Dr Slaa hajapona mkono?

Dr Slaa hajapona mkono?

Eeka Mangi

JF-Expert Member
Joined
Jul 27, 2008
Posts
3,173
Reaction score
486
Jama nimemwona Dr wetu, Dr Slaa! Hivi kumbe ile ajali alopata wakati wa kampeni umemlemaza mkono. Hope Mungu atamjalia apone.
 
Jama nimemwona Dr wetu, Dr Slaa! Hivi kumbe ile ajali alopata wakati wa kampeni umemlemaza mkono. Hope Mungu atamjalia apone.

Kwa sisi ambao hatukumwona hatuna hakika unazungumzia nini mkuu. Ulemavu gani huo?
 
Kwa sisi ambao hatukumwona hatuna hakika unazungumzia nini mkuu. Ulemavu gani huo?

Nimeona mkono wake wa kushoto umesinyaa mkuu na nahisi kiwango chake cha kufanya kazi ni hafifu. Ushikaji wake wa kitu sio kwa uimara sana.
 
Jama nimemwona Dr wetu, Dr Slaa! Hivi kumbe ile ajali alopata wakati wa kampeni umemlemaza mkono. Hope Mungu atamjalia apone.
Mkuu,
Umefanya ufuatiliaji wa ishu hii japo kidogo, au macho yako tu?
 
Mkuu,
Umefanya ufuatiliaji wa ishu hii japo kidogo, au macho yako tu?

Nimeyaamini macho yangu kaka. Kwa walioona taarifa ya habari ya saa mbili watakubalina nami mkuu.
 
Nimeyaamini macho yangu kaka. Kwa walioona taarifa ya habari ya saa mbili watakubalina nami mkuu.

Nimeangalia taarifa ya habari ITV sikubaliani na wewe! Labda kama unajicho la kichawi
 
Ni kweli kwa kiasi flani, Dr. Slaa hajapona mkono kikamilifu.

Huwa nashangaa anapoingia JF na kuandika kw kirefu kuwajibu watanzania hoja zao, ni jitihada ya ziada na inafurahisha kuona hachoki kuja kushiriki discussions. Nadhani atapona siku si nyingi.
 
Mkono ukifungwa plaster au haswa ile POP kwa munda mrefu huwa unasinyaa kidogo. Hiyo ni kawaida, Labda ndilo lililotokea.
 
Nimeona mkono wake wa kushoto umesinyaa mkuu na nahisi kiwango chake cha kufanya kazi ni hafifu. Ushikaji wake wa kitu sio kwa uimara sana.
Hakufanyiwa physical therapy ya kutosha?
 
Tunaomba kama kuna daktari wake aje ajibu hoja hii ili tuelewe. Wengine tutajikanyaga mno maana hatuna majibu sahihi saana
 
Wepesi wa kupona unatofautiana sana kati ya mtoto na mtu mzima aliyevunjika.
Yeye ni mtu mzima, hatapona kwa haraka kama mtoto.
Yet, I'm wishing quick recovery.
 
Tunakuombea Dr. upone haraka na uwe mzima taifa linakuhitaji sana
 
Duh,bole sana boss,..
ungekua raisi labda na wewe ungeenda kutibiwa uingeleza,..
Get well soon
 
Nilisikia alidondoka bafuni! Sijui hata alikua anafanya nini mpaka akateleza na kudondoka jamani! Get well soon Dokta
 
Duh, sasa tukiwa na Rais mlemavu itakuwa vipi tena? Atashikana vipi mikono na Obama? Haijatulia kabisa. Namwombea apone mapema.
 
Back
Top Bottom