Masanilo
Platinum Member
- Oct 2, 2007
- 22,286
- 4,493
Bila ajizi mzee John Malecela amekuwa nguzo muhimu sana kwenye ustawi na kukifika CCM mahali ilipo leo. Ni Kada wa chama hiki kikongwe Afrika ambaye amekuwa akikisimamia kila anachokiamini. Nakumbuka ushauri wake kwa sisiem kuwa ifike wakati chama kichukue maamuzi magumu zidi ya Chenge na hata Lowassa ili kurudisha imani kwa wananchi. Mzee alidharauliwa na ushauri wake haukufutwa. Amedhalilishwa sana Chimwaga kwenye vikao vya ndani lakini Mh Malecela anaonyesha ukomavu wa kisiasa. Ila kwa sasa naona amechukia na kutokipenda tena chama chake cha CCM ndiyo sababu haonekani kwenye sherehe ya miaka 35 hapo Mwanza. Mzee chukua maamuzi magumu CCM si wazazi wako,