Dr Slaa ninamashaka na upeo wako,,!!

Dr Slaa ninamashaka na upeo wako,,!!

security guard

JF-Expert Member
Joined
Sep 27, 2011
Posts
799
Reaction score
603
NINA MASHAKA NA UPEO WA Dr SLAA,,!!

Leo vyombo vya habari vimeripoti kuwa Dr Slaa anamlaumu Katibu Mkuu wa CCM kutaka kuhujumu mwenendo wa Kesi ya rufaa ya Tundu Lisu kwakuweka wanasheria makini kuhakikisha Lisu anashindwa kesi hii,,!!

Kwanza anachokifanya dr slaa nikuingilia uhuru wa mahakama kwakujadili kesi iliyoko mahakamani,,huu ni uhuni na uvunjifu wa sheria amabo sikutegemea kiongozi wa juu wa chama kufanya.!

Pili mtu yeyote mwenye kesi mahakamani ana haki yakuomba msaada wakisheria kama anahitaji bila kujali msaada huo anupata kwa nani?awe ni Kinana au Mwanakijiji kutoka Singida,,hivyo walalamikaji kama wameomba msaada wakupatiwa mawakili sheria haikatazi,,!

Tatu,tumeshuhudia kesi nyingi za rufaa ambazo chadema wameshinda,,Arusha,Ubungo kwa uchache wake lakini viongozi wa chadema walikuwa wa kwanza kuisifu mahakama iweje leo wakose uvumilivu nakuiacha mahakama ifanye kazi yake?mbona CCM haikulalamika kwenye kesi chadema walizoshinda?

Nne,,Kinana ni kiongozi makini,hajawahi wala haitatokea akafanya upuuzi wa namna hii,,kama dr slaa anaushahidi na anacho zungumza ni vema akakiweka hadharani badala yakuwahadaa watanzania anapoona hali ya kesi inambana Lisu,,!!

Mwisho,,Ushauri wangu kwa huyu babu,Kinana siyo saizi yako utapasuka mapafu ukitaka kushindana nae,,badala yakutunga uongo na majungu ungetumia muda huu kujenga chama chenu na kujifunza kutoka kwa CCM,,!!
 
Hoja zako zote ni nzuri but ziko out of topic. Slaa hajalalamika kuwekwa kwa mawakili wazuri... Kasome tena lile tamko alafu urudi.... Limeandikwa kiswahili tu...
 
Hoja zako zote ni nzuri but ziko out of topic. Slaa hajalalamika kuwekwa kwa mawakili wazuri... Kasome tena lile tamko alafu urudi.... Limeandikwa kiswahili tu...

ahsante kwa kumfafanulia mkuu
 
Maelezo mengi yasiyo na maana kama hujui kaa kimya sio lazima kuandika usichokijua wewe ni cuf nn?
 
Hoja zako zote ni nzuri but ziko out of topic. Slaa hajalalamika kuwekwa kwa mawakili wazuri... Kasome tena lile tamko alafu urudi.... Limeandikwa kiswahili tu...
Mkuu katika mambo ya kijamii yaliyomengi ni mweupe sana anajua mambo ya kanisa tu japo nayo yalimshinda kuyaishi.
 
NINA MASHAKA NA UPEO WA Dr SLAA,,!!
Mwisho,,Ushauri wangu kwa huyu babu,Kinana siyo saizi yako utapasuka mapafu ukitaka kushindana nae,,badala yakutunga uongo na majungu ungetumia muda huu kujenga chama chenu na kujifunza kutoka kwa CCM,,!!

Kama vipimo vya upeo ni mlingotini Bagamoyo ni kweli hatakidhi, kama shule huna jinsi maana si wewe JK na CCM nzima hakuna mwenye uwezo wa kupima uwezo wa DR. Slaa.

Kinana ni msomali aliyefuzu ujangili period kakutana na dhaifu wanahangaika kuongoza akili kubwa.
 
Babu anatumika kutuhujumu.
Tena kuna tetese kwamba 'magamba'wanapanga kumtumia ili kukipoteza CHADEMA kabla ya mwaka 2015.

Wanachadema tusipokua makini huyu mzee atatuhalibia safari yetu ya ukombozi.

Babu must go bhana!
 
Wabongo wavivu sana wa kusoma,yale yale ya cuf,unalipuka tu na badae unarejea kwenye mstari,kesi haijapewa hata number pili walalamikaji hawajashirikishwa na zaidi ya hapo kesi ishapitisha mwaka mzima kwa hyo ukienda ifungua tena unakiuka sharia za nchi sasa kinana anataka kesi isikilizwa upya ana maana gani? wenye akili timamu tumeelewa wewe kaa hivyo hivyo
 
Hivi Tanzania hakuna siasa bila Dr Slaa?
Hivi mnadhani kumuandika sana ndio kuichafua CDM? Imefika mahali tukiona thread kichwa cha habari ni Dr Slaa wengine hatakuisoma hawataki maana ni hoja za kitoto tu!
 
Usipende kukurupuka, tafuta ripoti yote ya press conference ya jana naamini ukishaisoma utaondoa hii takataka yako maana kwa sasa inakudharirisha.
 
Hivi Tanzania hakuna siasa bila Dr Slaa?
Hivi mnadhani kumuandika sana ndio kuichafua CDM? Imefika mahali tukiona thread kichwa cha habari ni Dr Slaa wengine hatakuisoma hawataki maana ni hoja za kitoto tu!
Kweli mkuu,hakuna siku haijaja hoja kuhusu Dr.Slaa,mpaka rangi za kucha zake wataleta hapa,hakuna hoja zenye tija kabisa
 
Hivi Tanzania hakuna siasa bila Dr Slaa?
Hivi mnadhani kumuandika sana ndio kuichafua CDM? Imefika mahali tukiona thread kichwa cha habari ni Dr Slaa wengine hatakuisoma hawataki maana ni hoja za kitoto tu!

ni kweli mkuu hata mimi cjasoma nimekoment tu
 
mkuu nafikiri hujaelewa alichosema dr hebu kasome tena au sikiliza kama una video. kwa msaada tu kidogo nikwamba hiyo kesi haiko mahakamni ndo wako kwenye mchakato wakuifungua, tatizo nikwamba wanaosemekana wameifungua wamekana wao hawajafungua tena kwa kiapo, na doc zinaonyesha waliofungua tatizo lake liko wapi, hata kama wakatimwingine mkistukiwa inauma vumilia tu ndo siasa mkuu.
 
Hoja zako zote ni nzuri but ziko out of topic. Slaa hajalalamika kuwekwa kwa mawakili wazuri... Kasome tena lile tamko alafu urudi.... Limeandikwa kiswahili tu...

Upeo wake ndo mdogo,mana hata hajaelewa tamko la Chadema.
 
Mkuu katika mambo ya kijamii yaliyomengi ni mweupe sana anajua mambo ya kanisa tu japo nayo yalimshinda kuyaishi.

NA ndiye atakayekuja kuwa rais wako, wewe pamoja na Waliberali wenzako.
 
Kijana nakushauri, kabla hujaanza kuhoji upeo wa watu wengine, anza kwanza kuhoji upeo wako. Kwa ulichokiandika hapa umepoteza sifa ya kuhoji upeo wa Dr. Slaa. Kwanza inaonekana hii ishu umehadithiwa au kama hujahadithiwa basi tukubaliane tu kuwa upeo wako hautoshi kuchambua hii issue hivyo ni vyema ukabaki kuwa msomaji wa hoja za wenzako ili ugain some understanding about the issue in question.

Kama ungekuja kwa busara kuuliza nini kimetokea tungeweza kukuelekeza, ila kwa kuwa umekuja macho juu acha tu tukulipue. Kwanza fahamu tu kuwa upeo wako wewe ni wa kushikisha na gundi. Sisi wenzako wakuelewa tumeshaelewa kuwa Kinana zaidi ya kuwa jangiri, pia ni mbakaji wa haki!

Kusema kuwa anaingilia mwenendo wa kesi au uhuru wa mahakama, wewe unaona kuna kesi gani hasa inayoingiliwa kwa Dr Slaa kusema aliyoyasema?? Hebu tutajie ni kesi gan! Usiwe unakurupuka tu. Hadi sasa hivi hakuna kesi bado hivyo kama ulihadithiwa aliyekupa story hizo amekumislead.

Kuhusu haki ya kukata rufaa ni kweli mhukumiwa anayohaki ya kukata rufaa kupinga hukumu iliyotolewa dhidi yake, lakin unafahamu kuwa katika issue hii wahukumiwa sio waliokata rufaa??? Unafahamu kuwa mmoja wa wahukumiwa sasa hiv ni mwanachama wa chadema na hayupo tena CCM??? Wewe hujui unachoongea, kaa kimya kijana na dont be reckless in your choice of words.

Ushahidi wa anachokiongelea Dr. Slaa upo humuhumu mtandandaoni acha uvivu take your time to read and usikurupuke tu. Mwisho kabisa ushauri wako naukataa sababu huna sifa ya kutushauri kwenye suala hili kwa maana wewe mwenyewe hujui hata unaongea nini, sisi ndo tukushauri wewe kuwa rudi kasome na ukielewe anachokiongelea Dr. Slaa.
 
Back
Top Bottom