Dr. Slaa makampuni yasiyorejesha pesa za EPA hadharani

Tunashukuru kwa taarifa nzuri sana ila tunaomba uwe wazi hapa:

(Hata hivyo, alizitaja kampuni 13 ambazo zimegoma kurejesha fedha hizo (majina tunayo) na kwamba hazijalipa jumla ya fedha zote zinazokisiwa kufikia sh bilioni 50.)

Mwanahalisi itayaanika yote wiki ijayo
 
Huyu Slaa hana mambo mengine ya msingi ya kufanya? Anachoona TZ hii ni ufisadi na EPA tu?
Ni muda muafaka kwake kubadilika, tunataka kusikia mambo mapya kutoka kwake, siyo haya ambayo yameshaota sugu masikioni mwetu!!

Hakika fisadi hajifichi
 
Mbona gazeti halijataja makampuni mbayo hayajarudisha hizo pesa. Kumbe serikali ilijitahidi wote hao wamerudisha mabilioni. Hapa JK alicheza. Kama angekurupuka awaburuze mahakama nadhani ingekuwa ngumu kuzipata hizo pesa kwa kuwa unaweza kukuta makampuni mengine yamejifilisi.

Nadhani kitu muhimu ilikuwa kuzipata kwanza hizo pesa.

Hivi yule jamaa aliyefunguliwa mashitaka na kupatikana na hatia sijui anaitwa Farijala amerudisha kiasi gani baada ya kufungwa?
 
Hakika fisadi hajifichi

Hana ufisadi wowote,ni aliyejaa na njaa kiasi kwamba kawa mvivu hata wa kufikiri kwa mambo yanayofikirika hata na wadogo zetu wa nursery schools,Dr hakizungumzia ugumu na hali ya kupananda kwa maisha tena juzi tu yeye Rajeo hajaliona au kwa kua mvivu wa kufikiri kaliona sio jipya!na hata suala la Epa na ufisadi bado kama watanzania hatujapata majibu kwa vyombo stahiki kua hatima yake imefikia wapi,sasa yeye anaposema Dr hana jipya la kuongea kwani hayo ya epa na ufisadi yalimalizwa kikamilifu na watanzania kujua?ajaribu kufikiri kwa brain na si kwa
 
Huyu Slaa hana mambo mengine ya msingi ya kufanya? Anachoona TZ hii ni ufisadi na EPA tu?
Ni muda muafaka kwake kubadilika, tunataka kusikia mambo mapya kutoka kwake, siyo haya ambayo yameshaota sugu masikioni mwetu!!

kuna lingine nch hii zaid ya ufsad? Sema wewe lngne, mbona la tumethubutu, tumeweza na tunasonga mbele nalo limeota usugu masikion mwetu, alaf husem
 
Mbona gazeti limetuficha hizo kampuni ambazo hazikurejesha fedha zetu jamani, nina hiamini JF ni jukwaa huru, naomba mtu mwenye hayo majina ya hizo kampuni ambazo hazikurejesha pesa zetu hatuwekee hapa Jamvini;

"Hata hivyo, alizitaja kampuni 13 ambazo zimegoma kurejesha fedha hizo (majina tunayo) na kwamba hazijalipa jumla ya fedha zote zinazokisiwa kufikia sh bilioni 50"

Natumaini inaeleweka kutokana na kitu kinachoeleweka kama uamuzi wa busara kutoweka hapa, ila ipo siku mambo yatawekwa hadharani. Gazeti kama mnavyojua tasmini ya wahariri wanapoweka kitu hadharani lazima utafiti ufanyike na kujiridhisha, vinginevyo wakigeuziwa kibao hawatakuwa na pakutokea ingawa Dr. ameanika hadharani.

Nadhani Vyombo vya habari vinafanya jitihada kuhakiki makampuni hayo yasiyolipa na ukweli utaanikwa hadharani punde tu. Thanks.
 
Natumaini inaeleweka kutokana na kitu kinachoeleweka kama uamuzi wa busara kutoweka hapa, ila ipo siku mambo yatawekwa hadharani. Gazeti kama mnavyojua tasmini ya wahariri wanapoweka kitu hadharani lazima utafiti ufanyike na kujiridhisha, vinginevyo wakigeuziwa kibao hawatakuwa na pakutokea ingawa Dr. ameanika hadharani.

Nadhani Vyombo vya habari vinafanya jitihada kuhakiki makampuni hayo yasiyolipa na ukweli utaanikwa hadharani punde tu. Thanks.

Nimeipenda hii mkuu,imekaa vizuri sana!
 
Slaa kweli ni "opportunist" kwani anajuwa kabisa kuwa hili jambo linashughulikiwa na Serikali na Takukuru na anajuwa kabisa kuwa karibu litatangazwa, anawahi aonekane yeye ndio kaliibuwa. Amma kweli mfa maji haishi kutapatapa.

Hiyo serikali yako legelege au
 
Kwa mtazamo huo huna tofauti na kichaa anaeokota kopo ubungo hajui chochote Tz.ungependa akizungumzia nini?au akusifu we mzuri.
 
Serikali ya JK aibu ilishafutika katika nyuso zao, subiri tu utakuja sikia wanaibuka kwa kuwahutubia wazee wa DMS

Wamezeeka fikra na hata utendaji ni dhahiri kabisa Jk siku za kukaa ikulu ni zinahesabika otherwise Tz hapatakalika
 
Slaa kweli ni "opportunist" kwani anajuwa kabisa kuwa hili jambo linashughulikiwa na Serikali na Takukuru na anajuwa kabisa kuwa karibu litatangazwa, anawahi aonekane yeye ndio kaliibuwa. Amma kweli mfa maji haishi kutapatapa.

He is a politician. what do you expect from him? playing with cards, all politicians do so
 
Slaa kweli ni "opportunist" kwani anajuwa kabisa kuwa hili jambo linashughulikiwa na Serikali na Takukuru na anajuwa kabisa kuwa karibu litatangazwa, anawahi aonekane yeye ndio kaliibuwa. Amma kweli mfa maji haishi kutapatapa.

Angalia ulivyo na ufinyu wa kufikiri ingekuwa wanafanyia uchunguzi si ingalikuwa ushakamilika siku zote? Ishu hata ni wao kushirikiana na Jk ktk wizi huo ikiwemo heka ccm walizotumia kupigia kampeni 2005 ni za EPA
 
i
:peep::peep: IF WISHES WERE HORSES EVERY BODY WOULD CHOOSE CHADEMA TO BE THE RULING PARTY AND THAT WILL
THE END OF CORRUPT AND IRRESPONSIBLE LEADERSHIP.LIVE LONG DR WA UKWELI.
 
Slaa alipua kombora jingine
Dr. Slaa makampuni yasiyorejesha pesa za EPA hadharani


Hata hivyo, alizitaja kampuni 13 ambazo zimegoma kurejesha fedha hizo (majina tunayo) na kwamba hazijalipa jumla ya fedha zote zinazokisiwa kufikia sh bilioni 50.

Tunaambiwa hadharani kisha mnaogopa kutaja? Dr. Mwenyewe aliyataja, kisha gazeti lenu la TzDaima linaogopa kusema tuwaeleweje?
 
Back
Top Bottom