Down memory lane...

Wyatt...
Ukoloni ulikuja na changamoto nyingi sana.

Leo hii katika umri wangu wa uzee nikiangalia nyuma naona zaidi kuliko
nilivyokuwa naoana nilipokuwa kijana.

Uoni huu si wa macho bali ni kuangalia kwa ndani ya nafsi.

Nimezaliwa tayari nimekuta wazee wangu wengi wamechotwa sana na
Uzungu na wakau-perfect hata kuwashinda Wazungu wenyewe.

Mtoto aliyezaliwa katika mazingira kama haya hawazi kusalimika kwa
urahisi.

Napata akili nasikia muziki unaopigwa nyumbani kwetu ni wa Loius
Armstrong, Alma Cogan, Victor Sylvester, Septet Habanero na kidogo
Salum Abdallah, Kiko Kids na Cuban Marimba Cha Cha Band na Mwenda
Jean Bosco kuwataja wachache.

Afro Americans walikuwa na ushawishi mkubwa lakini zaidi si kwa wazee .
wetu ila kwetu sisi ambao kwao ni kizazi cha pili.

Tukisikiliza muziki wa Wilson Picket, James Brown, Aretha Franklin,
Helen Shapiro, Cliff Richard na Elvis Presley.

Sal Davis alikuwa ''all rounder,'' aliweza kupiga mchanganyiko wa muziki
wa Kimarekani na muziki wa Ulaya na hata staili za kwao Mombasa.

Nimeandika maisha ya Sal Davis bado kuchapa kitabu lakini unaweza
kusoma maisha yake hapo chini kwenye hii link:


View attachment 1176734

Unataka sasa kujua asili yangu...

Sidhani kama kuna watu wanataka kujua baba yangu nani, mama yangu
nani, nk.

Ila nitakueleza kuwa historia yetu iko Dar es Salaam sasa miaka 100 na
mimi nimejifunza historia hii na naweza kwenda nyuma vizazi saba ingawa
sasa na wajukuu zangu tushafika vizazi tisa wote Waafrika weusi kutoka
Tanganyika na Belgian Congo.
Hizo picha ungezitolea Maelezo
 
Mikocheni...
Huwa kuna watu hawapendi kalamu yangu.
Hili si tatio.

Tatizo linakuja pale kwa kuwa hapendi niandikayo ananitukana.

Ikiwa matusi ni makubwa sana nami nachelea nikimjibu anaweza kuja na
matusi makubwa zaidi mie hunyamaza kimya huwa simjibu kuepusha shari.

Kheri nusu shari kuliko shari kamili.

Nakujibu wewe kwa kuwa tusi lako linastahamilika.

Wataalamu wa Development Theory wanasema kuwa jinsi nchi inavyokuwa
na watu wanaothamini dini kwa kuipenda ndivyo maendeleo yanavyopatikana.

Sasa hii wataalamu wakaipeleka mbele zaidi na wamegundua kuwa binadamu
wenye dini wakafuata mafunzo sahihi huwa na maisha mazuri na huepukana
na mengi ya kudhuru.
Kuna watu wakiona umepandisha uzi, basi matumbo yanawakata utafikiri wamewekewa nyembe tumboni!!
 
Msimamo wangu Kuhusu wazee wetu wapigania uhuru wote walifanya kazi kubwa
Wewe una weakness moja ya kudhani wazee wakiislam waliplay role kubwa Kuliko wale ambao hawakuwa waislam Hii si kweli kabisa

Ahsante mkuu
Mikocheni,,,
Tatizo lako ni kuwa wewe huijui historia ya TANU.

Sikulaumu hauko peke yako wewe ni moja wa kundi kubwa sana wa wasiojua.

Mimi ''sidhanii'' katika historia hii nimefanya utafiti na nimeandika kwanza kitabu
na nina ''paper,'' nyingi nimeandika kuhusu somo hili kiasi nimeshirikishwa katika
miradi miwili ya kuhifadhi historia hii.

Nimeshiriki katika mradi wa Oxford University Press, Nairobi na wamechapa kitabu
nilichoandika, ''The Torch on Kilimanjaro,'' (2007).

1565533671575.png


Nimeshiriki katika mradi wa Dictionary of African Dictionary (DAB) uliokuwa chini
ya Havard na Oxford University Press, New York (2011).

Kitabu cha Sykes kimepitiwa na wanahistoria maarufu wanaoijua historia ya Tanzania
kama John Iliffe, Jonathon Glassman na James Brennan.

Ukimtoa Iliffe hao wawili waliobakia tunafahamiana kwa miaka na kilichotukutanisha
ni historia hii.

Ningeweza kuendelea zaidi.

Lakini kubwa katika waasisi wa African Association (1929) aliyeandika historia hiyo ni
Kleist Sykes na walikuwa watu 9 hakuna aliyeandika historia hiii na moja ya sababu
ni kuwa michango yao haikuwa mikubwa sana na haikudumu kwa muda mrefu hivyo
hawakuwa na mengi ya kuandika.

Katika waasisi 17 wa TANU (1954) hakuna aliyeweza kuandika historia yake ukimtoa
Abdul Sykes na yeye aliweza kufanya hili kwa kuwa alikuwa anaijua historia yote na
alikuwa na nyaraka.

Jambo la kusikitisha ni kuwa historia hii Abdul hakumaliza kuindika kwa sababu
palizuka sintofahamu kama hizi tunazojadili hapa hivi sasa.

Wewe huijui historia hii lakini hutaki kuwasikiliza wenye kuijua.

Hivi tunavyojadili, kutokana na kitabu cha Sykes Prof. Shivji na wenzake wanaandika
kitabu cha maisha ya Mwalimu Nyerere nia ikiwa pamoja na mengine, kujua nini
ulikuwa mchango wake katika kuunda TANU.

Naamini unauona mnyororo huo wa TANU kuanzia kwa Kleist Sykes hadi kwa
wanae Abdul na Ally katika historia hii.

Ikiwa ipo historia ya TANU isiyo kuwa hii hadi hivi sasa kitabu kipo mwaka wa 20
bado hakijaandikwa.
 
Mikocheni,,,
Tatizo lako ni kuwa wewe huijui historia ya TANU.

Sikulaumu hauko peke yako wewe ni moja wa kundi kubwa sana wa wasiojua.

Mimi ''sidhanii'' katika historia hii nimefanya utafiti na nimeandika kwanza kitabu
na nina ''paper,'' nyingi nimeandika kuhusu somo hili kiasi nimeshirikishwa katika
miradi miwili ya kuhifadhi historia hii.

Nimeshiriki katika mradi wa Oxford University Press, Nairobi na wamechapa kitabu
nilichoandika, ''The Torch on Kilimanjaro,'' (2007).

View attachment 1178395

Nimeshiriki katika mradi wa Dictionary of African Dictionary (DAB) uliokuwa chini
ya Havard na Oxford University Press, New York (2011).

Kitabu cha Sykes kimepitiwa na wanahistoria maarufu wanaoijua historia ya Tanzania
kama John Iliffe, Jonathon Glassman na James Brennan.

Ukimtoa Iliffe hao wawili waliobakia tunafahamiana kwa miaka na kilichotukutanisha
ni historia hii.

Ningeweza kuendelea zaidi.

Lakini kubwa katika waasisi wa African Association (1929) aliyeandika historia hiyo ni
Kleist Sykes na walikuwa watu 9 hakuna aliyeandika historia hiii na moja ya sababu
ni kuwa michango yao haikuwa mikubwa sana na haikudumu kwa muda mrefu hivyo
hawakuwa na mengi ya kuandika.

Katika waasisi 17 wa TANU (1954) hakuna aliyeweza kuandika historia yake ukimtoa
Abdul Sykes na yeye aliweza kufanya hili kwa kuwa alikuwa anaijua historia yote na
alikuwa na nyaraka.

Jambo la kusikitisha ni kuwa historia hii Abdul hakumaliza kuindika kwa sababu
palizuka sintofahamu kama hizi tunazojadili hapa hivi sasa.

Wewe huijui historia hii lakini hutaki kuwasikiliza wenye kuijua.

Hivi tunavyojadili, kutokana na kitabu cha Sykes Prof. Shivji na wenzake wanaandika
kitabu cha maisha ya Mwalimu Nyerere nia ikiwa pamoja na mengine, kujua nini
ulikuwa mchango wake katika kuunda TANU.

Naamini unauona mnyororo huo wa TANU kuanzia kwa Kleist Sykes hadi kwa
wanae Abdul na Ally katika historia hii.

Ikiwa ipo historia ya TANU isiyo kuwa hii hadi hivi sasa kitabu kipo mwaka wa 20
bado hakijaandikwa.
Mwafrika anaamini kuna mzungu huko uzunguni anaijua historia yake yeye mwafrika kuliko yeye mwenyewe


Sisi tuna matatizo wacha iendelee kubaki mzungu ndio aligundua Mlima Kilimanjaro, ziwa Victoria nk
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom