Dr Shein amtimua kazi Waziri Himid!

Mwana Mpotevu

Platinum Member
Sep 7, 2011
3,295
2,500
Taarifa nilizozipata hivi punde ni kwamba waziri Mansoor Himid (CCM) ambaye alikuwa waziri asiyekuwa na wizara maalum, ametimuliwa uwaziri na Rais wa Zanzibar Dr Shein.

Kisa cha kutimuliwa ni kutokana na msimamo wake wa kutaka muuungano wa mkataba jambo ambalo ni kinyume na sera za CCM za serikali mbili.

Nitawapeni taarifa zaidi

Updates:

Ni kweli.

Shein afanya mabadiliko katika Baraza la Mapinduzi

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dkt Ali Mohammed Shein amefanya mabadiliko katika Baraza la Mapinduzi. Taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi, Dkt Abdulhamid Yahya Mzee imesema katika mabadiliko hayo, Rais Dkt Shein amemteua Shawana Bukheti Hassan kuwa mjumbe wa Baraza la Mapinduzi.

Rais Dkt Shein amefuta uteuzi wa mjumbe wa Baraza la Mapinduzi, Mansoor Yussuf Himid.

Katika uteuzi mwengine Dkt Shein amewateua Mtumwa Kheir Mbarak kuwa Naibu Waziri wa Kilimo na Maliasili na Mohammed Said Mohamed kuwa Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi. Katika hatua nyengine, Rais Dkt Shein amefanya mabadiliko ya baadhi ya Makatibu Wakuu katika Wizara za Miundombinu na Mawasiliano, Wizara ya Ardhi,Makaazi,Maji na Nishati.

Dkt. Juma Malik Akili ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano akichukua nafasi ya Dkt. Vuai Idd Lila atapangiwa kazi nyengine. Ali Khalil Mirza ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Ardhi,Makaazi,Maji na Nishati.
Kabla ya uteuzi huo, Mirza alikuwa Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Utalii Zanzibar,aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo,Mwalimu Ali Mwalimu atapangiwa kazi nyengine.

Taarifa ya Ikulu imesema pia Rais Dkt Shein amemteua Tahir M. Abdulla kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano,aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Msanif Haji Mussa atapangiwa kazi nyengine.
Uteuzi mwengine ni Mustafa Aboud Jumbe ameteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi,Makaazi,Maji na Nishati. Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo alikuwa Tahir M Abdulla ambaye amehamishiwa Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano.

Rais Dkt Shein ameteua CDR Julius Nalim Maziku kuwa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ambaye anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Kapteni Juma Abdulla Juma ambaye ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bandari Zanzibar hivi karibuni.

Uteuzi mwengine ni Juma Ameir Hafidh ameteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais(Fedha,Uchumi na Mipango ya Maendeleo) ambaye amechukuwa nafasi iliyoachwa wazi na Abdi Khamis Faki aliyeteuliwa kuwa Kamishna wa Bodi ya Mapato Zanzibar.

Aidha, aliyepata kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Zanzibar, Saleh Ramadhan Ferouz ameteuliwa kuwa Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Utalii Zanzibar ambaye anachukuwa nafasi iliyoachwa wazi na Ali Khalil Mirza aliyeteuliwa kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Makaazi,Maji na Nishati.

Pia Rais Dk Shein amemteua Mussa Haji Ali kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu uchumi Zanzibar. Uteuzi huo wote unaanza Oktoba 15 mwaka 2012.

Thanks EMT for this


 
Last edited by a moderator:
Kama wazenj wamechoka na neema toka bara si muwaache wende zao? Nadhani Shein analijua hili. Hataki hawa wanaopiga kelele baadaye wamsumbue wakilia lia baada ya kupata kitu tofauti na walivyodanganywa baada ya muungano kuvunjika. Watu wengine hata hawafikirii vizuri. Hivi zenj bado haioni inavyobebwa kwa kipande cha ardhi kisicholingana na hata wilaya ya kibaha kupewa hadhi ya nchi?
 
Ataingia uamsho kwa nguvu zaidi huku akijipalia makaa..kazi ipo vuguvugu si dogo ati Shein ajipange sana kwa mapambano maana adui yake hawezi kumjua kwa sasa wako wengi chini kwa chini
 
Taarifa nilizozipata hivi punde ni kwamba waziri Mansoor Himid (CCM) ambaye alikuwa waziri asiyekuwa na wizara maalum, ametimuliwa uwaziri na Rais wa Zanzibar Dr Shein.

Kisa cha kutimuliwa ni kutokana na msimamo wake wa kutaka muuungano wa mkataba jambo ambalo ni kinyume na sera za CCM za serikali mbili.

Nitawapeni taarifa zaidi

Hata hivyo hakuwa na wizara maalumu so he was just a political prostitute!
 
Kama wazenj wamechoka na neema toka bara si muwaache wende zao? Nadhani Shein analijua hili. Hataki hawa wanaopiga kelele baadaye wamsumbue wakilia lia baada ya kupata kitu tofauti na walivyodanganywa baada ya muungano kuvunjika. Watu wengine hata hawafikirii vizuri. Hivi zenj bado haioni inavyobebwa kwa kipande cha ardhi kisicholingana na hata wilaya ya kibaha kupewa hadhi ya nchi?

Na huyu waziri ni ndugu wa damu na Shadya Karume
 
Kama wazenj wamechoka na neema toka bara si muwaache wende zao? Nadhani Shein analijua hili. Hataki hawa wanaopiga kelele baadaye wamsumbue wakilia lia baada ya kupata kitu tofauti na walivyodanganywa baada ya muungano kuvunjika. Watu wengine hata hawafikirii vizuri. Hivi zenj bado haioni inavyobebwa kwa kipande cha ardhi kisicholingana na hata wilaya ya kibaha kupewa hadhi ya nchi?

Kupewa hazi ya nchi na nani?

Sent from my GT-I9300 using Tapatalk
 
Ataingia uamsho kwa nguvu zaidi huku akijipalia makaa..kazi ipo vuguvugu si dogo ati Shein ajipange sana kwa mapambano maana adui yake hawezi kumjua kwa sasa wako wengi chini kwa chini

Jussa naye ni mpiga debe mkuu wa hili, dawa yake huenda inachemmka maana la CCM ndio la CUF
 
Naona hapo ndiyo wameshawasha moto, itabidi watimuliwe wengi kama ndiyo hivyo sasa.
 
Wakati huo huo.....


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete anaanza ziara rasmi ya Kiserikali ya siku nne katika Taifa la Kifalme la Oman, ikiwa ni ziara ya kwanza ya Kiserikali kufanywa na Rais wa Tanzania katika nchi hiyo.

Rais Kikwete na ujumbe wake ameondoka mjini Dar es Salaam asubuhi ya leo, Jumatatu, Oktoba 15, 2012, kwenda Oman kuanza ziara hiyo inayofanyika kwa mwaliko wa Kiongozi wa Ufalme wa Oman, Mfalme Qaboos bin Said, ambaye atakuwa mwenyeji wake kwa siku zote nne.

Kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Muscat, Rais Kikwete anatarajiwa kulakiwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman, Mheshimiwa Yousef bin Abdullah bin Alawi ambaye ataandamana naye hadi Jumba la Muscat Gate ambako Rais atapokelewa na Mfalme Qaboos. Kutoka hapo wataandamana hadi Kasri ya Kifalme ya Al Alam ambako atapokelewa rasmi kwa heshima zote za Kiserikali.

Shughuli kubwa ya jioni ya leo ya Mheshimiwa Rais itakuwa ni kufanya mazungumzo rasmi ya Kiserikali kati ya Serikali za Tanzania na Ufalme wa Oman na pia kuhudhuria dhifa rasmi ambayo Mfalme Qaboos atamwandalia mgeni wake kwenye Kasri ya Al Alam.

Kesho, Jumanne, Oktoba 16, 2012, Rais Kikwete atatembelea Jumba la Makumbusho la Majeshi ya Ulinzi ya Oman, atafungua Mkutano wa Wafanyabiashara wa Tanzania na Oman, atashuhudia utiaji saini makubaliano ya mikataba miwili kati ya nchi hizo mbili, ukiwamo ule wa kuundwa kwa Baraza la Biashara la Tanzania na Oman na ule wa Kuendeleza na Kulinda Uwekezaji katika nchi hizo mbili.

Jioni, Rais Kikwete atatunukiwa nishani ya juu kabisa ambayo Ufalme wa Oman hutoa kwa viongozi wa nchi za nje ya First Order Medal kwenye Chakula Maalum cha Usiku kitakachoandaliwa na Mfalme Qaboos kwa heshima ya Rais Kikwete.
 
Wakati huo huo.....


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete anaanza ziara rasmi ya Kiserikali ya siku nne katika Taifa la Kifalme la Oman, ikiwa ni ziara ya kwanza ya Kiserikali kufanywa na Rais wa Tanzania katika nchi hiyo.

Rais Kikwete na ujumbe wake ameondoka mjini Dar es Salaam asubuhi ya leo, Jumatatu, Oktoba 15, 2012, kwenda Oman kuanza ziara hiyo inayofanyika kwa mwaliko wa Kiongozi wa Ufalme wa Oman, Mfalme Qaboos bin Said, ambaye atakuwa mwenyeji wake kwa siku zote nne.

Kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Muscat, Rais Kikwete anatarajiwa kulakiwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman, Mheshimiwa Yousef bin Abdullah bin Alawi ambaye ataandamana naye hadi Jumba la Muscat Gate ambako Rais atapokelewa na Mfalme Qaboos. Kutoka hapo wataandamana hadi Kasri ya Kifalme ya Al Alam ambako atapokelewa rasmi kwa heshima zote za Kiserikali.

Shughuli kubwa ya jioni ya leo ya Mheshimiwa Rais itakuwa ni kufanya mazungumzo rasmi ya Kiserikali kati ya Serikali za Tanzania na Ufalme wa Oman na pia kuhudhuria dhifa rasmi ambayo Mfalme Qaboos atamwandalia mgeni wake kwenye Kasri ya Al Alam.

Kesho, Jumanne, Oktoba 16, 2012, Rais Kikwete atatembelea Jumba la Makumbusho la Majeshi ya Ulinzi ya Oman, atafungua Mkutano wa Wafanyabiashara wa Tanzania na Oman, atashuhudia utiaji saini makubaliano ya mikataba miwili kati ya nchi hizo mbili, ukiwamo ule wa kuundwa kwa Baraza la Biashara la Tanzania na Oman na ule wa Kuendeleza na Kulinda Uwekezaji katika nchi hizo mbili.

Jioni, Rais Kikwete atatunukiwa nishani ya juu kabisa ambayo Ufalme wa Oman hutoa kwa viongozi wa nchi za nje ya First Order Medal kwenye Chakula Maalum cha Usiku kitakachoandaliwa na Mfalme Qaboos kwa heshima ya Rais Kikwete.

Rekebisha kwenye red: Mwl Nyerere, mwaka 1985 na miezi michache kabla ya kuondoka madarakani alifanya ziara ya kiserikali nchini Oman.
 
Wakati huo huo.....


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete anaanza ziara rasmi ya Kiserikali ya siku nne katika Taifa la Kifalme la Oman, ikiwa ni ziara ya kwanza ya Kiserikali kufanywa na Rais wa Tanzania katika nchi hiyo.

Rais Kikwete na ujumbe wake ameondoka mjini Dar es Salaam asubuhi ya leo, Jumatatu, Oktoba 15, 2012, kwenda Oman kuanza ziara hiyo inayofanyika kwa mwaliko wa Kiongozi wa Ufalme wa Oman, Mfalme Qaboos bin Said, ambaye atakuwa mwenyeji wake kwa siku zote nne.

Kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Muscat, Rais Kikwete anatarajiwa kulakiwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman, Mheshimiwa Yousef bin Abdullah bin Alawi ambaye ataandamana naye hadi Jumba la Muscat Gate ambako Rais atapokelewa na Mfalme Qaboos. Kutoka hapo wataandamana hadi Kasri ya Kifalme ya Al Alam ambako atapokelewa rasmi kwa heshima zote za Kiserikali.

Shughuli kubwa ya jioni ya leo ya Mheshimiwa Rais itakuwa ni kufanya mazungumzo rasmi ya Kiserikali kati ya Serikali za Tanzania na Ufalme wa Oman na pia kuhudhuria dhifa rasmi ambayo Mfalme Qaboos atamwandalia mgeni wake kwenye Kasri ya Al Alam.

Kesho, Jumanne, Oktoba 16, 2012, Rais Kikwete atatembelea Jumba la Makumbusho la Majeshi ya Ulinzi ya Oman, atafungua Mkutano wa Wafanyabiashara wa Tanzania na Oman, atashuhudia utiaji saini makubaliano ya mikataba miwili kati ya nchi hizo mbili, ukiwamo ule wa kuundwa kwa Baraza la Biashara la Tanzania na Oman na ule wa Kuendeleza na Kulinda Uwekezaji katika nchi hizo mbili.

Jioni, Rais Kikwete atatunukiwa nishani ya juu kabisa ambayo Ufalme wa Oman hutoa kwa viongozi wa nchi za nje ya First Order Medal kwenye Chakula Maalum cha Usiku kitakachoandaliwa na Mfalme Qaboos kwa heshima ya Rais Kikwete.

naona tumekluwa na rais wa kuhudhuria dhifa za kitaifa ugenini kila wiki as if nyumbani ugali hakuna, simtofautishi na mtoto mdogo anayekataa kurudi kwao ili mradi kaona kwa jirani kuna chakula kitamu anachokipenda kimepikwa, hivyo hulazimika kusubiri hadi wapakue
 
I hope it is true kwani mkala yangu ya mwishi ilimtaja Shein kuwa Anawaendekeza. Wakitaka muungano wa mkataba watoker ccm na cuf kwanza halafu waanze harakati za kudai uhuru. Lazima afuatie mwanasheria mkuu wa Zanzibar naye.

Mwanasheria mkuu wa Zanzibar ndiye alistahili kuangaliwa kwanza halafu ndiyo wengine wafuate. Huyo amekuwa anawapotosha watu na kwasababu ya cheo chake (mwanasheria mkuu) watu wanadhani anajua anachoongea. Ni yeye alikuja na hoja za muungano wa mkataba kama wa Swiss! Swiss?!
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom