Nchi ikija kupata machafuko hii,mods wa jamii forum watakuja kujibu baadhi ya mambo ya uchochezi ndani ya hii jamii,tumeona nchi zilizopata machafuko,source na chuki zote zinaanzaga kwenye mitandao ya kijamii,huko nyuma zilikuwa zinatumika redio na tv na wahusika wamechukuliwa hatua za kinidhamu kwa kuruhusu ama kwa kueneza chuki ndani ya jamii.Na hili ndilo ninaloliona katika jukwaa hili linalojipambanua kama ni jukwaa la siasa,wakati si kweli,hili ni jukwaa la kueneza chuki ndani ya jamii ya Kitanzania.Nimejaribu kuweka uzi wa kuwaomba kusimamia hili jukwaa kukaa kwenye sera yao ya kisiasa,lakini uzi umeondolewa kwa makusudi tu ili kuruhusu upuuzi uendelee kutawala hili jukwaa.Niseme kazi yangu ya kushauri nimeimaliza yatakayofuata si kazi yangu.