Mwaka 2010 nikiwa natokea south africa kikazi nafanikiwa kukaa karibu na kiti cha mwanasiasa mahili wa upinzani wa tanzania dk slaa, nafanikiwa kumsalimia dk slaa kwa bashasha kwa sababu ni moja ya wanasiasa ninao waheshimu zaidi. baada ya salamu tulizungumza nae maneno mawili matatu na hasa upande wa siasa na uchumi, mara nyingi dk alitaka kujua mimi ni mfuasi wa chama gani,haraka nilimjibu mimi ni muumini wa siasa za mabadiliko ya kweli na yasiyo tetereka ,nilimuelezea kwa kirefu maana ya maneno uumini wangu huo japo tulibishana hapa na pale mpaka tulipofika dar es salaam.
tulipo fika dar es salaa uwanja wa ndege yeye alitokea geti la watu mashuhuli na mimi nikatokea geti la kawaida,nikachukua gari (taxi)nakuanza safari,kabla hata sijafika nje ya barabara kuu gari nililokuwamo linapata hitilafu niliamua kutafuta gari nyingine ili niendelee nasaafari yangu ya kuelekea nyumbani ,niliporudi nyuma ya gari ili nichukue mizigo yangu mara naona gari aina ya land cruiser vx ya kijani inasimama pembeni yangu na kiookushushwa,na mara naona sura ya dk slaa ,mara moja ananiuliza tatizo na mimi bila kusita nikamuelezea ,papo hapo akanitaka niingie kwenye gari alilo kuwemo,nami bila kusita nili tii ,alinitaka nikae kiti cha mbele maana nyuma alikua amekaa na mtu ambae mara ya kwanza sikumfahamu vizuri ila nilipo ingia ndani ya gari nikafanikiwa kumjua ,alikua dk harrison mwakyembe,haraka nilimsalimia na kwa mara ya kwanza katika maisha yangu nafanikiwa kukutana na mtu ambae naweza kusema kwangu nina mchukulia kama mtu mwenye uwezo mkubwa zaidi katika kukisimamia kile anacho amini. kwa mara ya kwanza nimekua nikimfuatilia mwakyembe mara baada ya sakata la richmond,mimi binafsi ni mwanasheria na naweza sema nimesoma kati ya moja ya vyuo vizuri duniani , nadiriki kusema ripoti iliyo andikwa na kamati ya dk mwakyembe ni moja ya ripoti bora zaidi duniani, naomba nieleweke nazungumzia kisheria yaani kwa namna ripoti ilivyo andikwa iliandikwa kitaalam zaidi kiasi ya kwamba situ inaweza kukufanya ujiuzulu au ukafungwa kabisa lakini inaweza pia kutumika katika kufundishia kwa namna ilivyo andikwa kitaalam. ripoti inayo kubana katika nyuzi 360 bila kuacha mwanya wa aina yoyote ya mshukiwa kutoka. Baada wa ripoti ile wote tunajua kilicho mtokea dk mwakyembe , alitaka kuuwawa kwa sababu tu ya kusema ukweli,lakini wauwaji walisahau neno moja , bibilia takatifu inasema hvi mwenye haki wangu ataishi kwa imani.
mwakyembe aliishi kwa imani na alikisimamia kile alichokiamini ni ukweli mpaka leo hii.watu waliotaka kumuua dk mwakyembe ni watu wenye maono makubwa sana kwenye siasa hawakuwa watu wa kubabaisha hawakuwa majambazi hawakua vibaka walikua ni watu waliokua na malengo ya kisiasa ya muda mrefu, kundi la wauwaji hawa lilijumuisha wasomi wachambuzi wa mambo ya siasa wafanya biashara wakubwa na bila kusahau wanasiasa wakubwa,lakini swali la kujiuliza ni kwann dk mwakyembe pekee ndiye aliye taka kuuwawa na sio wenzake walioshirikiana kuandika ripoti, maana ripoti ile haikuandikwa na dk mwakyembe mwenyewe,ntarudia kusema tena watu waliotaka kutekeleza mpango ulioshindikana wa kumuua dr mwakyembe walikua watu wenye ufahamu mkubwa sana na walijua vizuri uwezo wa dk mwakyembe. dk mwakyembe alikua ndiye mtu pekee ambaye angeweza kuzuia mpango wao wa muda mrefu wakushika madaraka na kukomba rasilimali,walijua ripoti ya richmond ingeweza kuwa mwiba mchungu kwao,walijua jinsi dk mwakyembe anaweza kujenga hoja walijua na walishalishuhudia hilo haraka wakaona hamna namna ni kumuua kwa namna yoyote ile iwe kwa bunduki na kusingizia majambazi au sumu ,vikao vilikaa usiku na mchana kutafuta namna ya kutekeleza azma yao,baada ya majadiliano ya siri kubwa na kubumbuluka kwa mipango ya awali wakakubaliano kutumika kwa sumu ,watu hawa ni matajiri walitafuta sumu umbali wa maelfu yakilometa kutoka walipo, walifanikiwa kuipata na pia walifanikiwa kumuwekea dokta mwakyembe ,lakini MUNGU ni mkubwa sumu waliyo mwekea dk mwakyembe mwili uliitema kwenye ngozi yaani maini yake hayakuruhusu damu iliyo changanyika na sumu kupita na badalayake kwa uwezo wa kiuumbaji u