Nikupe pole sana kwa maumivu unayoyapata kutokana na taarifa hii. Mimi binafsi sina chama. Nilikuwa mwanachama wa TANU zamani lakini baada ya Nyerere kufariki, nikaona ccm imeivamiwa na uzimwi, nikachoma kadi yangu mimi mwenyewe. Lakini sasa ninadhani kuna haja ya kujiunga na chama cha siasa ila si ccm ili tulikomboe taifa kwa maslahi ya ninyi vijana na vizazi vyetu.
Kwa kukusaidia, rudi nyuma hatua moja, vuta pumzi nyingi kwa nguvu na iitunze kwenye mapafu na kuitoa mara tano. Sasa urudi kwenye hoja:-
1. Wewe unaongelea takwimu ulizozitoa kwenye database ya mwaka gani na pia ujua mtoa taarifa anatumia database ya lini.
2. Tangu ulipo update takwimu zako kwa mara ya mwisho, ni mambo gani yametokea katika jamii na ndani ya ccm na chadema ambayo yamekifanya ccm kiendelee kuwa imara na wanachama wake ama kukidhoofisha kikimbiwe na watu.
3. Sambamba na 2 hapo juu, fikiria ni ninin kinaendelea kwa CHADEMA ambacho unaona kinasababisha CHADEMA isiongeze wanachama ama ikue na kusambaa sana.
4. Unapoongelea kura za uraisi wa 2010, ni vizuri pia ukawa na majibu ni namna gani tume ya uchaguzi ilirekebisha tatizo la majumuisho ya kura za uraisi. Na kwa sababu gani hata kwenye website kuna sehemu nyingi tu ambazo kura zake hazijawa posted hadi leo. Unawezaje kusema kwa ujasiri kwamba CHADEMA ilishindwa katika mazingira tata naman hiyo? Ikiwa hata chief malenga ( nje ya record) amewahi kukiri kwamba 2010 hakushinda kwa wingi wa kura bali alishinda kwa mamlaka aliyopewa na katiba?
5. Ninaomba utafakari na uukubali ukweli ili ukweli ukuweke huru. Huwezi kubisha kwa kutumia outdated data wakti wenzako wanatumia za leo!. lAKINI ALL IN ALL CCM HAIPO TENA, HILI LIFAHAMU NA ULIKUBALI.
Cdm ni mabigwa wa uongo . uwe na wanachama ml 10 ukose kula ml 7 ili kutangazwa rais? Sasa maana ya kapeni nini?