Dr. Kigwangwala alitakiwa awe waziri Kamili

Dr. Kigwangwala alitakiwa awe waziri Kamili

Nimevutiwa na alivyowauliza amana kwa nini wanafunga chumba cha ultrasound...na ku refer wagonjwa Muhimbili unnecessarily

Wewe ni reflection ya watanzania vilaza na wavivu kufikiri.

Unavutiwa kwa vitu ambavyo vipo very obvious hata mtoto wa nursery anaweza kufikiri.
 
Yes hiki ndicho kilicho serikalini. Vitanda havipo hospitalini eti Manesi wamevihamishia kwao. Tunagombanisha Watumishi na Wananchi then Wanasiasa wanapeta. Hii siyo haki. Tusitumie uelewa mdogo wa Wananchi kusukuma mzigo kwa watumishi wa umma.

Asante.
 
Mara zote tunasema vijana na watanzania hamtaki kusumbua akili zenu kufanya utafiti wa kina wa issue na masuala mbalimbali ambayo ni mhimu sana kwa ajili ya uelewa wa mambo, mtu ameandika hapa kwa mawazo yake Kigwangala anafaa kuwa full Minister kama unaona hafai binashana na hoja kwamba huyu hafai kwasababu hii na hii sio kuanza kumshambulia...hii sehemu JF imevamiwa sana sana watu wengi humu wamesababisha pameonekana kama FB wakati sio..

Assnte Somoche.
Wise words!
 
Mtu kuvamia Hosp ndiyo kuwa na uwezo mkubwa??

Hayo sasa ni mawazo yako, je Lowasa alivyopanda daladala si watu wote walifurahia, Muhimbilia John alivyotembelea? Bandarini?
Matembezi yao ni kama catalyst fulani hivi ya kuwaamsha watu.
 
kama sikosei Dr hamis kingwangala ndiye aliyekua kiongozi wa mgomo wa madaktari pale muhimbili mwaka ya 2000s ambapo sumaye alienda wakamzomea kwa kupiga makofi

Ndio maana nakuambia kuwa hiyu jamaa katoka mbali kwenye hii sekta, kama aligoma sio sababu ya yeye kuwa disqualified bali imemuongezea cv. Sasa yale waliyokuwa wanayagomea bado hayajaisha huyu ndio suluhisho la matatizo yote.
Kigwa anajua siri zote za Muhimbili. Anajua wezi wote anajua mashine zote za muhimbili anajua wanaoziharibu.
Go brother kigwa japo sikujui binafsi.
 
Huko Amana alienda na Vitanda? dawa za bure kwa ajili ya wazee? majengo ya kulazwa wagonjwa? Kama kazi zao ni kukagua daftari la mahudhurio sioni kipya? Hayo matatizo yanafahamika, wasituletee siasa bali wayatatue. Watawahadaa watanzania, halafu watanzania hao wanakuja kutupigia kelele sisi wataalamu.

Mgonjwa anakuja, unasoma prescription, unamwambia dawa hii hatuna. Utamsikia mzee wa watu analalamika, "tumeambiw dawa zipo, mnatuibia nk..." Inachofanya serikali ni kutuchonganisha watumishi na watanzania. Tatueni kero, acheni siasa. Sasa, nitoe hela yangu nimnunulie mgonjwa dawa? Nitasaidia wangapi?

Wazee wanakumbwa na magonjwa ambayo dawa zake ni ghali; Magonjwa ya moyo & homoni ... Na serikali inapaswa kuwapatia dawa hizi, ndo vitu anavyopaswa kuvisimamia waziri sio kukagua attendance sheets. Zinamsaidia nini mtanzania? Siku akipita ofisini kwangu nitamweleza hayo, sipendi unafiki. Otherwise, mkitaka wazee wenu waishi vizuri wakatieni BIMA, vinginevyo utaingia gharama kubwa sana.
Dr heshima kwako kigwa sio lazima hadi apite ofisini kwako . Hata ulivyoandika tu hapa ujumbe umewafikia.
 
Kama humfahamu si UTULIE TU uulizie kwanza habari zake? Ona "walivyokushukia"..
.
Ati ?? Hakika wewe ni mgeni hapa JF.
Tafuta thread nyingi utaona maana ya thread.
Hapa unaleta hoja na watu wanakupinga kwa hoja
Sister do your research about JF, hapa sio JF mnapochambana. Nimeleta hii hoja ili nipete upinzani. Soma post zote uta gain vitu vingi sana
Viva JF
saint ivuga
 
Naungana 100% na mleta mada, uzuri kigwa anauliza kitaalamu na kushauri kama mwana taaluma haswa

alipaswa kufanya utafiti.Haya yalionekana muhimbili yapo ngazi zote. Ukawa wanayajua sana na wameyasema sana. Ccm kazi kubwa kukanusha
 
dr kigwangala sio mtu wa kuentertain nonsense kwenye kwenye kazi.tusubiri miezi 6 tu ifike kisha tumjadili tena hapa.nina uhakika wengi wenu mtabadili mtazamo wenu juu yake
 
Wewe ni reflection ya watanzania vilaza na wavivu kufikiri.

Unavutiwa kwa vitu ambavyo vipo very obvious hata mtoto wa nursery anaweza kufikiri.
Wewe unavutiwa na nini mfano??? Urembo????Acha roho ya wivu...haikusaidii utapata maradhi ya moyo
 
Mkuu, ugomvi wangu mimi na hawa mawaziri & watendaji ni vipaumbele. Kama uliangalia juzi baada ya kuapishwa wote walivamia maeneo yao, na kipaumbele kilikuwa ni kukagua ma counter books. Mkuu, Naweza kukaa pale na nisimuhudumie mtu katika ubora. Issue sio kushinda kazini siku nzima, bali ni kutatua changamoto zikiwemo za watumishi

Mahudhurio kwanza, huwezi itisha kikao cha wafanyakazi kueleza changamoto kama ni watoro. Akili zako unaziacha wapi?
 
Zile show mbili alizopull kwenye tv hazitoshi, viongozi wa sasa hivi show off nyingi tu ili kuleta mwamko lakini wakishasepa hali inarudi palepale, bado njia ndefu sana, inabidi watafute system tofauti ambayo itaweka effect hata wakiondoka ile effect iendelee kuwepo kwa muda mrefu.

Hizi show wanazotupa kuita waandishi wa habari wanazunguka nao kila kona mimi nazichukulia ka show tu and nothing more, matatizo makubwa sana na ya msingi bado yapo ambayo hayajawa addressed.
 
Wewe unavutiwa na nini mfano??? Urembo????Acha roho ya wivu...haikusaidii utapata maradhi ya moyo

Sivutiwi na urembo.

Kiongozi mahiri najua kupanga safu yake na wakafanya kazi bila makelele na output ikaonekana.

Mawaziri wa Magufuli wanachota akili za vilaza kama wewe.
 
Back
Top Bottom