Dr Slaa ninamashaka na upeo wako,,!!

Dr Slaa ninamashaka na upeo wako,,!!

Kwanza ma-ccm neno upeo mlikuja kujua kwa dr.slaa,afu mleta mada hata hajalisoma tamko la dr.slaa ndo mana sintamjibu huyu mpuuzi wa lumumba kichwa kama mkama
 
NINA MASHAKA NA UPEO WA Dr SLAA,,!!

Leo vyombo vya habari vimeripoti kuwa Dr Slaa anamlaumu Katibu Mkuu wa CCM kutaka kuhujumu mwenendo wa Kesi ya rufaa ya Tundu Lisu kwakuweka wanasheria makini kuhakikisha Lisu anashindwa kesi hii,,!!

Kwanza anachokifanya dr slaa nikuingilia uhuru wa mahakama kwakujadili kesi iliyoko mahakamani,,huu ni uhuni na uvunjifu wa sheria amabo sikutegemea kiongozi wa juu wa chama kufanya.!

Pili mtu yeyote mwenye kesi mahakamani ana haki yakuomba msaada wakisheria kama anahitaji bila kujali msaada huo anupata kwa nani?awe ni Kinana au Mwanakijiji kutoka Singida,,hivyo walalamikaji kama wameomba msaada wakupatiwa mawakili sheria haikatazi,,!

Tatu,tumeshuhudia kesi nyingi za rufaa ambazo chadema wameshinda,,Arusha,Ubungo kwa uchache wake lakini viongozi wa chadema walikuwa wa kwanza kuisifu mahakama iweje leo wakose uvumilivu nakuiacha mahakama ifanye kazi yake?mbona CCM haikulalamika kwenye kesi chadema walizoshinda?

Nne,,Kinana ni kiongozi makini,hajawahi wala haitatokea akafanya upuuzi wa namna hii,,kama dr slaa anaushahidi na anacho zungumza ni vema akakiweka hadharani badala yakuwahadaa watanzania anapoona hali ya kesi inambana Lisu,,!!

Mwisho,,Ushauri wangu kwa huyu babu,Kinana siyo saizi yako utapasuka mapafu ukitaka kushindana nae,,badala yakutunga uongo na majungu ungetumia muda huu kujenga chama chenu na kujifunza kutoka kwa CCM,,!!

eti kumbe wewe ndo jangili unaemsaidia alshabab kinana kuua tembo wetu e.lazma mtalipa ifikapo 2015.
 
Mzee slaa anazeeka vibaya, alichonichekesha zaidi ni pale alipokemea wakuu wa mikoa kumiliki magari ya 2oomilioni ili hali yeye mwenyewe alifika kiwanjani alipokuwa anapiga porojo hizo na gari ya gharama hiyohiyo. Kama siyo kuzeeka vibaya nini? Tumsamehe
 
Masalia bwana mumefanya hazina na ruzuku ya CCM iishe kwa sababu book saba kwa watu zaidi ya 200 kwenye mitandao,kimefirisi kisima cha CCM,Kinana ni jangiri wa wanyama wetu na ni jangiri wa siasa za nchi hii anaendesha umafia wa kisiasa utafikiri tuko Somalia alikotoka akiwa na miaka saba ,vile vinasaba vya fujo kakua navyo na hata sasa anamiaka kibao bado hajabadirika,huwezi kuwa juu ya sharia za nchi kwa kutumia majaji wasio na heshima na kazi zao kuwanyamazisha watu na kujidai kwamba hakuna atakayekuweza, na haya yote ni michoro ya Kikwete, ujinga wao wakufinyanga na kuharibu kila chombo cha dola kumefanya nchi iwe vitani,Polisi,DPP,Mahakama wote wanafanya kazi za mwenyekiti na secretariat yake, ni waovu wanaharibu nchi wanatengeneza chuki kubwa miongoni mwa wananchi, wabaya hao
 
Mzee slaa anazeeka vibaya, alichonichekesha zaidi ni pale alipokemea wakuu wa mikoa kumiliki magari ya 2oomilioni ili hali yeye mwenyewe alifika kiwanjani alipokuwa anapiga porojo hizo na gari ya gharama hiyohiyo. Kama siyo kuzeeka vibaya nini? Tumsamehe
Gari alikopeshwa akiwa bungeni na amelipa,wakuu wamikoa magari ni fedha ya serikali,uzee wa Slaa huwezi kuulinganisha na wa Kikwete ambaye nyumbani kwake siku hizi ni nchi za watu,huyo ndio utakayesema kazeeka vibaya anakimbia wananchi,hawezi kukaa nao,nchi inayumba sijui kile kifafa cha kuanguka anguka kimemla ubongo
 
Babu anatumika kutuhujumu.
Tena kuna tetese kwamba 'magamba'wanapanga kumtumia ili kukipoteza CHADEMA kabla ya mwaka 2015.

Wanachadema tusipokua makini huyu mzee atatuhalibia safari yetu ya ukombozi.

Babu must go bhana!

Bongo lala mkubwa!!
 
Kuwa na upungufu wa kinga za mwili ni hatari na ina athiri hata uwezo wa kufikiri msamaha hapa lazima uhusishwe
 
Babu anatapa tapa,,huwezi kuhubiri usichokifanya,,!!akapumzike karatu awaachie watu makini waendeshe chama,,!!
 
Maccm mburula sana kisheria rufaa inatakiwa isajiriwe ndani ya mwaka mmoja ikizidi huo muda kwishney ccm inakufa slowly
 
Hivi Tanzania hakuna siasa bila Dr Slaa?
Hivi mnadhani kumuandika sana ndio kuichafua CDM? Imefika mahali tukiona thread kichwa cha habari ni Dr Slaa wengine hatakuisoma hawataki maana ni hoja za kitoto tu!

Naunga mkono hoja

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom