Salary Slip
Platinum Member
- Apr 3, 2012
- 52,154
- 162,570
Dr.Kitima ni miongoni mwa watu ambao mara kwa mara huwa anaalikwa Star tv katika vipindi mbalimbali na niseme ukweli tu huwa navutiwa sana na michango na kauli zake kwenye vipindi anavyoalikwa na kwakweli siku zote huwa anakuwa "outspoken".Mara nyingi anakuwa ni mtu wa kuikosoa serikali bila woga wala hofu,naamini wale ambao huwa mnamfuatilia katika luninga mtakubaliana nami.
Lakini ninachoshangaa ni kwanini mpaka leo yuko kimya juu ya sakata hili la Kikwete na Tundu Lissu kuhusu uteuzi wa mjumbe wa TEC kwenye tume ya katiba.Dr.Kitima ndie alietajwa na mh.Lissu kuwa aliiambia kamati ya bunge ya katiba,sheria na utawala kuwa mtu alieteuliwa na Raisi kuingia katika tume hiyo hakupendekezwa na TEC.
Sasa Dr. unashindwa nini kusema hadharani juu ya hili?
Hata hivyo,inawezekana hawezi kuongea bila idhini ya TEC kuhusu jambo hii.
Itakuwa ni jambo la ajabu Taasisi ya kidini kushindwa kusema ukweli au kuficha ukweli.
Watanzania tuachane na Jk na Lissu na badala yake tuzikabe koo hizi Taasisi.Haiingii akilini kuwajadili Tundu Lissu na Kikwete bila kuhoji ukimya wa hizi Taasisi.
Kitu kingine cha kujiuliza ni mbona hawakuhoji uteuzi wa wajumbe hao mara baada ya majina ya wajumbe wa katiba mpya kutangazwa??!!
Lakini ninachoshangaa ni kwanini mpaka leo yuko kimya juu ya sakata hili la Kikwete na Tundu Lissu kuhusu uteuzi wa mjumbe wa TEC kwenye tume ya katiba.Dr.Kitima ndie alietajwa na mh.Lissu kuwa aliiambia kamati ya bunge ya katiba,sheria na utawala kuwa mtu alieteuliwa na Raisi kuingia katika tume hiyo hakupendekezwa na TEC.
Sasa Dr. unashindwa nini kusema hadharani juu ya hili?
Hata hivyo,inawezekana hawezi kuongea bila idhini ya TEC kuhusu jambo hii.
Itakuwa ni jambo la ajabu Taasisi ya kidini kushindwa kusema ukweli au kuficha ukweli.
Watanzania tuachane na Jk na Lissu na badala yake tuzikabe koo hizi Taasisi.Haiingii akilini kuwajadili Tundu Lissu na Kikwete bila kuhoji ukimya wa hizi Taasisi.
Kitu kingine cha kujiuliza ni mbona hawakuhoji uteuzi wa wajumbe hao mara baada ya majina ya wajumbe wa katiba mpya kutangazwa??!!