayarisho ya kueleweka unaweza kukosea step.
mi nadhani ni kuwa na amani ni kulinda usalama wako na ustawi wa familia yako.
Utamu wa ngoma ingia ndani ucheze, asidanganywe na wanaojifanya kum suport wkt hawaathiriki moja kwa moja na kilicho mkuta au kitakacho mkuta.
Dr ni mtu mzima, msomi mwenye akili zake timamu.
Atachagua lili lililobora zaidi kwa maslahi yake na familia yake kwa ujumla.
MamaJack, huhitaji kuwa Dr. Ulimboka kutetea maslahi fulani, hata wewe unaweza kutetea unaloamini na kuwa mfano au ukawa role mode wa wengine. Kwa kipindi chote ambacho Dr. alikuwa kwenye matatizo tumefanya nini especially kwa familia yake..... Talking is cheap
None of ya'll can take care of his family zaidi ya kumjaza upepo halafu mwisho wa siku kila mtu na maisha yake.ni juu yake kuchagua kati ya heahima na utu wake au pesa, asiposema atakuwa amewasaliti wote waliomsapoti, just too bad.
Tutasikia mengi sana kabla dr.ulimboka hajafunguka......funguka dr funguka!!!!!!
daah tuliguswa sana juu ya unyama alio fanyiwa ndugu yetu.ukweli kama hatataja watu husika wa kisa hiki basi usaliti huu juu ya watu wote utamtafuna.
Amekaa ametafakari kwa kina na amejua mchezo wote mwanzo hadi mwisho amesikitika sana ndio maana amesema anamuachia Mungu. ninasikitika kusema "mission failed"
Ikiwa hivyo basi wamejitumbukiza kwenye deni, na hili deni litakuja kudaiwa 2015Siku Ullimboka akifunguka na kueleza ukweli kwamba kuna ranks za TISS zikishirikiana na CHADEMA zilifanya mpango mzima wa utekaji ndio watanzania watajua kwa nini aliamua kumuachia mungu. Kwani watu aliowategemea wangemsaidia ndio walitaka kumuua ili kujipatia umaarufu na huruma kutoka kwa Watanzania.
Bwana Mkubwa jamaa amebaini ukweli na ameamua kulichukulia hili jambo kama lake binafsi hata hivyo yeye si mwanasiasaWote tulikua na wasiwasi nae tangu tune Kauli sake zikibadilika. Lakini uamuzi wake itakula kwako, Utakua huna Tofauti na nao waliookufanyia ushenzi huo, lakini how about watanzania wote.waliokupigania wakiamini Utakua chanzo cha,ukombozi wao? How about mwanahalisi lililofungwa kwa kukupigania? Stupid Mtanzania, Mimi ntakuchukia sana kwa ujinga wako, who are you protecting wakati wanaharakati wana taffeta evidence ya,kuwapeleka Wakina Nzoka the Hague?
Ameona tatizo kwamba akija akiongea yale mambo ambaye ni kinyume cha wengi wanavyotegemea iwe itakuwa tatizo. kwani ni rahisi sana kusema amepewa kitu kidogo na serikali. kuhusu usalama wake nadhani serikali ndiyo msitari wao wa mwisho wa kujilinda hivyo ni jukumu lao kumlinda. Mkuu alikwisha sema wanamuhitaji mno Dr Uli katika mazungumzo yao na serikali haihusiki katika unyama huo na kama kuna mtu ndani ya serikali alifanya hivyo basi hakufanya kwa niaba ya serikali. Kwahiyo inawezerkana ni watu wa serikali walifanya kwa niaba ya watu fulani na hili ndilo limempa Kamanda Uli tabu kuliongelea hadharani kwani litaleta mkanganyiko mkubwa sana katika jamiiMadaktari wenzake wakajitolea kufa na kupona, wakahakikisha inapigwa harambee fasta, akapelekwa sauzi tena chini ya ulinzi mkali, yote kwa ajli ya maisha yake, hiyo yote igeuke kuwa bure jamani! hapana haifai hata kidogo, kama unavyosema bila support hiyo saa hizi angekuwa historia, tena ndio kesi ingeisha kiulaini kabisa. post namba 30 hapo juu mohamedi tantawi anasema tumwache apiganie uzima wake, huo uzima angeupata wapi bila support ya hao anaotaka kuwasaliti sasa (kama ni kweli). Halafu kumbuka mohamedi, hili siyo suala la kisiasa tena ni suala la ubakaji wa haki za binadamu,
Pia lazima muelewe kwamba siri haiwezi kufichwa daima, huwa inamkereketa mtu kuisema, kwa hiyo ataitoa kwa mtu wake wa karibu na kumwambia usimwambie mtu, na huyo naye atampata mshikaji wake atamwambia na kumpa masharti kama hayo ya kutomwambia mtu... yani ni kama mtandao wa 'tuko wangapi' unavyokuwa. sasa kwa kuhofia hilo sidhani kama....
Huyu dokta asitake kutuzingua hapa aseme kilichomkuta atakuwa salama zaidi kwa sababu watesi wake hawatakuwa na haja naye tena baada ya ukweli kuwa umewekwa wazi labda kama ni kwa ajili ya kulipa kisasi tu baada ya kuumbuliwa, na sijuji huko alikokuwa anakutana nao kama hawajamwambukiza kitu.