Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,707
Wakati anaamua kuachana na kazi ya kiroho,hakuiacha kwa kashfa mbaya,bali aliamua kufanya shughuli nyingine ya kuisaidia jamii,alipoingia kwenye siasa akagundua mambo hayaendi sawa,yeye kama Mtanzania na binadam amechukua jukumu la kuimbia jamii uovu unaotendeka,amewataja wanaoidhulumu jamii kwa majina,bahati mbaya hawajachukuliwa hatua zozote coz wanaotakiwa kushtakiwa ndo haohao washitaki,wamedai wamechafuliwa,wameshindwa kujisafisha bado wapo madarakani wanaendelea kuivuruga nchi,maisha ya Watanzania hayana mbele wala nyuma,asilimia 85 ya watanzania wanaishi bila umeme na kwenye nyumba za matope,Dr Slaa akawaambia hawa wanyonge kwenye kampeni za uchaguzi kuwa atawashushia gharama za ujenzi ili wanyonge hawa watoke kwenye matope,wezi wa haki za wanyonge wakamwambia anachofanya ni ndoto ya mchana,akawaeleza namna atakavyopunguza gharama hizo na pia atafanya elimu bure kutoka darasa la kwanza mpaka form 6 wakakosa hoja,wakadai ameiba mke wa mtu walipoona hoja hiyo haina mashiko wakamuibia kura akawaambia wazi wahusika,wameingia madarakani wamepandisha zaidi gharama za maisha,Dk Slaa amewaambia watanzania wasikubali kwa maandamano wamemuita mtu hatari kwa taifa,15% ya Watanzania ndo wana umeme,hata hao wachache wameshindwa kuwapa huo umeme,unakuwa wa mgao kila siku ili wauze magenereta yao,huduma za jamii wamezifanya kuwa za wenye hela yaani anasa,ukitaka kuwa na umeme,matibabu mazuri,maji safi ya kunywa,usafiri wa uhakika,shule nzuri n.k ni lazima uwe kwenye"sistimu"hii chafu au uwe mwizi wakukamate wajisifu wamekamata jambazi wakati na wao ni majambazi wakubwa,jamani nasikia kizunguzungu hivi nisaidieni