mzenjiboy
JF-Expert Member
- Aug 28, 2010
- 907
- 383
Watanganyika naona wamepagawa kwa kauli za Dr. Shein, eti si kauli yake au si maneno yake. Gazeti gani linaweza kuchapisha habari za uwongo za kumsingizia kiongozi wa nchi, hebu jiiulizeni hapo tu. Na kama kiongozi huyo anazuliwa uwongo ni hatua gani huchukuliwa kisheria dhidi ya gazeti husika. Shein na Wazanzibari kwa jumla wamechoshwa na huu muungano wenu hebu tuacheni ili TUPUMUE. Sijui ni lipi hasa munalolitaka kwetu wakati Mungu kakupeni nchi kubwa yenye kila aina ya utajiri lakini bado na kinchi chetu kidogo pia munaking'ang'nia.