Ajali hiyo ilitokea jana ambapo gari ilipoteza uelekeo kutokana na hitilafu ya barabara na hivyo kuvutwa, kugonga gema na kupinduka mara moja na gari kukaa matairi juu.
Kuna upotevu mkubwa wa maisha ya watu na mali zao unaotokea kila siku kutokana na ubovu wa barabara. Ukichukulia kwamba kila tunaponunua petroli au dizeli tunalipia utengenezaji wa barabara (road toll), niliwahi kupendekeza kwamba Waziri wa Ujenzi (Magufuri) na serikali kwa ujumla washitakiwe kila inapotokea ajali au uhalibifu wa gari kutokana na hitilafu ya barabara, kama vile shimo kubwa la ghafla ambapo hakuna hata alama ya tahadhari. Mara nyingi sana nimeponea chupuchupu kutokana na mashimo ya ghafla barabarani.