Down memory lane...

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,917
30,259
DOWN MEMORY LANE...​

1565333078602.png

Kushoto Salim Himid na Sal Davis (Shariff Salim Abdallah)

Hii ni historia ya Msikiti Mkuu wa Paris ambao wenyewe wanauita Grande Mosquee de Paris na ni msikiti wenye mengi sana ya kukumbukwa.

Nimeswali msikiti huu mara mbili mwaka wa 1993 na mwaka wa 2011.
Sala moja ya mwaka wa 2011 ilikuwa Sala ya Ijumaa.

Wangazija wako wengi sana Pairis na huu ni msikiti wao,

Mwaka wa 2011 nilikuwa Paris na rafiki yangu na Salim Himid na yeye ndiye aliyenipeleka kuswali Ijumaa.

Salim Himid is an extremely intelligent person yaani ni mmoja wa watu ambao Allah kawajalia akili ambayo si za kawaida na nimefahamishwa hili na jamaa zake.

Kabla ya kufahamiana na Salim nilipata siku moja kukutana na kaka yake Dr. Said Himid.

Dr. Himid alikuwa amekuja Dar es Salaam na tukakutana kwenye mwaliko wa futari kwa jamaa yake mmoja.

Dr. Said Himid wakati wake alitokea mwanafunzi wa kwanza katika mitihani ya Cambridge.

Salim Himid amezaliwa Zanzibar akasoma Ufaransa akawa Foreign Minister Comoro chini ya uongozi wa Ali Solih.

Inawezekana Salim Himid alikuwa Mzanzibari wa kwanza kushika nafasi ya juu Ngazija au mmoja wa Wazanzibar walioshika nafasi muhimu kisiwani hapo.

Salim anasema Kingazija, Kiingereza, Kifafaransa, Kiarabu na Kiswahili vizuri bila wasiwasi.
Serikali ya Ali Solih ilipopinduliwa na Bob Denard mamluki kutoka Afrika ya Kusini. Salim akafungwa ingawa alikuwa hayuko serikalini baada ya kutofautiana na Solih.

Salim Himid alipotoka jela akaenda exile Paris.

Salim Himid na Salim Abdallah aka Sal Davis nimewapiga picha katika Barza yetu Lumumba Avenue.

Walikuwa wanakutana takriban baada ya zaidi ya miaka 40.

Salim mara ya mwisho kamuona Sal Davis ilikuwa mwaka wa 1963 kabla ya mapinduzi,
Salim akamkumbusha kitu Sal alichokuwa amesahau na Sal akapiga mshangao akasema, ''Nilisahau kabisa wewe una kumbukumbu kubwa sana.''

Salim alimwambia Sal Davia kuwa mara ya mwisho kamuona ilikuwa mwaka wa 1963 alipofanya show Zanzibar katika Ukumbi wa Said Khalifa.

Salim akiusudu muziki wa Sal.

Akamwambia baada ya show Sal alikwenda kwenye gari lililokuwa nje ya ukumbi linauza Hall's Ice Cream, kulikuwa na microphone na loud speaker na Sal akaimba nyimbo moja ya Perry Como vijana wenzake wakiwa wamelizunguka gari lile.

Sal Davis miaka ile alikuwa star mkubwa aliyeanza career yake Uingereza akiwa kijana mdogo hajafikisha hata miaka 20.

Baada ya 1963 mapinduzi Salim akaondoka kwenda France kutafuta elimu akisafiri overland akivuka mpaka mmoja hadi mwingine hadi akafika Cairo kabla ya kuvuka bahari kuingia Ulaya.

Anasema alipofika Cairo akakuta Mohamed Abduwahab mwimbaji maarufu wa Misri enzi hizo ametoa nyimbo ambayo ilivuma Misri yote.

Nyimbo hii ilikuwa kipigwa kwenye radio taxi drivers wanaegesha taxi zao pembeni wakiongeza sauti za radio zao ndani ya magari yao kusikiliza.

Hii ilikuwa miaka ya 1960s wakati wa Gamal Abdel Nasser na siasa za Arab Nationalism zilikuwa juu kabisa.

Iko siku nilikuwa nasafiri na Egypt kutoka Dar es Salaam naelekea London.

Ndege yetu inaondoka sita ya usiku lakini kwa bahati mbaya ikawa na hitilafu ikabidi tuondoke siku ya pili mchana kwa hiyo kufika Cairo ndege yetu ya kuunganisha ikawa iemshaondoka ikabidi tuwekwe hoteli sehemu moja inatwa Heliopolis hadi siku ya pili mchana.

Tulipokuwa tuna-check in pale hotelini nikawa naona kwenye TV Mohamed Abdulwahab anapiga muziki wake na ikisha nyimbo hii inaingia nyingine.

Kumbe siku ile ndiyo alikuwa amefariki na TV stations na FM Radio zote zilikuwa katika maombolezo.

Nilikuwa na Salim Paris nikitokea Berlin kila siku asubuhi alikuwa akinifuata hotelini kwangu kunitembeza mjini na mie sikumwacha akawa njia nzima na kutwa nzima ananisomesha mambo yaliyopita Zanzibar, Comoro na Ufaransa na katika duru za siasa na diplomasia katika mambo aliyoshuhudia kwa macho yake mwenyewe.

Ugomvi wangu na Salim kila akija Dar es Salaam tikikaa na kuzungumza ni kuwa hajakubali kuandika.

Sijui kwa nini anafanya ajizi.

1565333648454.png

Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje Salim Himid na Seif Shariff Ngazija

Picha: Kushoto Salim Himid na Sal Davis wakiwa Barzani Lumumba Avenue, Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje Salim Himid na Seif Shariff Ngazija, Sal Davis akiwa Ujerumani na Mwandishi nje ya Grande Mosquee de Paris 1993.
 
Hivi miaka ya 1960’s kulikua na “FM” radios kweli?

I mean “FM”!

Yaani Frequency Modulation technology ilikua tayari ishakuja mainstream miaka ya early 1960’s?

Mmh
Babu katugonga fix eeh? Maana 1985 bado hazikukuwepo, tulikuwa tunakula RTD kwenye AM1 na AM2 :D:D:D
 
Always talking about religion ujue unatatizo pahala
Psychological your not okey at all
Mikocheni...
Huwa kuna watu hawapendi kalamu yangu.
Hili si tatio.

Tatizo linakuja pale kwa kuwa hapendi niandikayo ananitukana.

Ikiwa matusi ni makubwa sana nami nachelea nikimjibu anaweza kuja na
matusi makubwa zaidi mie hunyamaza kimya huwa simjibu kuepusha shari.

Kheri nusu shari kuliko shari kamili.

Nakujibu wewe kwa kuwa tusi lako linastahamilika.

Wataalamu wa Development Theory wanasema kuwa jinsi nchi inavyokuwa
na watu wanaothamini dini kwa kuipenda ndivyo maendeleo yanavyopatikana.

Sasa hii wataalamu wakaipeleka mbele zaidi na wamegundua kuwa binadamu
wenye dini wakafuata mafunzo sahihi huwa na maisha mazuri na huepukana
na mengi ya kudhuru.
 
Whytt,
Hapana rejea usome tena.

Hapo nazungumza kifo cha Mohamed Abdulwahab na ambae alifariki 1991 siku niko Cairo.

Mohamed

Hakuna shida mkuu,nimekuelewa!

Kuhusu Sal Davis mkuu yaelekea mlikua mpo influenced sana na utamaduni wa ki-black America kama tulivyo sisi sasa hivi!

Kwa kifupi mlikua mabitozi of the time!

Ndio maana hata marehemu Abdulrahman Babu alikua anawapenda sana Niggaz mpaka akaenda ishi nao America!

Pamoja na kwamba mnapenda sana utamaduni wa Mwarabu ila Mmarekani mweusi ilikua ni kitu roho yenu inapenda zaidi!

Hivi ustaadhi Mohamed nataka nijue asili yako genetically,uzao wenu ulitoka wapi originally?

Kwa mfano mimi ni Mchagga kwa wazazi wote wawili,ancestors wangu wali-migrate from Ethiopia to Kenya then Moshi 500yrs iliyopita,ndio maana genetically nina 6%-Eurasia na 4%-Maasai na 70%-Eastern Bantu na 20%-Western Bantu!

I want to know kama una Arabic ancestry maana upo strongly attached to Arabic way of living,talking,etc..Which is totally okay

Ila sometimes I wonder kama wewe ni black African Bantu,hutoi shout out kwa black African ancestry ambayo I think wewe una more than 90%!
 
Mikocheni...
Huwa kuna watu hawapendi kalamu yangu.
Hili si tatio.

Tatizo linakuja pale kwa kuwa hapendi niandikayo ananitukana.

Ikiwa matusi ni makubwa sana nami nachelea nikimjibu anaweza kuja na
matusi makubwa zaidi mie hunyamaza kimya huwa simjibu kuepusha shari.

Kheri nusu shari kuliko shari kamili.

Nakujibu wewe kwa kuwa tusi lako linastahamilika.

Wataalamu wa Development Theory wanasema kuwa jinsi nchi inavyokuwa
na watu wanaothamini dini kwa kuipenda ndivyo maendeleo yanavyopatikana.

Sasa hii wataalamu wakaipeleka mbele zaidi na wamegundua kuwa binadamu
wenye dini wakafuata mafunzo sahihi huwa na maisha mazuri na huepukana
na mengi ya kudhuru.
Sawa mohamed said LAKINI tumekuwa wamoja zaidi kuliko. Mambo ya dini ambayo kwa nchi yetu dini ni person issue maana tunaepusha balaaa ambalo ww kwa mtizamo wako hulioni maana waislam na wakristo kama...half-half, sasa tukikosea kidogo tu kwenye kuli-handle mlipuko utatokea na ndio maana wapinzani wako huwa wanaku-crash mapema kwa nia nzuri tu...nakuomba kaka mkubwa VUMILIA na badilika usiengemee sana udini kwenye public edition
 
Sawa mohamed said LAKINI tumekuwa wamoja zaidi kuliko. Mambo ya dini ambayo kwa nchi yetu dini ni person issue maana tunaepusha balaaa ambalo ww kwa mtizamo wako hulioni maana waislam na wakristo kama...half-half, sasa tukikosea kidogo tu kwenye kuli-handle mlipuko utatokea na ndio maana wapinzani wako huwa wanaku-crash mapema kwa nia nzuri tu...nakuomba kaka mkubwa VUMILIA na badilika usiengemee sana udini kwenye public edition
Emanuel...
Tatizo ni kuwa Waislam wanabaguliwa kwa dini yao na hili ndilo
Prof. Malima alililolikuta Wizara ya Elimu na akamweleza Rais
Mwinyi.


Hii ilikuwa mwaka wa 1987.

Mwaka wa 1991 Kitwana Kondo ndani ya Bunge akatahadharisha
tena tatizo hili hili.

Soma hapo chini:

''Ninayo ripoti ya mwaka huu. Waliofanya mtihani wa darasa la saba kuingia darasa la tisa, asilimia 71 Waislamu. Asilimia 29 ni wengine. Walioshinda katika wale asilimia 71 ni asilimia 21. Katika wale 29 walioshinda tena sema mwenyewe. Katika asilimia 29 waliokwenda shuleni ni asilimia 79. Katika asilimia 71 waliokwenda darasa la tisa ni asilimia 21.

Sasa kuna moja, ama Waislamu wajinga ama akili yao haifanyi kazi, ama mtu ukiwa Muislamu wewe huna kitu, ama kuna kitu. Sasa namwomba Waziri anayehusika, anaposema aseme ya kwamba kwa hali ilivyo Waislamu wameumbwa wajinga. Au kwa hali ilivyo kuna sababu kadha, kadha. Mwalimu Nyerere alisema zamani ifanywe bidii ya kuwanyanyua waliokuwa chini. Sasa bidii hii siyo ya kuwanyanyua waliokuwa chini. Bidii hii ni ya kuwakandamiza waliokuwa chini.''

Hotuba ya Mh. Kitwana Kondo (MB) aliyoitoa Bungeni Dodoma, 1999
Mohamed Said February 17, 2015 0
Annur Na.187- Feb.5-11, 1999
Hotuba ya Mh. Kitwana Kondo (MB) aliyoitoa Bungeni Dodoma


Wizaraya Elimu haikuweza kutoa majibu maana hapa aliyekuwa anakula na kipofu kamshika
mkono.

Ushahidi uko mwingi sana.

Ndugu yangu kweli unawaasa Waislam wavumilie kudhulumiwa?

Labda nikuulize swali haya yangefanywa na Waislam wewe
ungekuja la nasaa kwa ndugu zako wavumilie watoto wao
kunyimwa elimu?

Nakuhitimishia kwa kukupa kauli nini Allah anawafunza Waislam.
Allah anasema, ''Msidhulumu wala msikubali kudhulumiwa.''

Huo mlipuko ambao wewe unauogopa kutokea hautokei ila penye
dhulma.
 
Mohamed

Hakuna shida mkuu,nimekuelewa!

Kuhusu Sal Davis mkuu yaelekea mlikua mpo influenced sana na utamaduni wa ki-black America kama tulivyo sisi sasa hivi!

Kwa kifupi mlikua mabitozi of the time!

Ndio maana hata marehemu Abdulrahman Babu alikua anawapenda sana Niggaz mpaka akaenda ishi nao America!

Pamoja na kwamba mnapenda sana utamaduni wa Mwarabu ila Mmarekani mweusi ilikua ni kitu roho yenu inapenda zaidi!

Hivi ustaadhi Mohamed nataka nijue asili yako genetically,uzao wenu ulitoka wapi originally?

Kwa mfano mimi ni Mchagga kwa wazazi wote wawili,ancestors wangu wali-migrate from Ethiopia to Kenya then Moshi 500yrs iliyopita,ndio maana genetically nina 6%-Eurasia na 4%-Maasai na 70%-Eastern Bantu na 20%-Western Bantu!

I want to know kama una Arabic ancestry maana upo strongly attached to Arabic way of living,talking,etc..Which is totally okay

Ila sometimes I wonder kama wewe ni black African Bantu,hutoi shout out kwa black African ancestry ambayo I think wewe una more than 90%!
Wyatt...
Ukoloni ulikuja na changamoto nyingi sana.

Leo hii katika umri wangu wa uzee nikiangalia nyuma naona zaidi kuliko
nilivyokuwa naoana nilipokuwa kijana.

Uoni huu si wa macho bali ni kuangalia kwa ndani ya nafsi.

Nimezaliwa tayari nimekuta wazee wangu wengi wamechotwa sana na
Uzungu na wakau-perfect hata kuwashinda Wazungu wenyewe.

Mtoto aliyezaliwa katika mazingira kama haya hawazi kusalimika kwa
urahisi.

Napata akili nasikia muziki unaopigwa nyumbani kwetu ni wa Loius
Armstrong, Alma Cogan, Victor Sylvester, Septet Habanero na kidogo
Salum Abdallah, Kiko Kids na Cuban Marimba Cha Cha Band na Mwenda
Jean Bosco kuwataja wachache.

Afro Americans walikuwa na ushawishi mkubwa lakini zaidi si kwa wazee .
wetu ila kwetu sisi ambao kwao ni kizazi cha pili.

Tukisikiliza muziki wa Wilson Picket, James Brown, Aretha Franklin,
Helen Shapiro, Cliff Richard na Elvis Presley.

Sal Davis alikuwa ''all rounder,'' aliweza kupiga mchanganyiko wa muziki
wa Kimarekani na muziki wa Ulaya na hata staili za kwao Mombasa.

Nimeandika maisha ya Sal Davis bado kuchapa kitabu lakini unaweza
kusoma maisha yake hapo chini kwenye hii link:


1565360019922.png


Unataka sasa kujua asili yangu...

Sidhani kama kuna watu wanataka kujua baba yangu nani, mama yangu
nani, nk.

Ila nitakueleza kuwa historia yetu iko Dar es Salaam sasa miaka 100 na
mimi nimejifunza historia hii na naweza kwenda nyuma vizazi saba ingawa
sasa na wajukuu zangu tushafika vizazi tisa wote Waafrika weusi kutoka
Tanganyika na Belgian Congo.
 
Sorry KM nakukwazwa mkuu mi huwa nipo mnyoofu sipindishi neno ila kuongelea kitu kimoja in a regular times lazima kuna Tatizo pahala wala sina lengo la kukudhalilisha
Mikocheni...
Huwa kuna watu hawapendi kalamu yangu.
Hili si tatio.

Tatizo linakuja pale kwa kuwa hapendi niandikayo ananitukana.

Ikiwa matusi ni makubwa sana nami nachelea nikimjibu anaweza kuja na
matusi makubwa zaidi mie hunyamaza kimya huwa simjibu kuepusha shari.

Kheri nusu shari kuliko shari kamili.

Nakujibu wewe kwa kuwa tusi lako linastahamilika.

Wataalamu wa Development Theory wanasema kuwa jinsi nchi inavyokuwa
na watu wanaothamini dini kwa kuipenda ndivyo maendeleo yanavyopatikana.

Sasa hii wataalamu wakaipeleka mbele zaidi na wamegundua kuwa binadamu
wenye dini wakafuata mafunzo sahihi huwa na maisha mazuri na huepukana
na mengi ya kudhuru.
 


Wataalamu wa Development Theory wanasema kuwa jinsi nchi inavyokuwa
na watu wanaothamini dini kwa kuipenda ndivyo maendeleo yanavyopatikana.

.


No research no right to speak

Wazungu wa ulaya walikuwa masikini wakutupwa walipokuwa wanakumbatia dini kumbuka (medieval period) ila walipoamua kutenganisha dini na utaalamu ndio walianza kuonja maendeleo

Dini inakiasi chake

Hata nchi za kiarabu zimeanza kupiga hatua baada ya kuanza kutenganisha dini na utawala
 
No research no right to speak

Wazungu wa ulaya walikuwa masikini wakutupwa walipokuwa wanakumbatia dini kumbuka (medieval period) ila walipoamua kutenganisha dini na utaalamu ndio walianza kuonja maendeleo

Dini inakiasi chake

Hata nchi za kiarabu zimeanza kupiga hatua baada ya kuanza kutenganisha dini na utawala
Mikocheni...
Ahsante kaka huo si uwanja wangu kwa hiyo sina mengi ya kuchangia.
Amini na fuata staili ya maisha uyapendayo kwani hii ni nchi huru.

Lakini hujasema lolote kuhusu wale wana TANU waliomsindikiza Baba
wa Taifa
safari ya kwanza UNO Februari 1955.
 
Mohamed Said Bitozi wa siku nyingi wewe, toka enzi za Earl Klugh mpaka crooning tunes za Perry Como.

Ninazo rekodi zao hawa, ukimuweka Earl Klugh halafu ukafuatia na Wes Montgomery balaa tupu.

Watoto wa siku hizi ukiwatajia majina haya hata hawawezi kuyajua.
 
Wyatt...
Ukoloni ulikuja na changamoto nyingi sana.

Leo hii katika umri wangu wa uzee nikiangalia nyuma naona zaidi kuliko
nilivyokuwa naoana nilipokuwa kijana.

Uoni huu si wa macho bali ni kuangalia kwa ndani ya nafsi.

Nimezaliwa tayari nimekuta wazee wangu wengi wamechotwa sana na
Uzungu na wakau-perfect hata kuwashinda Wazungu wenyewe.

Mtoto aliyezaliwa katika mazingira kama haya hawazi kusalimika kwa
urahisi.

Napata akili nasikia muziki unaopigwa nyumbani kwetu ni wa Loius
Armstrong, Alma Cogan, Victor Sylvester, Septet Habanero na kidogo
Salum Abdallah, Kiko Kids na Cuban Marimba Cha Cha Band na Mwenda
Jean Bosco kuwataja wachache.

Afro Americans walikuwa na ushawishi mkubwa lakini zaidi si kwa wazee .
wetu ila kwetu sisi ambao kwao ni kizazi cha pili.

Tukisikiliza muziki wa Wilson Picket, James Brown, Aretha Franklin,
Helen Shapiro, Cliff Richard na Elvis Presley.

Sal Davis alikuwa ''all rounder,'' aliweza kupiga mchanganyiko wa muziki
wa Kimarekani na muziki wa Ulaya na hata staili za kwao Mombasa.

Nimeandika maisha ya Sal Davis bado kuchapa kitabu lakini unaweza
kusoma maisha yake hapo chini kwenye hii link:


View attachment 1176734

Unataka sasa kujua asili yangu...

Sidhani kama kuna watu wanataka kujua baba yangu nani, mama yangu
nani, nk.

Ila nitakueleza kuwa historia yetu iko Dar es Salaam sasa miaka 100 na
mimi nimejifunza historia hii na naweza kwenda nyuma vizazi saba ingawa
sasa na wajukuu zangu tushafika vizazi tisa wote Waafrika weusi kutoka
Tanganyika na Belgian Congo.

Umetoa madini hatari kabisa!

Once again nimeamini wewe ni very good author and story teller!

Kwahiyo nipo safe nikisema true origin ni Eastern Congo?

Ambapo offshoot yenu ni Waha?

Miaka 100 si mingi sana,nitakua safe zaidi nikisema labda nyie ni ile wave ya migration ya watu kutoka Eastern Congo na Kigoma kuja Dar hasa hasa kwa shughuli ya reli ya Mjerumani?

Kwa kifupi nyie ndio generally mnaitwa Waha (japo ni mixture ya makabila kibao kutoka western TZ) mlio occupy Kariakoo na Posta!?

Au nyie ndio wale wa mapema kabisa kipindi cha utumwa mka occupy Bagamoyo,hapa Dar centre na Zanzibar?

Sawa!

Kwahiyo hamna any trace ya Arabic ancestor kwenye uzao wenu ambae you know off?

Sawa pia!

Mimi nilidhani nyie ni lazima mtakua Wandengereko,au Wazaramo,au Waswazi,etc na pia mixed up with Arabic traces!Kumbe I was wrong!

Kwa jinsi ulivyo,unavyoandika,misimamo yako,coast culture ndio hasa yenu.

Pamoja na islamic religious influence na Swahili/Arabic culture mlionayo,bado mabitoz wa Kimarekani!

Kwa akili yangu fupi nilijua utakua upo very very affiliated na Arabic music and zero Western influence hasa ya Black Americans!

Wewe ni Mmarekani mweusi,dini ni msikitini tu!

Hahhahaha
 
Umetoa madini hatari kabisa!

Once again nimeamini wewe ni very good author and story teller!

Kwahiyo nipo safe nikisema true origin ni Eastern Congo?

Ambapo offshoot yenu ni Waha?

Miaka 100 si mingi sana,nitakua safe zaidi nikisema labda nyie ni ile wave ya migration ya watu kutoka Eastern Congo na Kigoma kuja Dar hasa hasa kwa shughuli ya reli ya Mjerumani?

Kwa kifupi nyie ndio generally mnaitwa Waha (japo ni mixture ya makabila kibao kutoka western TZ) mlio occupy Kariakoo na Posta!?

Au nyie ndio wale wa mapema kabisa kipindi cha utumwa mka occupy Bagamoyo,hapa Dar centre na Zanzibar?

Sawa!

Kwahiyo hamna any trace ya Arabic ancestor kwenye uzao wenu ambae you know off?

Sawa pia!

Mimi nilidhani nyie ni lazima mtakua Wandengereko,au Wazaramo,au Waswazi,etc na pia mixed up with Arabic traces!Kumbe I was wrong!

Kwa jinsi ulivyo,unavyoandika,misimamo yako,coast culture ndio hasa yenu.

Pamoja na islamic religious influence na Swahili/Arabic culture mlionayo,bado mabitoz wa Kimarekani!

Kwa akili yangu fupi nilijua utakua upo very very affiliated na Arabic music and zero Western influence hasa ya Black Americans!

Wewe ni Mmarekani mweusi,dini ni msikitini tu!

Hahhahaha
Wyatt...
Mimi ni Mmanyema na babu yangu mkuu aliingia Tanganyika miaka ya
mwisho ya 1800 kama askari wa Wajerumani na alifikizia Shirati Bomani.

Hili Boma lipo mpaka sasa.
Jina lake Abdallah Samitungo Muyukwa.

Sisi ni Wamanyema.
Mama yangu Mzaramo jina lake Baya bint Sheikh Mohamed Mvamila.

Hiyo ''influence,'' unayoizungumza imetoka huko kwa Sheikh Mohamed
Mvamila
kutoka Mkamba.

Lakini kabila katika miaka hii imepoteza maana pakubwa sana.

''Social class,'' ndiyo imechukua nafasi ya makabila.
Wamanyema na Waha ni watu mbali sana.

Mhariri wa kitabu changu cha Sykes alikuwa Mama wa Kiingereza na
alipomaliza kuhariri kitabu akaniletea ''note'' kaandika kwa mkono wake
akanambia kuwa kitabu changu kimempa raha sana kukihariri na akasema,
''You are a story teller.''

Ikiwa umependezewa ingia mohamedsaidsalum.blogspot.com kuna mengi
unaweza kufanya search kwa majina ya watu au matukio etc.
 
Mohamed Said Bitozi wa siku nyingi wewe, toka enzi za Earl Klugh mpaka crooning tunes za Perry Como.

Ninazo rekodi zao hawa, ukimuweka Earl Klugh halafu ukafuatia na Wes Montgomery balaa tupu.

Watoto wa siku hizi ukiwatajia majina haya hata hawawezi kuyajua.
Kiranga,
Umenipeleka mbali sana...
 
[B[/B]
Lakini hujasema lolote kuhusu wale wana TANU waliomsindikiza Baba
wa Taifa
safari ya kwanza UNO Februari 1955.

Msimamo wangu Kuhusu wazee wetu wapigania uhuru wote walifanya kazi kubwa
Wewe una weakness moja ya kudhani wazee wakiislam waliplay role kubwa Kuliko wale ambao hawakuwa waislam Hii si kweli kabisa

Ahsante mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom