mmoja tunajua dhahiri kakimbia kwa ugonjwa ila mwengne kakimbia kwa kuogopa maswali na hoja za serikal anayoitetea.
Ni lini ccm inatimizaga ahadi? walisema kampeni zao watatumia barabara tu matokeo yake utadhani wana kiwanda cha chopa.CCM ni waongo sana si bora wangekataa tangu awali kama CHADEMA...
Mgombea Urais wa CCM Dr.John Pombe Magufuli, ameshindwa kuhudhulia katika Mdahalo wa Marais wanaogombea Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambao Unaendelea Hivi sasa.
Hapo mwanzo alitoa taarifa kwamba atashiriki, lakini dakika 45 kabla ya kuanza mdahalo, ametoa taarifa kwa waandaaji kwamba hatahudhulia, hali ambayo imepokelewa kwa hisia tofauti.
Hadi sasa Wagombea urais waliohudhulia ni wawili tu ambao ni Mgombea wa ADC Chief Lutasola Yemba, Mgombea wa ACT Wazalendo Mama Anna Mghwira huku akisubiriwa mgombea wa CHAUMA Hashim Rungwe ambaye amesema yupo airport anakuja kwenye mdahalo.
Hii sio picha nzuri kwa wagombea wetu. Ni aibu Mdahalo wa Marais kukudhuliwa na Marais wawili tu kati ya Marais wanane.
Mdahalo uliokuwa umeandaliwa Twaweza Maghufuri amekacha sababu ameshidwa kuzieleza.
Viva Lowasa uliona mbali sana huu mdahalo ulikuwa umendaliwa kumpigia Campaign Maghufurika.
Cha ajabu huyu Maria ameeleza sababu za kutoudhuria kwa Lowasa akionyesha kumponda Lowasa lakini kwa Maghufuri akawa mpole,CCM mmechamka pesa zimeliwa na hakuna lilofanikiwa.
Hii Inaonyesha, kufuli anacheza ngoma ya CHADEMA,safi sana,sasa mlitaka akadahale na nani?kama babu aligoma?Namsifu sana Magufuli kwa kweli
CCM ni waongo sana si bora wangekataa tangu awali kama CHADEMA...
Kwa mkwara Mzito mnaotoaga UKAWA kwamba lazima muende ikulu ilitakiwa leo mgombea wenu awepo hapo jukwaani! lakini ndo wa kwanza kukimbia!
halafu unawahi kupiga madongo CCM, Kweli nyani haoni...............................
nchi za africa midahalo bado hawajui kuiandaa ina kaushabiki fulani na ndio maana haina uzito.ingefaa vyama ambavyo havina ilani ya uchaguzi kama chadema wangefika kwenye mdahalo