Ni
mara ya kwanza kwa kiongozi wa kiafrika kupewa mapokezi makubwa ambayo
Dr. Slaa ameyapokea katika ufunguzi wa mchezo wa mpira maarufu kama
football. Dr. Slaa alialikwa na Chancellor pamoja na Rais wa chuo kikuu
cha Alabama kuwa mgeni rasmi katika mchezo huo baina ya Alabama na
Georgia State. Kiongozi huyo wa Chadema alipokewa na viongozi wa ngazi
mbali mbali wa kitaifa na wa jimbo la Alabama
Akimkaribisha Dr. Slaa katika chakula cha asubuhi iliyoandaliwa kwa
ajili yake, Chancellor wa chuo hicho, amemfananisha Dr. Slaa na Nelson
Mandela kutokana na juhudi zake za kupambana ufisadi nchini Tanzania.
Tunajua jinsi polisi wanavyowaua raia na kuwakamata wapinzani alisema
kiongozi huyo. Kadhalika kiongozi huyo amemsifu Dr. Slaa kutokana na
msimamo wake, sera zake za kulikomboa Tanzania kutoka katika umasikini
licha ya chama chake kutungiwa kesi za ughaidi.
Kwa upande wake, wakiwa kama moja ya vyuo vikuu nchini marekani, wako
tayari kufanya kazi kwa ukaribu na Dr. Slaa hasa katika sekta ya elimu.
Wamemuomba ajisikie nyumbani na kufurahia mchezo wa American football.
Kwa unyenyekevu Dr. Slaa aliwashukuru governor, na viongozi wengine kwa
kuwa wakarimu sana kwake na mkewe na watu wa Tanzania. Amefurahishwa
jinsi wamarekani wanavyokuwa na hamasa na kuipa kipaumbele michezo.
Nimejifunza kwamba michezo ni moja ya mbinu ya kuiunganisha taifa hasa
tunapokuwa na changamoto nyingi kama za kwetu alisema Dr. Slaa.
Kadhalika amesema kwamba, chama chake cha Chadema ina sera ya kukuza
vipaji kupitia taasisi za michezo nchini Tanzania na siyo kuwaleta
Makocha wa kigeni, mmoja baada ya mwingine na kuwapeleka Ikulu kula
pilau na kupiga picha.
Nilichojifunza ni kwamba, lazima nirudi na ujumbe kwa watanzania kuweka
mifumo endelevu ya michezo kuanzia shule za misingi hadi vyuoni.
Nilichoona hapa ni mfano wa kuigwa alimalizia Dr. Slaa
![]()
Dr.
Slaa na Mkewe wakilakiwa na Rais wa Chuo
![]()
Moja
wa mamea mashuhuri marekani akimsalimia Dr. Slaa
![]()
Dr.
Slaa akikaribishwa Ukumbuni kwenye Chakula cha Asubuhi iliyoandaliwa
kwa ajili yake
![]()
Moja
ya Viongozi wa Juu Nchini Marekani
![]()
Dr.
Slaa akibadilishana mawazo na baadhi ya viongozi ya Masenators
walioalikwa kujumuika naye
![]()
Watoto
nao walijitokeza kumsalimia na kupiga picha na mgeni mashuhuri Dr. Slaa
![]()
Watu
wengi mashuhuri walioalikwa walimiminika kusalimiana na Dr. Slaa
![]()
Dr.
Slaa na Senator Shelby wakibadilishana mawazo wakielekea uwanjani
![]()
Msafara
wa Dr. Slaa ukiwasili uwanjani
![]()
Watu
wa kila aina mashuhuri walifika kumsalimia Dr. Slaa
![]()
Dr.
Slaa na Gavana
![]()
Dr.
Slaa akisalimiwa na mmoja wa US congressmen waliohudhuria mchezo
![]()
Mshindi
wa Nobel Peace Price na Dr. Slaa ndani ya Chumba cha watu mashuhuri
wakijadili neno
![]()
Viongozi
Mashuhuri wakiwa uwanjani kabla ya mchezo kuanza. Dr. Slaa ndiye mgeni
Rasmi. Hapa ni chumba maalum cha rais kwa ajili ya wageni mashuhuri
![]()
Uwanja
ulijaa hasa. Watu zaidi ya laki moja walihudhuria
![]()
wakiwa
katika chumba cha watu mashuhuri. Baadhi ya watu mahuhuri kama yeye
hawakujizuia kwenda kumsalimia. Akifungua mchezo wa leo, Dr. Slaa
alirushwa moja kwa moja na moja ya luninga kubwa zaidi nchini
marekani
Napenda chadema,Slaa asiposimamishwa urais basi wamsimamishe Tundu Lissu.
Amen
Ni mara ya kwanza kwa kiongozi wa kiafrika kupewa mapokezi makubwa ambayo Dr. Slaa ameyapokea katika ufunguzi wa mchezo wa mpira maarufu kama football. Dr. Slaa alialikwa na Chancellor pamoja na Rais wa chuo kikuu cha Alabama kuwa mgeni rasmi katika mchezo huo baina ya Alabama na Georgia State. Kiongozi huyo wa Chadema alipokewa na viongozi wa ngazi mbali mbali wa kitaifa na wa jimbo la Alabama
Akimkaribisha Dr. Slaa katika chakula cha asubuhi iliyoandaliwa kwa ajili yake, Chancellor wa chuo hicho, amemfananisha Dr. Slaa na Nelson Mandela kutokana na juhudi zake za kupambana ufisadi nchini Tanzania.
Tunajua jinsi polisi wanavyowaua raia na kuwakamata wapinzani alisema kiongozi huyo. Kadhalika kiongozi huyo amemsifu Dr. Slaa kutokana na msimamo wake, sera zake za kulikomboa Tanzania kutoka katika umasikini licha ya chama chake kutungiwa kesi za ughaidi.
Kwa upande wake, wakiwa kama moja ya vyuo vikuu nchini marekani, wako tayari kufanya kazi kwa ukaribu na Dr. Slaa hasa katika sekta ya elimu. Wamemuomba ajisikie nyumbani na kufurahia mchezo wa American football.
Kwa unyenyekevu Dr. Slaa aliwashukuru governor, na viongozi wengine kwa kuwa wakarimu sana kwake na mkewe na watu wa Tanzania. Amefurahishwa jinsi wamarekani wanavyokuwa na hamasa na kuipa kipaumbele michezo.
Nimejifunza kwamba michezo ni moja ya mbinu ya kuiunganisha taifa hasa tunapokuwa na changamoto nyingi kama za kwetu alisema Dr. Slaa. Kadhalika amesema kwamba, chama chake cha Chadema ina sera ya kukuza vipaji kupitia taasisi za michezo nchini Tanzania na siyo kuwaleta Makocha wa kigeni, mmoja baada ya mwingine na kuwapeleka Ikulu kula pilau na kupiga picha.
Nilichojifunza ni kwamba, lazima nirudi na ujumbe kwa watanzania kuweka mifumo endelevu ya michezo kuanzia shule za misingi hadi vyuoni. Nilichoona hapa ni mfano wa kuigwa alimalizia Dr. Slaa
![]()
Dr. Slaa na Mkewe wakilakiwa na Rais wa Chuo
![]()
Moja wa mamea mashuhuri marekani akimsalimia Dr. Slaa
![]()
Dr. Slaa akikaribishwa Ukumbuni kwenye Chakula cha Asubuhi iliyoandaliwa kwa ajili yake
![]()
Moja ya Viongozi wa Juu Nchini Marekani
![]()
Dr. Slaa akibadilishana mawazo na baadhi ya viongozi ya Masenators walioalikwa kujumuika naye
![]()
Watoto nao walijitokeza kumsalimia na kupiga picha na mgeni mashuhuri Dr. Slaa
![]()
Watu wengi mashuhuri walioalikwa walimiminika kusalimiana na Dr. Slaa
![]()
Dr. Slaa na Senator Shelby wakibadilishana mawazo wakielekea uwanjani
![]()
Msafara wa Dr. Slaa ukiwasili uwanjani
![]()
Watu wa kila aina mashuhuri walifika kumsalimia Dr. Slaa
![]()
Dr. Slaa na Gavana
![]()
Dr. Slaa akisalimiwa na mmoja wa US congressmen waliohudhuria mchezo
![]()
Mshindi wa Nobel Peace Price na Dr. Slaa ndani ya Chumba cha watu mashuhuri wakijadili neno
![]()
Viongozi Mashuhuri wakiwa uwanjani kabla ya mchezo kuanza. Dr. Slaa ndiye mgeni Rasmi. Hapa ni chumba maalum cha rais kwa ajili ya wageni mashuhuri
![]()
Uwanja ulijaa hasa. Watu zaidi ya laki moja walihudhuria
![]()
wakiwa katika chumba cha watu mashuhuri. Baadhi ya watu mahuhuri kama yeye hawakujizuia kwenda kumsalimia. Akifungua mchezo wa leo, Dr. Slaa alirushwa moja kwa moja na moja ya luninga kubwa zaidi nchini marekani