Dr Benson Bana ni nani kwa Nchi hii?

Dr Benson Bana ni nani kwa Nchi hii?

Mboko

JF-Expert Member
Joined
Oct 8, 2010
Posts
1,095
Reaction score
293
Nimekusudia kuuliza hili swali kwani huyu mtu kila uteuzi yeye anasema ni mzuri na mwisho wake utasikia oooh watu aliochagua Rais wanamuangusha, nilimfuatilia sana yeye kila leo kitu kinachofanywa na CCM au serikali yake lazima aseme ni uamuzi mzuri sasa nashindwa kumuelewa, huu U Dr wake kaupata wapi??Nasema hivyo kwa kuwa mara nyingi anashindwa kusoma alama za nyakati mapema amekalia tu kusifu,sasa hapa huu mzigo wa baraza la Mawaziri kutoka 50 mpaka 55 bado tu anasema ni uteuzi mzuri ama kweli hawa Wasomi wa Bongo ni vituko vituko tu.
Hivi inakuwaje waandishi wa habari wamfuate kupata maoni mtu kama huyu anayeitwa Benson Bana wakati kuna wasomi wazuri tu zaidi yake huyu mtu anashindwa hata na mwanafunzi wake wa mwaka wa kwanza ambaye anachukua kozi ya Uongozi ifike wakati waandishi wa habari wajaribu kufuata watu wengine na sio huyu Bana kila siku.
Pia ningeomba tu ushauri kwa mustakabali wa Taifa letu hebu tuweke mambo ya siasa nje kidogo na kulinda ajira maake nimeona watu wengi sana especially watu wa Dar es Salaam ni wanafiki sana inapofika wakati wa kulinda maslahi ya Taifa wako radhi wakubali madudu ili walinde maslahi yao wakati hali hii ndo inarudisha maendeleo ya Taifa letu nasema hivyo kwa kuwa hawa wanaojiita wasomi wanaoishi Dar es Salaam wako hivyo wakati wanajisahua kuwa kama watapigania maslahi ya Taifa hata hao wanyewe watapunguza ule utegemezi ambao familia zao nyingi zinawategemea wao wamekalia kusifu kila kitu kinachofanywa na Serikali.
Sasa kinachotakiwa hapa kama kweli wengi wao wanasifu uteuzi huu wa mawaziri basi wakomae na kushurutisha wale wote waliofukuzwa kama Mawaziri na ambao wataendelea kufukuzwa basi wafikishwe mahakamani na sio aaah baraza limekaa vizuri.
 
Ni kibaraka wa jk na anampigia debe in the name of redet. Prof Mkandara alianzia huko akawa bosi udsm. Ndio maana anapambana apate nafasi kama mwenzie.
 
Dar wote wanaojifanya wasomi ni wanafiki na ndio mkoa unahujumu mapinduzi ya kweli.

Sashangai magazeti yanamfata huwa ni Jambo Leo, Uhuru na Habari Leo magazeti mengune hawawezi mfata.

Na TV huwa ni Channel Ten na TBC
 
Dr bana ni mmoja wa majambazi wakubwa wa ccm ambao wamelifikisha taifa mpaka hapa 2lipo.
 
Ni Mchumia tumbo ambaye amekosa mvuto siyo kwa wanafunzi,Wakufunzi wenzake,media makini bali hata wananchi kwa ujumla!Mpotezee tu.......Atakufa nao!
 
Benson Bana ni Kibaraka wa CCM kama walivyo watendaji wengi walioko serikalini na usalama wa Taifa. Wanabaki kusifia kusubiri kutupiwa chochote ili nao watumbue nchi kama hao waliopo. Siyo makosa yake lakini, kwa kiasi fulani ni hulka ya binadabu kupenda kufuata makandokando yanayopatikana kirahisi.
 

Hivi inakuwaje waandishi wa habari wamfuate kupata maoni mtu kama huyu anayeitwa
Benson Bana wakati kuna wasomi wazuri tu zaidi yake huyu mtu anashindwa hata na mwanafunzi wake wa mwaka wa kwanza ambaye anachukua kozi ya Uongozi ifike wakati waandishi wa habari wajaribu kufuata watu wengine na sio huyu Bana kila siku.
.

aisee huyo jamaa jina lake linafanana na bunsen burner kile kifaa kwenye chemistry laboratory...ndio yeye aliyekigundua nini...:whip:
 
nafikiri kama mawazo yako yanataka kufanana na ya kwangu!!! nimekuwa nikijiuliza sana kuhusu huu mtu DR.Benson Bana, baada ya Mkandala kuukwaa uongozi kama vice chancellor pale mlimani kupitia REDET(Kusifu Mgamba)na baada ya MTU MWENYE JINA GUMU aliyeteuliwa tume ya warioba sijui Palamagamba Kabudi..(ambaye nae ni mchumia tumbo) huyu Dr Bana amekuwa akijionyesha waziwazi ili angalau aambulie chochote..kifupi ni mchumia tumbo anasifu kila kitu.Nataka nimpe Dr ushauri wa bure its too late Dr!! think of the alternatives you missed the train 1hr!!
 
Bana = Nape. wote ni mavuvuzela...
 
sasa ulitaka ufwatwe wewee.tataizo letu watanzania wengi tunataka mtu asiseme ukweli halisi wa mambo.mtu hadhi ya bana ni msomi wa kiwango cha juu na ndio sababu mlimani wamempa aongoze idara muhimu.hao wasomi wengine unaosema wafuatwe malingo mengi na visomo vyao hawtoiushirikiano na waandishi wa habari sasa kwa nin Dr Bana asiwe chanzo kikuu cha maswala ya siasa kwa waandishi wa habari.RAI YANGU KWA JF...lazima jamani tuwe na ustahimili wa ma,bo ambayo wenzetu wanayasema hata kama yanatukera hasa wakati huu tunapohanza mchakato wa kupata KATIBA MPYA.ASANTE
 
Dkt Bana ni mkuu wa Idara ya Sayansi ya Siasa na Utawala.Katika taasisi za Elimu ya Juu,huwa kuna utarabu ama vigezo vinavyotumiwa kupata wakuu wa Idara.Moja ya taratibu ama vigezo hivyo ni uwezo wa kuongoza wanataaluma wenzake katika Idara,kiwango cha elimu na uzoefu wa mhusika.Hayo ni mambo ya ndani ya vyuo na hatuwezi kuyajua,angalau naamini kuwa wateuzi wanaelewa kuwa jamaa ni mzamivu.Sisi wananchi hatuwezi kuhoji taaaluma yake.Wasomi wenzake waliokubali kumpa PhD wanajua uwezo wake.Kuna mchakato mgumu unaofuatwa kwa mtu kuweza kupata PhD.
Sisi, huku mitaani, tumezoea kupima mtu kwa uzito wa hoja anazoibua na kuangalia iwapo zinaendana na kile tunaamini na kufuata.
Wapo watu wanaokubali mawazo ama fikra za kina Dkt. Mvungi na Dk.Lwaitama ...Lakini pia wapo watu wasiowakubali hawa wazamivu wetu.
Tofauti inayojitokeza ni ya kiitikadi.
 
Bana = Nape, wote ni vuvuzela... Yani kwa jinsi walivyo, JK akiwaambia geuka huku nataka.... wanageuka bila tatizo...
 
Nimekusudia kuuliza hili swali kwani huyu mtu kila uteuzi yeye anasema ni mzuri na mwisho wake utasikia oooh watu aliochagua Rais wanamuangusha, nilimfuatilia sana yeye kila leo kitu kinachofanywa na CCM au serikali yake lazima aseme ni uamuzi mzuri sasa nashindwa kumuelewa, huu U Dr wake kaupata wapi??Nasema hivyo kwa kuwa mara nyingi anashindwa kusoma alama za nyakati mapema amekalia tu kusifu,sasa hapa huu mzigo wa baraza la Mawaziri kutoka 50 mpaka 55 bado tu anasema ni uteuzi mzuri ama kweli hawa Wasomi wa Bongo ni vituko vituko tu.
Hivi inakuwaje waandishi wa habari wamfuate kupata maoni mtu kama huyu anayeitwa Benson Bana wakati kuna wasomi wazuri tu zaidi yake huyu mtu anashindwa hata na mwanafunzi wake wa mwaka wa kwanza ambaye anachukua kozi ya Uongozi ifike wakati waandishi wa habari wajaribu kufuata watu wengine na sio huyu Bana kila siku.
Pia ningeomba tu ushauri kwa mustakabali wa Taifa letu hebu tuweke mambo ya siasa nje kidogo na kulinda ajira maake nimeona watu wengi sana especially watu wa Dar es Salaam ni wanafiki sana inapofika wakati wa kulinda maslahi ya Taifa wako radhi wakubali madudu ili walinde maslahi yao wakati hali hii ndo inarudisha maendeleo ya Taifa letu nasema hivyo kwa kuwa hawa wanaojiita wasomi wanaoishi Dar es Salaam wako hivyo wakati wanajisahua kuwa kama watapigania maslahi ya Taifa hata hao wanyewe watapunguza ule utegemezi ambao familia zao nyingi zinawategemea wao wamekalia kusifu kila kitu kinachofanywa na Serikali.
Sasa kinachotakiwa hapa kama kweli wengi wao wanasifu uteuzi huu wa mawaziri basi wakomae na kushurutisha wale wote waliofukuzwa kama Mawaziri na ambao wataendelea kufukuzwa basi wafikishwe mahakamani na sio aaah baraza limekaa vizuri.

Huyu jamaa ni kiazi kabisa nina wasiwasi na upeo wake amesoma lakini hakuelimika..
 
Back
Top Bottom