Dr. Slaa afanyiwa hujuma Kalenga

Dr. Slaa afanyiwa hujuma Kalenga

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,361
Huku Chadema ikiteka kampeni za uchaguzi mdogo jimbo la Kalenga tayari hujuma zimeanza kuonekana mapema leo

Watu wasiojulikana wametega misumari barabarani katika njia ya kuelekea eneo la Mwasa muda mfupi kabla msafara wa Dr Slaa na mgombea ubunge kupita eneo hilo.

Hata hivyo Dr Slaa amechelewa kumaliza mkutano eneo la kwanza hivyo kuchelewa kupita muda ambao wategaji wameweka mtego wao.

Kutokana na sababu hiyo gari nyingine iliyopita njia hiyo imeharibika kabisa matairi yake baada ya kukanyaga misumari hiyo iliyotegeshwa barabarani.

Source Tumaini Makene Afisa Habari Mkuu Chadema.
 
Last edited by a moderator:
si mnatumia chopa,chopa na misumar wap na wapi.slaa ana phd ya uongo na kutengeneza siasa za matukio
 
Mbinu za kitoto kabisa kama zile za kuweka kura kwenye mahopot ya vyakula!!!
 
Unajua Tumain ccm wamekosa mwelekeo ndio maana wanafanya upuuzi kama huu.walaaniwe waliofanya kitendo hicho
 
propaganda za kipumbavu kabisa hivi. yaani nimeona propaganda nyngi za chadema ila hii imetia fora. Kwani barabara hiyo linapita gari la DR SLAA pekee? au katika ina maana kwa chadema gari la DR SLAA ndo linakuwa lakwanza? kama ndo hivyo, basi DR SLAA hatendewi haki.
 
propaganda za kipumbavu kabisa hivi. yaani nimeona propaganda nyngi za chadema ila hii imetia fora. Kwani barabara hiyo linapita gari la DR SLAA pekee? au katika ina maana kwa chadema gari la DR SLAA ndo linakuwa lakwanza? kama ndo hivyo, basi DR SLAA hatendewi haki.

mkuu. dr.slaa anafanya siasa za kitoto sana. amezoea kudanganya misukule yake basi anaona watu wote ni wakudanganya tu, huyu mzee apimwe akili
 
hao watakuwa ni chadema wenyewe wametega hiyo misumari kutafuta huruma ya wana kalenga, dr.slaa anafanya siasa za kitoto sana, akadanganye misukule yake.

Hakika Mkuu. Kama waliweza kujilipua wenyewe pale SOWETO, ARUSHA, iweje hilo la misumari? kama walijaribu kumuua zitto kwa sumu, watashindwaje kwa hilo? kama wameweza kumuua CHACHA WANGWE, watashindwaje kwa hilo? yapo matukio mengi ambayo chadema inahusika lakini inaruka vihunzi. Dr SLAA na vibaraka wake akina Makene wameona kuwa wameshindwa na sasa wanataka kutafuta sababu za kushindwa kwao
 
Back
Top Bottom