Dr.Charles Kitima na wewe umenunuliwa?

Dr.Charles Kitima na wewe umenunuliwa?

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
52,154
Reaction score
162,570
Dr.Kitima ni miongoni mwa watu ambao mara kwa mara huwa anaalikwa Star tv katika vipindi mbalimbali na niseme ukweli tu huwa navutiwa sana na michango na kauli zake kwenye vipindi anavyoalikwa na kwakweli siku zote huwa anakuwa "outspoken".Mara nyingi anakuwa ni mtu wa kuikosoa serikali bila woga wala hofu,naamini wale ambao huwa mnamfuatilia katika luninga mtakubaliana nami.

Lakini ninachoshangaa ni kwanini mpaka leo yuko kimya juu ya sakata hili la Kikwete na Tundu Lissu kuhusu uteuzi wa mjumbe wa TEC kwenye tume ya katiba.Dr.Kitima ndie alietajwa na mh.Lissu kuwa aliiambia kamati ya bunge ya katiba,sheria na utawala kuwa mtu alieteuliwa na Raisi kuingia katika tume hiyo hakupendekezwa na TEC.

Sasa Dr. unashindwa nini kusema hadharani juu ya hili?

Hata hivyo,inawezekana hawezi kuongea bila idhini ya TEC kuhusu jambo hii.

Itakuwa ni jambo la ajabu Taasisi ya kidini kushindwa kusema ukweli au kuficha ukweli.

Watanzania tuachane na Jk na Lissu na badala yake tuzikabe koo hizi Taasisi.Haiingii akilini kuwajadili Tundu Lissu na Kikwete bila kuhoji ukimya wa hizi Taasisi.

Kitu kingine cha kujiuliza ni mbona hawakuhoji uteuzi wa wajumbe hao mara baada ya majina ya wajumbe wa katiba mpya kutangazwa??!!
 
Religion is an opium!!!!!!

They have never been,they are not,never will they be neutral
 
Wewe akili ya Lissu na Kitima unaona zipo sawa?hawa wote wapenda sifa na camera hwana kitu........
 
Nadhani unafahamu kwamba star tv inamilikiwa na kada wa ccm Anton Diallo sasa wakiona mtu kama dk Kitima wanaacha kumwalika kwa kuwa wanajua msimamo wake! Hujui star tv siku hizi ni star tvccm dam! Pia dk Kitima si mkuu wa saut tena... Ni mhadhiri wa kawaida...
 
Kamaliza kazi yake ya VC chuo kikuu SAUT Mwanza kapewa post mpya Morogoro.
 
Watanzania tuachane na Jk na Lissu na badala yake tuzikabe koo hizi Taasisi.Haiingii akilini kuwajadili Tundu Lissu na Kikwete bila kuhoji ukimya wa hizi Taasisi.

Unaweza kaba koo taasisi kubwa za kidini zenye hadhi kubwa kama TEC na CCT? Pigana vita kote usisigee hizo taasisi kama CHADEMA inataka ipigwe chini nzima nzima uchaguzi 2015 pamoja na huyo Tundu Lisu isogeze vita zake kwenye hizo taasisi.Hizo taasisi ni moto wa kuotea mbali hasa kwa wanasiasa uchwara.

Huyo Padre katima na huyo mwingine wa CCT ni watu wadogo sana CCT na TEC hata kama waliiiona list ya wajumbe walioteuliwa katika hatua za awali haikuwa ndio fainal viongozi wa juu ambao ni maaskofu walikuwa na uwezo wa kuweka majina mengine tofauti na hilo la DR.katima na mwenzie yaliyopendekezwa bila kuwajibika kurudisha feedback kwa huyo Dr.KATIMA kwa kuwa kwa mfumo wao hawajibiki kwa junior.

Sasa kama huko mbele kwa mbele hakuona jina lake mtu wa kumwuuliza sio Tundu Lisu na hiyo kamati au Raisi .Na Chadema WAJIFUNZE Kuwasiliana na wakubwa wa taasisi za kidini kama raisi anavyofanya wakiiga staili hii ya tundu lissu ya kuwasiliana na kuchukulia serious hoja ya mtu mdogo wameisha.Raisi alichosema ni sahihi anajua alikopata majina.

Pole Tundu lISSU ULIYEPATA majina kwa DR.katima.
 
Wewe akili ya Lissu na Kitima unaona zipo sawa?hawa wote wapenda sifa na camera hwana kitu........

Kwa mtu mwenye akili timamu hawezi kuandika kipuuzi kama ulivyoandika hapo! Hivi wewe unamfikia dk Kitima hata kwa punje? Je unamfikia Lissu hata kwa nukta? Acha ushabiki wa akili za juha... Ukweli utakuweka huru.. Acha kuwa -----...
 
Nadhani unafahamu kwamba star tv inamilikiwa na kada wa ccm Anton Diallo sasa wakiona mtu kama dk Kitima wanaacha kumwalika kwa kuwa wanajua msimamo wake! Hujui star tv siku hizi ni star tvccm dam! Pia dk Kitima si mkuu wa saut tena... Ni mhadhiri wa kawaida...

Mkuu hayo tote hayamzui kusema ukweli!

Media ziko nyingi tu.

Hofu yangu ni msimamo wa TEC juu ya swala hili.
 
Nadhani alichokisema Dk Kitima alikisema kama Mwakilishi wa TEC na sio kama mtu binafsi. Ninachojua mimi TEC wako very organized kwenye mambo ya kutoa taarifa. Walipoenda kwenye Kamati walienda Kitaasisi na walitoa malalamiko hayo kwa Taasisi (Kamati ya Bunge). Hawakupeleka malalamiko kwa Tundu Lissu as mtu binafsi. Kwangu mimi kwa kuwa Bunge liliarifiwa kuhusu kilichotokea wakati wa uteuzi nadhani TEC hawana cha kuongezea tena. Kazi yao walishaimaliza kwenye kamati na bila shaka maelezo yao walipeleka kwa maandishi kwa hiyo hiyo taarifa kwa sasa ni mali ya bunge kupitia Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala. Vinginevyo tuwalaumu hata CCT, TEC kwa ujumla na Walemavu kwa kupeleka taarifa hizo kwenye kamati badala ya kutangaza kwenye media
 
Tusihukumu bila ushahidi.

Je, ikithibitika Jk ndio muongo,mnafiki na mzandiki utasema nini?

Kwanini watu hamuhoji ukimya wa hizi Taasisi?

Nasi tusiwe wanafiki!
Huyu si mtu makini ni mshabiki wa CCM na watu wake!
 
Unaweza kaba koo taasisi kubwa za kidini zenye hadhi kubwa kama TEC na CCT? Pigana vita kote usisigee hizo taasisi kama CHADEMA inataka ipigwe chini nzima nzima uchaguzi 2015 pamoja na huyo Tundu Lisu isogeze vita zake kwenye hizo taasisi.Hizo taasisi ni moto wa kuotea mbali hasa kwa wanasiasa uchwara.

Huyo Padre katima na huyo mwingine wa CCT ni watu wadogo sana CCT na TEC hata kama waliiiona list ya wajumbe walioteuliwa katika hatua za awali haikuwa ndio fainal viongozi wa juu ambao ni maaskofu walikuwa na uwezo wa kuweka majina mengine tofauti na hilo la DR.katima na mwenzie yaliyopendekezwa bila kuwajibika kurudisha feedback kwa huyo Dr.KATIMA kwa kuwa kwa mfumo wao hawajibiki kwa junior.

Sasa kama huko mbele kwa mbele hakuona jina lake mtu wa kumwuuliza sio Tundu Lisu na hiyo kamati au Raisi .Na Chadema WAJIFUNZE Kuwasiliana na wakubwa wa taasisi za kidini kama raisi anavyofanya wakiiga staili hii ya tundu lissu ya kuwasiliana na kuchukulia serious hoja ya mtu mdogo wameisha.Raisi alichosema ni sahihi anajua alikopata majina.

Pole Tundu lISSU ULIYEPATA majina kwa DR.katima.

Ungekuwa mtu wa kutafakari kabla ya kuongea ungejiuliza hivi:

Hata CCT na shirikisho la vyama vya walemavu wote ni waongo??!!

Alafu hivi wewe ndio msemaji wa hizo Taasisi??!!
 
...hahahaaa kweli kamanda lisu kawashika pabaya,mmeambiwa,mmesikia,mnadhani,labda,huenda,nahisi...
Jamaa wameshindwa kabisa kujenga hoja wanabaki kusema muongo,mnafiki,mzandiki!
 
Tusihukumu bila ushahidi. Je, ikithibitika Jk ndio muongo,mnafiki na mzandiki utasema nini? Kwanini watu hamuhoji ukimya wa hizi Taasisi? Nasi tusiwe wanafiki!
lisemwalo either linaukweli or uwongo no matter what Lisu ni mwongo wa kupindukia, mie ni mwanangu wa kalibu sana ila hakishikilia kitu chake hakiachii kwa kuwa huwa anasema Tz bado ni wadhaifu sana, wakijua umesoma ata uwadanganye wanakubali kilahisi.
 
Tundu muongo, mnafik, mzandik.

Wewe changia mada kwa kujibu hoja na siyo kumtajataja mtu, nina mashaka na uelewa wako au la hujui unalolifanya ndo maana hoja zako siku zote ni majina ya watu tu na siyo maudhuhi.
 
Dr.Kitima ni miongoni mwa watu ambao mara kwa mara huwa anaalikwa Star tv katika vipindi mbalimbali na niseme ukweli tu huwa navutiwa sana na michango na kauli zake kwenye vipindi anavyoalikwa na kwakweli siku zote huwa anakuwa "outspoken".Mara nyingi anakuwa ni mtu wa kuikosoa serikali bila woga wala hofu,naamini wale ambao huwa mnamfuatilia katika luninga mtakubaliana nami.

Lakini ninachoshangaa ni kwanini mpaka leo yuko kimya juu ya sakata hili la Kikwete na Tundu Lissu kuhusu uteuzi wa mjumbe wa TEC kwenye tume ya katiba.Dr.Kitima ndie alietajwa na mh.Lissu kuwa aliiambia kamati ya bunge ya katiba,sheria na utawala kuwa mtu alieteuliwa na Raisi kuingia katika tume hiyo hakupendekezwa na TEC.

Sasa Dr. unashindwa nini kusema hadharani juu ya hili?

Hata hivyo,inawezekana hawezi kuongea bila idhini ya TEC kuhusu jambo hii.

Itakuwa ni jambo la ajabu Taasisi ya kidini kushindwa kusema ukweli au kuficha ukweli.

Watanzania tuachane na Jk na Lissu na badala yake tuzikabe koo hizi Taasisi.Haiingii akilini kuwajadili Tundu Lissu na Kikwete bila kuhoji ukimya wa hizi Taasisi.

Kitu kingine cha kujiuliza ni mbona hawakuhoji uteuzi wa wajumbe hao mara baada ya majina ya wajumbe wa katiba mpya kutangazwa??!!
Anzia title then usome thread yote uone kama unaelewa ulichoandika!
 
Back
Top Bottom