Dowans lazima walipwe

RIPOTI YA KAMATI YA BUNGE


YALIYOMO
VIFUPISHO VYA MANENO………………………………………………….iii - iv
1.0 UTANGULIZI...........................................................1
1.1 Hoja ya Kuunda Kamati Teule ......................................................................... 1
1.2 Wajumbe na Hadidu za Rejea.......................................................................... 2
1.3 Utekelezaji wa Majukumu ................................................................................ 4
2.0 UKAME NA TATIZO LA UZALISHAJI UMEME NCHINI .......... 10
2.1 Taarifa za Awali na Hatua za Serikali .......................................................... 10
2.2 Maandalizi ya Zabuni ....................................................................................... 15
2.3 Mchakato wa Zabuni ndani ya TANESCO ..................................................... 18
2.3.1 Vigezo vya Tathmini (Preliminary Evaluation)......................................... 19
2.4 Mchakato wa Zabuni Ndani ya Wizara ......................................................... 25
3.0 MKATABA KATI YA TANESCO NA RICHMOND DEVELOPMENT40
3.1 Madhumuni, Muundo na Muda wa Mkataba................................................ 40
3.2 Malipo ya Kodi.................................................................................................... 43
3.3 Malipo mengine ................................................................................................. 45
3.4 Kuhaulisha Mkataba.......................................................................................... 46
3.5 Fidia kwa Kuchelewa kutekeleza Mkataba................................................. 46
3.6 Ulinganisho na Mikataba Mingine.................................................................. 48
3.7 Uzingatiaji wa Mkataba huu katika kutekeleza Sheria ya CRB na ERB 57
4.0 UTEKELEZAJI WA MKATABA ..................................... 59
4.1 Barua ya Dhamana ya Benki (Letter of Credit) ......................................... 59
4.2 Majadiliano na Makubaliano kuhusu Masharti ya Barua ya Dhamana ya
Benki .................................................................................................................... 63
4.2.1 Maombi ya Masharti ya Barua ya Dhamana ya Benki (Awamu ya
Kwanza)............................................................................................................... 63
4.2.2 Mapendekezo ya Richmond Development Company LLC kutaka
Masharti mengine mapya ya Barua ya Dhamana ya Benki (Awamu ya
Pili)....................................................................................................................... 67
4.3 Mchakato wa Kufungua Barua ya Dhamana ya Benki............................... 70
ii
4.4 Maombi ya Richmond Development Company LLC kubadilisha tena
Masharti ya Barua ya Dhamana ya Benki (Awamu ya Tatu)................... 74
4.5 Kushindwa kwa Richmond Development Company LLC kutimiza
masharti ya Mkataba ........................................................................................ 84
4.6 Mwelekeo Mpya wa Mkataba wa Umeme wa Dharura ............................. 89
4.7 Uhaulishaji wa Mkataba kati ya TANESCO, Richmond na Dowans ........ 95
4.8 Mchakato wa Malipo kwa Dowans Holdings S.A......................................... 97
4.9 Madai na malipo ya Dowans Holdings S.A ya Capacity na Interim
Energy Januari 2006 hadi Oktoba, 2007.................................................. 101
5.0 TAARIFA ZA TAKURU/PPRA .....................................104
5.1 Chimbuko la Uchunguzi................................................................................. 104
5.2 Taarifa ya Mamlaka ya Udhibiti na Ununuzi wa Umma (PPRA) ........... 109
5.3 Taarifa ya TAKURU ......................................................................................... 114
5.4 Vyombo vya Habari – Magazeti .................................................................... 122
6.0 RICHMOND DEVELOPMENT COMPANY LLC NI KINA NANI? .125
6.1 Utambulisho wake Kisheria .......................................................................... 125
6.2 Hadhi ya Richmond kisheria/kikampuni Marekani ................................. 126
6.3 Hadhi ya Richmond kisheria/ kikampuni Tanzania ................................ 132
6.4 Uwezo wa Richmond Kifedha, Kitaalamu, Kiutendaji ........................... 138
7.0 HITIMISHO NA MAPENDEKEZO ..................................142
7.1 Hitimisho.........................................................................142
7.2 Mapendekezo ya Kamati Teule ............................................149
7.3 Shukrani..........................................................................164
iii
VIFUPISHO VYA MANENO
$ Alama ya Dola ya Kimarekani
Aggreko Aggreko International Projects Limited
Alstom Alstom Power Rentals
BoT Bank of Tanzania
BRELA Business Registration and Licensing Authority
CNG Compressed Natural Gas
COD Commercial Operating Date
CRB Contractors Registration Board
CTI Confederation of Trade and Industries
Dba Doing business as
Dk Daktari
Eng. Injinia
ERB Engineers Registration Board
GN Government Notice
GNT Government Negotiation Team
ICC International Chamber of Commerce
IPTL Independent Power Transmission Limited
kWh kilo Watt hour
LC Letter of Credit
LLC Limited Liability Company
Ltd Limited
Mb Mbunge
MDRI Multilateral Debt Relief Initiative
iv
Mhe. Mheshimiwa
MoF Ministry of Finance
MW Mega Watt
PPA Public Procurement Act
PPRA Public Procurement Regulatory Authority
t/a Trading as
TAKUKURU Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa
TAKURU Taasisi ya Kuzuia Rushwa
TANESCO Tanzania Electric Supply Company Limited
TPDC Tanzania Petroleum Development Corporation
TRA Tanzania Revenue Authority
UCP Uniform Customs Practice
US$ United State Dollar
USc United States cents
1
TAARIFA YA KAMATI TEULE ILIYOUNDWA NA BUNGE LA JAMHURI
YA MUUNGANO WA TANZANIA TAREHE 13 NOVEMBA, 2007
KUCHUNGUZA MCHAKATO WA ZABUNI YA UZALISHAJI UMEME WA
DHARURA ULIOIPA USHINDI RICHMOND DEVELOPMENT COMPANY
LLC YA HOUSTON, TEXAS, MAREKANI MWAKA 2006
1.0 UTANGULIZI
1.1 Hoja ya Kuunda Kamati Teule
Tarehe 13 Novemba, 2007 wakati Bunge likijadili Taarifa ya Kamati
ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Biashara kwa Mwaka 2006,
Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mheshimiwa William H. Shellukindo
(Mb), alitoa hoja ya kuunda Kamati Teule ya kuchunguza mchakato
ulioendeshwa nchini mapema mwaka 2006 wa kumpata mzabuni wa
kuzalisha umeme wa dharura wa MW 100 na kutathmini mkataba
baina ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na mshindi wa
zabuni hiyo Richmond Development Company LLC.
Hoja hiyo iliwasilishwa Bungeni kwa mujibu wa masharti
yaliyowekwa na Kanuni ya 104 (1) ya Kanuni za Bunge, Toleo la
mwaka 2004 inayotamka kwamba:-
2
"Kamati Teule yaweza kuundwa na Bunge kwa
madhumuni maalum, kwa hoja mahususi itakayotolewa
kwa ajili hiyo na kuafikiwa".
1.2 Wajumbe na Hadidu za Rejea
Baada ya hoja hiyo kuafikiwa na Bunge, Spika wa Bunge Mheshimiwa
Samuel J. Sitta, (Mb) aliteua Wabunge wafuatao, kuunda Kamati
Teule kwa mujibu wa Kanuni ya 104 (3) ya Kanuni za Bunge, Toleo
la 2004:
(a) Mhe. Dk. Harrison George Mwakyembe, Mb
(b) Mhe. Eng. Stella Martin Manyanya, Mb
(c) Mhe. Mohamed Habib Juma Mnyaa, Mb
(d) Mhe. Lucas Lumambo Selelii, Mb
(e) Mhe. Herbert James Mntangi, Mb
Tarehe 15 Novemba, 2007 Mhe. Spika aliipa Kamati Teule siku
thelathini kukamilisha kazi yake na Hadidu za Rejea zifuatazo kwa
ajili ya kutekeleza kazi hiyo ya uchunguzi;
1. Kubainisha Richmond Development Company LLC ni kina
nani, na ni kampuni ya shughuli zipi na hivyo kupima
uwezo wake kupatiwa zabuni ya kuleta nchini na
kujenga mtambo wa umeme wa gesi wa MW 100,
3
2. Kutathmini mchakato mzima wa jinsi zabuni
waliyoshinda Richmond ilivyoshughulikiwa kuanzia
Kamati ya Zabuni hadi mwisho ili kujiridhisha kuwa
sheria, taratibu, miiko na maadili ya zabuni
yanayotawala zabuni za aina hiyo vilifuatwa au vipi,
3. Kutathmini mkataba baina ya Richmond Development
Company LLC na TANESCO ili kujiridhisha kuhusu uhalali
wa masharti ya mkataba huo ukizingatia gharama na
masharti mengine ukilinganisha na masharti yaliyomo
katika mikataba ya aina hiyo iliyoafikiwa na
TANESCO/Serikali,
4. Kubainisha huduma na misaada mbalimbali waliyopewa
Richmond kama vile kufunguliwa Letter of Credit na
kupima uhalali wake,
5. Kuziangalia na kuzitolea maoni taarifa za TAKUKURU,
PPRA na taarifa zozote nyingine zilizoangalia utaratibu
wa zabuni ya Richmond, na
6. Kuangalia mambo mengine yoyote yenye uhusiano na
mchakato mzima wa Richmond ili kutoa mapendekezo ya
kuboresha taratibu za zabuni kwa siku zijazo, kwa
maslahi ya Taifa letu.
4
1.3 Utekelezaji wa Majukumu
Mara baada ya kuteuliwa, Wajumbe wa Kamati Teule walimchagua
Mhe. Dk. Harrison George Mwakyembe, (Mb) kuwa Mwenyekiti kwa
mujibu wa Kanuni ya 104 (3) ya Kanuni za Bunge, Toleo la mwaka
2004. Aidha, kwa kuzingatia masharti ya Kanuni ya 105(3) ya Kanuni
hizo za Bunge, upana wa hadidu rejea na kipindi kifupi cha mwezi
mmoja tu cha kukamilisha kazi hiyo, Kamati Teule ikaona umuhimu
wa kumchagua mmoja wao kutekeleza wajibu wa Makamu
Mwenyekiti kwa lengo la kuboresha ufanisi katika ufuatiliaji wa
karibu wa masuala mbali mbali ndani na nje ya vikao vya Kamati
Teule. Mhe. Eng. Stella Martin Manyanya, (Mb) akachaguliwa
kutekeleza wajibu huo. Vilevile, Mheshimiwa Spika alimteua Ndugu
Anselm Lyatonga Mrema kuwa Katibu wa Kamati Teule akisaidiwa na
Ndugu Emmanuel Mpanda, Lina Kitosi na Nenelwa Mwihambi.
Kamati Teule ilianza kazi yake mara moja kwa kukusanya na kusoma
nyaraka mbalimbali za msingi kama vile Mkataba kati ya TANESCO
na Richmond Development Company LLC, Sheria ya Ununuzi wa
Umma (Public Procurement Act) ya Mwaka 2004 na Kanuni zake
(Public Procurement Act (Goods, Works, non-Consultant Services &
Disposal of Public Assets by Tender) Regulations of 2005), taarifa ya
uchunguzi ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa
(TAKUKURU)1 na taarifa ya Mamlaka ya Udhibiti na Ununuzi wa
Umma (Public Procurement Regulatory Authority-PPRA) kuhusu
1 Wakati huo ikiitwa Taasisi ya Kuzuia Rushwa (TAKURU)
5
suala hilo. Vilevile, Kamati Teule ilianza kuandaa hati (summons)
kwa mujibu wa vifungu 13 (1) na 14 (1) na (2) vya Sheria ya Haki,
Kinga na Madaraka ya Bunge, 1988 (Sura ya 296) za kuita mashahidi
mbalimbali waliohusika kwa njia moja au nyingine katika mchakato
wa zabuni hiyo ya uzalishaji wa umeme wa dharura.
Hadi kufikia tarehe 15 Disemba jumla ya mashahidi 46 walihojiwa
na maswali 2061 kuulizwa. Pamoja na taarifa zetu tulizozitoa
kupitia vyombo vya habari na kuwataka wenye ushahidi wajitokeze
na kuhakikishiwa kuwa Sheria itawalinda, hakuna shahidi hata
mmoja aliyekuja kwa hiari yake mwenyewe bila kupelekewa hati ya
kuitwa. Aidha, hakuna mtu yeyote aliyeweza kutoa ushahidi wa
kimaandishi ulio wazi zaidi ya wale waliojifanya kuwa na uchungu
kwa kutoa taarifa zisizo na majina, namba za simu wala anwani kwa
madai ya kuogopa kuhatarisha maisha yao.2 Matokeo haya
yanaonesha hali ya uoga na kutojiamini inayowakumba Watanzania
wengi wanapotakiwa kuelezea rasmi yaleyale wanayoyanong'ona
kwa nguvu au kuyazungumza pembeni kwa hamasa kubwa. Kwa
mtindo huu Taifa linaweza kuishia kuwa la walalamishi wasio na
ujasiri wala dhamira ya dhati ya kukemea maovu pale inapobidi.
Mashahidi wengi walioitwa kwa hati hususan kutoka TANESCO,
Wizara ya Nishati na Madini, Wizara ya Fedha na Wizara ya Katiba
na Sheria walionesha hofu, mashaka na hali ya kutojiamini kwa
kutoa majibu yaliyofanana ya kiitifaki-itifaki na yaliyokosa mvuto na
2 Mfano wa barua kama hizo unaambatanishwa.
6
ushawishi wa kawaida mithili ya watu walioketishwa pamoja na
kukaririshwa hoja za kujibu. Kama itakavyoelezwa baadaye, baadhi
ya wataalam wa TANESCO walioikataa Richmond Development
Company LLC mara tatu wakati wa kutathmini zabuni ya umeme wa
dharura, kwa hoja za kitaalam kuwa haifai kwa vigezo vyote
muhimu, walifika mbele ya Kamati Teule wakiwa wapambe nambari
moja wa kampuni hiyo!
Aidha, nyaraka nyingi ambazo Kamati Teule ilizipata toka Serikalini
na taasisi mbali mbali, zilikuwa nakala zilizokosa mtiririko wa
kimasijala. Kamati Teule ilipodai nyaraka halisi kulinganisha na
nakala ilizokuwa nazo, ilipewa majalada yaliyoonesha dalili zote za
kukarabatiwa.
Hali hii ilijitokeza zaidi kwa TANESCO na Wizara ya Nishati na
Madini. Jalada halisi kutoka TANESCO lilichukua siku tatu kuifikia
Ofisi Ndogo ya Bunge likiwa na nyaraka zenye namba zilizokosa
mtiririko stahili. Wizara ya Nishati na Madini ndiyo iliyotia fora kwa
kumtuma Msaidizi wa Katibu Mkuu, Ndugu Julius Sarota tarehe 18
Disemba 2007 akiwa na maagizo ya kuwafungulia Wajumbe wa
Kamati Teule kurasa maalum tu na si nyinginezo hivyo kuinyima
Kamati Teule mtiririko halisi wa mawasiliano. Kamati Teule
haikuridhishwa na utaratibu huo, hivyo ilimtaka Msaidizi huyo wa
Katibu Mkuu aondoke na majalada yake na kumpelekea hati ya
kuitwa Katibu Mkuu, Ndugu Arthur Mwakapugi afike yeye mwenyewe
na majalada hayo.
7
Tarehe 19 Disemba 2007 Katibu Mkuu huyo kwa maneno mengi na ya
kuzunguka alithibitisha kuwa alichokifanya Msaidizi wake yalikuwa
maelekezo ya Wizara.3 Kwa kuzingatia uhaba wa muda wa
kukamilisha kazi ya Kamati Teule na kwamba suala hilo tayari
lilikuwa limechukua siku tatu nzima za Kamati Teule, ugeni wa
Katibu Mkuu huyo katika Wizara hiyo na katika masuala ya Bunge na
uwezekano uliokuwepo kwa Kamati Teule kupata taarifa za ziada
kupitia njia nyingine, Kamati Teule iliamua kusonga mbele na
kumuacha Katibu Mkuu huyo na siri kubwa za Wizara yake.
Pamoja na changamoto hizo, Kamati Teule iliona kuwa ni vyema
baadhi ya Wajumbe waende Houston, Texas, Marekani ili kupata
taarifa za kina na za ziada kuhusu suala hilo. Kamati Teule
inamshukuru sana Mhe. Spika kwa kuzielewa changamoto zilizokuwa
zinaikabili Kamati Teule na kuwawezesha Wajumbe watatu kwenda
Washington DC kukutana na maafisa wa Ubalozi wetu, na Houston
Texas kukutana na wamiliki wa Richmond Development Company
LLC. Wajumbe hao walioondoka Dar-es Salaam kwenda Marekani
tarehe 10 Disemba 2007 ni:
(a) Mhe. Eng. Stella Martin Manyanya, Mb
(b) Mhe. Lucas Lumambo Selelii, Mb
(c) Mhe. Mohamed Habib Juma Mnyaa, Mb, na
(d) Ndugu Anselm L. Mrema (Katibu wa Kamati)
3 Taarifa Rasmi za Bunge, HANSARD ya tarehe 19/12/ 2007 – Mahojiano na Ndugu Mwakapugi.
8
Tarehe 12 Disemba 2007 Kamati Teule ilimwandikia barua Mhe.
Spika kumuomba aiongezee muda kwa sababu kuu mbili: Kwanza,
Wajumbe watatu kati ya watano na Katibu wa Kamati Teule
walikuwa nchini Marekani kuanzia tarehe 10 Disemba 2007
kujiridhisha na taarifa mbalimbali ambazo Kamati Teule imekuwa
ikizipata kuhusu Richmond Development Company LLC. Kwa kuwa
Wajumbe hao walikuwa wanategemea kurejea nchini tarehe 15
Disemba 2007 siku ambayo Kamati Teule ilitakiwa kuwasilisha
taarifa yake kwa Mhe. Spika, na pia taarifa ambazo wangezipata
Marekani zingetakiwa kuingizwa kwenye taarifa ya Kamati Teule na
hata kubadilisha baadhi ya masuala katika taarifa hiyo.
Pili, baada ya uchambuzi wa kina wa ushahidi wa maandishi na wa
mdomo uliotolewa mbele ya Kamati Teule chini ya kiapo, Kamati
Teule iligundua kuwepo kwa mgongano wa ushahidi, hivyo kutia
mashaka juu ya dhamira ya baadhi ya mashahidi. Kamati Teule
iliona umuhimu wa kuwaita tena baadhi ya mashahidi kuthibitisha
kauli zao, na hata kuwachukulia hatua za kisheria baadhi yao ambao
wangeendelea kusema uongo chini ya kiapo ili kulinda heshima ya
Bunge.
Mhe. Spika aliona umuhimu wa kuiongezea Kamati Teule muda,
hivyo tarehe 13 Disemba 2007 akaridhia ombi la Kamati Teule na
kuweka tarehe 31 Disemba 2007 kuwa tarehe ya kuwasilisha taarifa
ya uchunguzi. Hadi kufikia tarehe 31 Disemba 2007 siku
9
ilipowasilisha taarifa yake kwa Mhe. Spika, Kamati Teule ilikuwa
imewahoji jumla ya mashahidi 75 na kuuliza maswali 2717 na
kuzipitia nyaraka na kumbukumbu 104. Mashahidi 4 kati ya hao
walikuja kwa hiari yao bila kupelekewa hati za kuitwa. Mashahidi 7
waliitwa mara mbili. Mashahidi wawili, Ndugu Daniel Yona na Mhe.
Rostam Aziz, (Mb) walipelekewa hati za kuitwa mbele ya Kamati
Teule lakini hawakufika kwa maelezo kwamba walikuwa nje ya nchi.
Ndugu Daniel Yona alitakiwa na Kamati Teule atoe maelezo kuhusu
msingi wa uamuzi wake wa kuipa Richmond Development Company
LLC, haki maalum ya kipekee (exclusive right) ya miezi 18 kuhusu
mradi wa Bomba la Mafuta kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza
mwaka 2004 wakati huo akiwa Waziri wa Nishati na Madini. Maelezo
ya kina ya mradi huu yako sehemu ya sita ya taarifa hii. Mhe.
Rostam Aziz alitakiwa atoe maelezo kuhusu uhusiano wake na
Kampuni za Richmond Development Company LLC na Dowans
Holdings S.A baada ya mashahidi zaidi ya watano kumtaja kuwa ana
uhusiano nazo. Aidha, alitakiwa na Kamati Teule aeleze kwanini
anwani ya posta na anwani ya barua pepe ya kampuni yake ya
Caspian Construction Company Ltd inatumiwa na Dowans Holdings
S.A. Kamati Teule ilipata majina ya baadhi ya wafanyakazi wa
Caspian ambao pia wanaitumikia Dowans Holdings S.A.
10
2.0 UKAME NA TATIZO LA UZALISHAJI UMEME NCHINI
2.1 Taarifa za Awali na Hatua za Serikali
Kwa takribani miaka mitatu mfululizo kuanzia mwaka 2002 nchi
yetu ilikumbwa na tatizo la ukosefu wa mvua za kutosha. Athari za
tatizo hilo hasa katika uzalishaji umeme, zilianza kuonekana mwaka
2004, na kufikia mwishoni mwa mwaka 2005 ikawa dhahiri kwamba
nchi ilikuwa inaelekea kwenye janga kubwa la upungufu wa umeme.
Mahitaji ya mitambo ya gesi ya kuzalishia umeme wa dharura
yakajitokeza.
Kutokana na hali hiyo, mwezi Disemba 2005, TANESCO iliiomba
Serikali kufikiria na kuidhinisha mpango wa kukodisha mitambo ya
kuzalisha umeme wa dharura kwa kutumia gesi kutoka kwenye
makampuni yanayofahamika kwa biashara hiyo chini ya Mikataba ya
kuuziana umeme kwa muda usiopungua miezi kumi na mbili.
Tarehe 28 Disemba 2005 Serikali ilikubali ombi hilo na kuiruhusu
TANESCO kuwasiliana moja kwa moja na kampuni ya Songas kuhusu
mahitaji hayo ya dharura ya nchi. Bila kuchelewa TANESCO
wakawasiliana na Songas ambayo ikaanza mara moja kuandaa
makisio ya mradi huo. Tarehe 11 Januari 2006, CDC Globeleq,
kampuni mama ya Songas, iliwasilisha TANESCO makisio ya
kukodisha mitambo ya gesi ya kuzalisha umeme wa MW 74 ambayo
ingefungwa Ubungo na kuanza kuzalisha umeme katikati ya mwezi
Aprili 2006.
11
Tarehe 13 Januari 2006 Bodi ya Zabuni ya TANESCO ilianza kujadili
zabuni hiyo ya CDC Globeleq na siku sita baadaye, yaani tarehe 19
Januari 2006, Bodi hiyo ikathibitisha mapendekezo ya zabuni hiyo
na kuingia katika majadiliano na CDC Globeleq. Tarehe 30 Januari,
2006 Bodi ya Zabuni ya TANESCO iliyakubali mapendekezo ya Kamati
ya Tathmini ya kuingia mkataba wa uzalishaji umeme kwa miaka
mitano au mitatu kama ifuatavyo: (i) miaka mitano kwa bei ya senti
za Kimarekani 3.2/kWh; au (ii) miaka mitatu kwa bei ya senti za
Kimarekani 5.3/kWh. Chini ya mpango huo, mitambo hiyo ya
kuzalisha umeme ingekuwa mali ya TANESCO baada ya kipindi cha
kukodi kumalizika.4
Taarifa hizi pamoja na mapendekezo ya Wizara ya Nishati na Madini
yaliwasilishwa na kujadiliwa katika Kikao cha Baraza la Mawaziri cha
tarehe 10 Februari 2006, yaani siku nne baada ya kuanza mgao wa
umeme kwa mikoa yote ya Tanzania Bara inayounganishwa na Gridi
ya Taifa.
Pamoja na mambo mengine, Baraza la Mawaziri liliiagiza Timu ya
Wataalamu (Technical, Financial and Legal Experts Team) iliyokuwa
inaundwa na Wizara ya Nishati na Madini, Wizara ya Fedha na Ofisi
ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali chini ya uenyekiti wa Katibu Mkuu
wa Wizara ya Nishati na Madini, ishugulikie masuala makuu manne:
4 Waraka wa Baraza la Mawaziri Na. 2/2006
12
(i) ununuzi wa mitambo ya MW 60-100 ambao ungefungwa
Ubungo pamoja na jenereta za mafuta za MW 40 ambazo
zingefungwa Mwanza, Arusha na Moshi kwa kutumia
fedha zilizotegemewa kutoka Mifuko ya Pensheni nchini;
(ii) ukaguzi wa mitambo ya kutoka CDC Globeleq ili
kujiridhisha na hali na ubora wa mitambo hiyo;
(iii) kuitaka CDC Globeleq ikubali kuiuzia Serikali mitambo
hiyo moja kwa moja tangu mwanzo au iikodishe Serikali
kwa bei ambayo Serikali ingeridhika nayo na siyo kwa
kipindi cha miaka mitano bali kipindi kile tu cha
matatizo ya umeme kutokana na ukame;
(iv) kutafuta na kukagua mitambo ya kuzalisha umeme wa
MW 60-100 Ubungo ikiwa ni pamoja na mitambo ya CDC
Globeleq kwa muda mfupi iwezekanavyo ili ipatikane na
kufungwa mara moja kupunguza tatizo la umeme nchini.
Ni dhahiri kuwa kwa maamuzi hayo, Serikali haikutaka kufanya
makosa kwa kuweka mayai yote kwenye kikapu kimoja kutokana na
hali ya kutisha ya upungufu wa nishati ya umeme nchini. Lakini
Kamati Teule imebaini kuwa utekelezaji wa maamuzi ya Baraza la
Mawaziri haukuwa makini kama inavyoelezwa hapa chini.
Siku hiyo hiyo ya tarehe 10 Februari 2006, Wizara ya Nishati na
Madini, badala ya kuwatumia ujumbe sahihi CDC Globeleq kuwa
Serikali inataka wapunguze kipindi cha ukodishaji mitambo,
washushe zaidi bei yao ya umeme na wawe tayari kuzalisha umeme
13
ifikapo Mei 2006, ilipeleka ujumbe tofauti kabisa kuwa Serikali
inafuta mpango wa kukodisha mitambo kutoka kwao. Sehemu ya
barua hiyo iliyoandikwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Ndugu
Arthur Mwakapugi, ikijibu barua iliyoandikwa na CDC Globeleq
kwenda kwa Waziri Mkuu, inasema:
"I wish to inform you that despite the progress you have so
far made in effecting the project, the Government has
decided to cancel the leasing of the plant and instead will be
provide (sic) funds to TANESCO to procure, install and
commission a similar plant".5 (Napenda kukufahamisha kuwa
licha ya maendeleo mazuri mliyoyafanya katika kutekeleza
mradi, Serikali imeamua kufuta ukodishaji wa mtambo na
badala yake itaipatia TANESCO fedha za kununulia, kufunga na
kuzindua mtambo wa aina hiyo hiyo).
Pamoja na kumhoji aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini kipindi
hicho Mhe. Dk. Ibrahim Msabaha, (Mb) na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo
Ndugu Arthur Mwakapugi kwa muda mrefu na katika siku nne tofauti,
Kamati Teule imeshindwa kupata majibu ya uhakika kwa maswali
yake manne:
(i) Je, kulikuwa na kikao kingine cha Baraza la Mawaziri siku hiyo
hiyo ya tarehe 10 Februari, 2006 kilichotengua maamuzi yake
ya awali ya siku hiyo hiyo?
5 Barua kutoka kwa Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Kumb. Na. CBD.286/397/01 ya tarehe
10/02/06.
14
(ii) Ikiwa jibu ni hapana, kwa nini Wizara ilipeleka CDC Globeleq
ujumbe tofauti na ule ilioagizwa na Baraza la Mawaziri?
(iii) Kwa nini Wizara isitume barua hiyo baada ya kushindwa
kuwashawishi CDC Globeleq kubadilisha masharti yao?
(iv) Maamuzi kama hayo, siku nne ndani ya mgao wa umeme wa
nchi nzima na katika kipindi ambacho Serikali haikuwa na
mkakati mbadala uliokuwa umeiva kama wa CDC Globeleq,
yalikuwa kweli maamuzi makini ya kunufaisha Taifa?6
Kutokana na msimamo huo mpya wa Wizara, TANESCO ikaachana na
mpango wa kukodisha mitambo na kuelekeza nguvu zake kwenye
kununua mitambo mipya ya kuzalishia umeme. Hivyo, tarehe 20
Februari 2006, TANESCO iliwasilisha kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya
Nishati na Madini mpango wa ununuzi wa moja kwa moja kutoka
kwa watengenezaji wa mitambo ya kuzalishia umeme
wanaofahamika duniani chini ya utaratibu unaotambuliwa kama
international shopping chini ya Sheria ya Ununuzi wa Umma ya
mwaka 2004 na Kanuni zake.
Hatua hiyo ikafuatiwa na kikao cha Waziri wa Nishati na Madini na
watendaji wa Wizara na TANESCO tarehe 21 Februari 2006 ambacho
Waziri alikitumia kusisitiza kuwa mpango wa Serikali si kukodisha
mitambo bali kununua. Hivyo akaiagiza TANESCO kutangaza mara
moja zabuni ya kununua mitambo mipya au iliyotumika ya kuzalishia
6 Taarifa Rasmi za Bunge, HANSARD za tarehe 4, 7, 10 na 19/12/07.
15
umeme ama sivyo hatua kali za kinidhamu zingechukuliwa dhidi ya
viongozi wa shirika.7
Waziri alitaka tangazo la zabuni lichapishwe magazetini siku ya
Alhamisi tarehe 23 Februari 2006 na kuwapa TANESCO masharti
yafuatayo kwa zabuni hiyo: (i) ifunguliwe baada ya siku 10 (yaani
tarehe 6 Machi 2006); (ii) tathmini ya zabuni ifanyike kwa siku mbili
(tarehe 7 - 8 Machi 2006). Aidha, Waziri alitaka Kamati ya
Kutathmini Zabuni iongozwe na TANESCO lakini iwe na wajumbe
wengine kutoka Hazina, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali,
Mifuko ya Pensheni na Wizara ya Nishati na Madini.8
2.2 Maandalizi ya Zabuni
Tarehe 22 Februari 2006 TANESCO iliomba idhini ya Mamlaka ya
Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) kutangaza zabuni hiyo kwa
muda wa siku 10 badala ya siku 45 zinazoainishwa katika Kanuni za
Ununuzi.9 Tarehe hiyo hiyo ya 22 Februari 2006, PPRA ikaijibu
TANESCO kwa kuitahadharisha kuwa utaratibu huo utakuwa kinyume
cha taratibu na Kanuni za ununuzi. Muda wa siku 10 hautoshi
kuitisha zabuni ya kimataifa na kuweza kupata wazabuni wenye sifa
zinazohitajika.
7 Muhtasari wa kikao cha tarehe 21/02/06.
8 Angalia Na.7
9 Barua Kumb. Na.DST/18/49 ya tarehe 22/02/06
16
Mamlaka ikaishauri TANESCO kuwa badala ya kutumia njia ya
kutangaza zabuni ya kimataifa (international competitive
tendering) itumie njia mbadala ya ununuzi wa kimataifa
(international shopping) ambapo makampuni mengi
yanayotengeneza mitambo ya kuzalisha umeme yanaalikwa na
"kuyashindanisha kwa kuyaomba yawasilishe zabuni zao badala ya
kutangaza kwani utaratibu huo ungesaidia kuondoa makampuni ya
kati yasiyohusika na uzalishaji umeme".10
Tarehe hiyo hiyo 22 Februari, 2006 TANESCO ikaiarifu Wizara kuhusu
ushauri wa PPRA. Wizara iliukataa ushauri huu na kuiagiza TANESCO
kutekeleza agizo la Waziri bila kukosa kwa kuitangaza zabuni hiyo.
Zabuni hiyo ikatangazwa kwa utaratibu wa ndani tarehe 23 Februari
2006. Hatua hiyo iliishitua PPRA ambayo iliiandikia barua TANESCO
kuelezea kushangazwa kwake na hatua ya shirika hilo kukaidi
ushauri wa kitaalamu na wa kisheria. PPRA ikasisitiza kuwa, njia
pekee kwa TANESCO kupata wazabuni wazuri na wenye sifa stahili
katika kipindi kifupi ni kutumia utaratibu iliyoupendekeza wa
international shopping.11
Hali ya uzalishaji umeme nchini iliendelea kuwa tete na kulazimu
kikao cha Baraza la Mawaziri kufanyika tarehe 23 Februari 2006, na
kuagiza utaratibu wa haraka (fast track) wa kukodi mitambo ya
kuzalishia umeme wa dharura ufanyike. Baraza liliagiza kuwa,
10 Barua Kumb. Na. PPRA/TANESCO/41/16 22/02/06
11 Barua Kumb. Na. PPRA/TANESCO/41/18 ya 23/02/06
17
katika kutekeleza maamuzi haya, Sheria ya Ununuzi wa Umma ya
mwaka 2004 na Kanuni zake za mwaka 2005 zizingatiwe. Pamoja na
msisitizo huo wa Baraza la Mawaziri, Wizara ya Nishati na Madini
ikaendelea kuishinikiza TANESCO kufuata maagizo ya Wizara na si
vinginevyo.
Jumapili tarehe 26 Februari 2006 TANESCO ikionyesha dhahiri
kusukumwa tu na Wizara, ikaiandikia tena barua PPRA kuelezea
kuwa sasa imeagizwa na Serikali kuitangaza zabuni hiyo magazetini,
hivyo mamlaka hiyo ya udhibiti wa ununuzi wa umma itoe idhini ya
kutangaza zabuni ya kimataifa kwa siku chache kuliko zilizowekwa
na sheria.12 TANESCO huku ikijua kabisa kuwa PPRA isingeweza
kuipata na kuijibu barua hiyo Jumapili, ikatangaza zabuni hiyo
magazetini tarehe 27 Februari 200613 na kuwataka wazabuni
wawasilishe zabuni zao tarehe 6 Machi 2006 yaani siku 10 baada ya
kuchukua nyaraka za zabuni tarehe 24 Februari 2006.
Tarehe 1 Machi 2006 PPRA ikaijibu TANESCO kuwa pamoja na
kuendelea na zabuni hiyo, isingekuwa rahisi kwa Shirika hilo la
umeme la Taifa kupata mzabuni anayefaa katika kipindi hicho kifupi
cha siku 10. Hata hivyo PPRA ikaitaka TANESCO kuufuatilia utaratibu
mzima wa zabuni hiyo kwa karibu ili kuhakikisha kuwa taratibu
12 Barua Kumb. Na.DST/18/50 ya tarehe 26/02/06
13 Gazeti la DAILY NEWS tarehe 27/02/06
18
zinafuatwa, ili kuepusha malamiko yasiyo ya msingi kutoka kwa
wazabuni.14
Pamoja na kuipongeza PPRA kwa kuonesha subira ya hali ya juu,
uwazi na ukweli wa kitaaluma, Kamati Teule ilishindwa kubaini
chanzo cha ujasiri wa kiburi ndani ya Wizara ya Nishati na Madini
kiasi cha kupindisha maamuzi ya Baraza la Mawaziri kama
tulivyoona pamoja na kukaidi ushauri wa Mamlaka zilizopo kisheria.
2.3 Mchakato wa Zabuni ndani ya TANESCO
Ili kupata muda zaidi wa zabuni ililazimu muda wa zabuni
kuongezwa hadi tarehe 20 Machi 2006 ambapo jumla ya wazabuni
ishirini na sita (26) walinunua nyaraka za zabuni zilizouzwa kwa
fedha isiyorejesheka (non refundable) ya Dola za Kimarekani 100.
Ni wazabuni wanane (8) tu ndio waliorudisha nyaraka za zabuni hiyo
kama ifuatavyo:
(i) M/S Aggreko International Projects Ltd ya Uarabuni,
(ii) M/S Quantus ya Ujerumani,
(iii) M/S APGUM Co. Ltd ya Ujerumani,
(iv) M/S Globeleq Ltd ya Kanada,
(v) M/S Real Energy Projects ya Uingereza,
(vi) M/S Renco SPA ya Italia,
(vii) M/S Richmond Development Company LLC ya Marekani, na
(viii) M/S GAPCO(T) Ltd ya Tanzania.
14 Barua Kumb. Na. PPRA/TANESCO/41/21 ya tarehe 01/03/06
19
Zabuni zikafunguliwa. Wazabuni wote waliorudisha nyaraka zao za
zabuni waliwakilishwa kwenye ufunguzi. TANESCO ikaunda Kamati
ya Kutathmini Zabuni iliyokuwa na wajumbe 12, kati yao wanane
walitoka TANESCO, wawili kutoka kampuni ya ushauri ya Lahmeyer
International, mmoja kutoka Wizara ya Fedha na mwingine Wizara
ya Nishati na Madini. Kamati hiyo ilipewa wiki moja tu kumaliza kazi
yake na kuiwasilisha taarifa ya tathmini kwenye Bodi ya Zabuni ya
TANESCO tarehe 28 Machi, 2006.
2.3.1 Vigezo vya Tathmini (Preliminary Evaluation)
Kamati ya Tathmini ilitumia vigezo vifuatavyo kupima uwezo wa
mzabuni:
(i) Muda wa kuleta mtambo na kuanza kazi,
(ii) Dhamana ya zabuni (Tender Security),
(iii) Kipindi cha mchakato wa Zabuni (Tender Validity),
(iv) Uwepo wa mitambo na uwezekano wa kusafirishwa,
(v) Uzoefu wa mzabuni kutekeleza na kuendesha mitambo ya aina
hiyo,
(vi) Kibali cha mtengenezaji wa mitambo,
(vii) Uwezo wa kupata mkopo,
(viii) Mapato (turnover)
(ix) Uzoefu na sifa za kiufundi za mzabuni,
20
(x) Viambatisho vya idhini ya kisheria vya kuweza kutoa maamuzi
ya mwisho (Power of Attorney)
(xi) Hati iliyotiwa saini ya mwakilishi wa kisheria wa mzabuni,
(xii) Hati iliyotiwa saini ya mwakilishi wa kisheria wa mtengenezaji
wa mitambo,
(xiii) Hati ya nchi anayotoka mzalishaji wa mitambo,
(xiv) Uwepo wa maelezo ya lazima ya kiufundi,
(xv) Barua ya dhamana kwa ajili mahitaji ya kiufundi na ubora wa
bidhaa inayotolewa na mtengenezaji wa mitambo,
(xvi) Ujazaji fomu ya zabuni kikamilifu,
(xvii) Mchanganuo wa bei/gharama ya umeme,
(xviii) Uhakika kuwa wakala/ kuwa na uwezo wa kufanya
matengenezo na kuwa na vipuri, na
(xix) Muda wa kukodisha mitambo.
Matokeo ya uchambuzi wa zabuni zote nane yalionesha kuwa hakuna
mzabuni hata mmoja aliyetimiza au kukidhi vigezo vya zabuni
vilivyowekwa (non responsive). Kutokana na hali mbaya ya
uzalishaji umeme nchini, Kamati ya Tathmini ikalazimika kuondoa
zaidi ya nusu ya vigezo na kuvibakiza tisa tu ilivyoviona kuwa ni
muhimu sana kwa ngazi ile ya uchambuzi ili kumpata mshindi katika
kundi hilo la wazabuni wanane. Vigezo vilivyobakizwa ni:
(i) Muda wa kuleta mtambo na kuanza kazi,
(ii) Dhamana ya zabuni (Tender Security),
21
(iii) Uwepo wa mtambo tayari kuletwa Tanzania,
(iv) Uzoefu wa mzabuni kutekeleza miradi/ kuendesha mitambo ya
aina hiyo,
(v) Uzoefu na sifa za kitaaluma/ kiufundi za mzabuni
 
(iii) Uwepo wa mtambo tayari kuletwa Tanzania,
(iv) Uzoefu wa mzabuni kutekeleza miradi/ kuendesha mitambo ya
aina hiyo,
(v) Uzoefu na sifa za kitaaluma/ kiufundi za mzabuni,
(vi) Viambatisho vya idhini ya kisheria kuweza kufanya maamuzi ya
mwisho (Power of Attorney),
(vii) Uwepo wa maelezo ya lazima ya kiufundi,
(viii) Ujazaji fomu ya zabuni kikamilifu, na
(ix) Mchanganuo wa bei/ gharama ya umeme.
Wazabuni wote wanane walifanyiwa tena tathmini ya pili kwa
kuzingatia vigezo hivyo tu. Hata hivyo matokeo yakawa yaleyale.
Wazabuni wote wanane wakashindwa kukidhi vigezo hivyo vichache.
Nyaraka tulizozipata kutoka TANESCO zinaonesha maeneo
mbalimbali ya udhaifu miongoni mwa wazabuni kama ifuatavyo:-
i) M/S Aggreko International Projects Ltd ya Uarabuni ilikutwa
na maeneo 7 yenye mapungufu,
(ii) M/S Renco SPA ya Italia maeneo 9,
(iii) M/S APGUM Co. Ltd ya Ujerumani maeneo 12,
(iv) M/S GAPCO(T) Ltd ya Tanzania maeneo 13,
(v) M/S Globeleq Ltd ya Kanada maeneo 14,
(vi) M/S Real Energy Projects ya Uingereza maeneo 15,
(vii) M/S Quantus ya Ujerumani maeneo 16, na
22
(viii) M/S Richmond Development Company LLC ya Marekani
ilikutwa na maeneo 17 yenye mapungufu.
Kamati ya Tathmini haikuona busara kutangaza kuwa imeshindikana
kabisa kumpata mshindi. Hivyo, ikapunguza vigezo zaidi na kubakiza
vitano tu kama ifuatavyo:
(i) muda ambao mtambo utaanza kazi,
(ii) uwepo wa mtambo tayari kuletwa Tanzania,
(iii) uzoefu wa mzabuni kutekeleza miradi/kuendesha mitambo ya
aina hiyo,
(iv) uzoefu na sifa za kitaaluma/ kiufundi za mzabuni, na
(v) uwepo wa maelezo ya lazima ya kiufundi.
Katika hatua hii wazabuni wanne (4) wakashindwa kukidhi vigezo
vichache vilivyobakizwa, hivyo kushindwa kufuzu kuingia hatua ya
pili ya kufanyiwa tathmini ya kina (detailed evaluation). Wazabuni
walioshindwa ni:
(i) M/S Aggreko International Projects Ltd ya Uarabuni,
(ii) M/S Quantus ya Ujerumani,
(iii) M/S APGUM Co. Ltd ya Ujerumani, na
(iv) M/S Globeleq Ltd ya Kanada.
Wazabuni walioonekana kuwa na afadhali kidogo na kuingia hatua
ya pili ya kufanyiwa tathmini ya kina ni:
23
(i) M/S Real Energy Projects ya Uingereza,
(ii) M/S Renco SPA ya Italia,
(iii) M/S GAPCO(T) Ltd ya Tanzania, na
(iv) M/S Richmond Development Company LLC ya Marekani.
Tathmini ya kina ya wazabuni hao wanne walioonekana afadhali
kidogo, ilionesha kuwa Richmond Development Company LLC ya
Marekani bado ilikuwa na mapungufu mengi yaani 13 kupita
wazabuni wengine watatu. M/s Renco SPA ya Italia ilifuatia kwa
kuwa na mapungufu 10; M/s GAPCO (T) Ltd ya Tanzania mapungufu
9 na M/s Real Energy Project ya Uingereza mapungufu 8. Kamati ya
Tathmini iliwasilisha matokeo ya tathmini kwa Bodi ya Zabuni ya
TANESCO ikielezea kwamba hakuna mzabuni hata mmoja
aliyetimiza masharti, na kwamba wote walikosa sifa za kupata
zabuni. Hivyo Kamati ikashauri kuwa zabuni itangazwe upya. Bodi
ya Zabuni ya TANESCO baada ya kuridhia mapendekezo hayo,
iliyawasilisha kwenye Bodi ya Wakurugenzi wa TANESCO tarehe 30
Machi 2006.
Bodi ya Wakurugenzi ya TANESCO ilipitia tathmini nzima na kuamua
kwa kauli moja kuishauri Serikali kurejea kwenye ushauri wa PPRA
wa kutumia njia ya international shopping ili kupata quotations
moja kwa moja kutoka kwa watengenezaji wa mitambo ya
kuzalishia umeme kwa gesi.
24
Kesho yake, yaani tarehe 1 Aprili 2006 Waziri wa Nishati na Madini,
wakati huo Mhe. Dk. Ibrahim Msabaha, (Mb.) akionesha dhahiri
kutotaka njia ya international shopping kutumika, akawaita
wajumbe wote wa Bodi ya Wakurugenzi ya TANESCO na kuwaagiza
wahakikishe kuwa Bodi ya Zabuni ya shirika inawaita tena wazabuni
wote waliojitokeza awali na makampuni mengine yoyote yenye
uwezo wa kuingiza nchini mitambo hiyo. Aidha, Mhe. Dk. Ibrahim
Msabaha, (Mb.) alisisitiza kwa barua kwamba:
"Mshindi wa tenda ya ununuzi wa mitambo mipya
atajulikana baada ya idhini ya Serikali kutolewa.
Composition ya wajumbe wa TANESCO Tender Board
ibadilishwe na kuimarishwa kwa kuwa na wajumbe
wenye uwezo na ni pro-active".15
Ni dhahiri kuwa agizo hili la Waziri lilikuwa batili kwani Sheria ya
Ununuzi wa Umma haimpi Waziri mamlaka ya kuteua Wajumbe wa
Bodi za zabuni za Mashirika yaliyo chini ya Wizara yake.
Tarehe 10 Aprili 2006, wakati Menejimenti ya TANESCO iko kwenye
zoezi la kutekeleza maagizo hayo ya Waziri, Mwenyekiti wa Bodi ya
Wakurugenzi ya TANESCO akasitisha mchakato huo kusubiri
maelekezo ya ziada toka Wizarani. Siku mbili baadaye, yaani tarehe
12 Aprili 2006, Waziri akamwandikia barua Mwenyekiti wa Bodi
15 Maagizo ya Waziri wa Nishati na Madini, Kumb. Na. CBD 88/286/01 ya tarehe 01/04/06
25
kuwa suala la zabuni hiyo haliko mikononi mwa TANESCO tena, na
kusisitiza kwamba:
"Suala la kushugulikia gas turbines za kukodisha
lilishashughulikiwa na Mhe. Waziri Mkuu, ambaye
aliunda Kamati ya wataalamu watatu: KM Hazina, KM
Nishati na AG. Nia ni kuliondoa suala zima kwenye
mikono ya Menejimenti ya TANESCO ambayo imeshindwa
kulishughulikia kwa ufanisi. Waachie Kamati
iliyoteuliwa kufanya kazi hiyo … Pasiwe tena na picha
kama vile Menejimenti ya TANESCO imerejeshewa kazi
hiyo, maana huko kutakuwa ni kukiuka maagizo ya Mhe.
Waziri Mkuu".16
Kesho yake tarehe 13 Aprili 2006, Mkurugenzi Mwendeshaji wa
TANESCO wakati huo, Bw. Adriaan Van De Merwe, akamtumia Katibu
Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini nyaraka zote kuhusu zabuni
yenyewe na uchambuzi wote kwa uamuzi na uteuzi wa mwisho wa
mzabuni.17
2.4 Mchakato wa Zabuni Ndani ya Wizara
Tarehe 20 Aprili 2006, Wizara ya Nishati na Madini iliamua kuunda
timu ya wataalamu ili ichague mzabuni mmoja kati ya wanane
walioshiriki kwenye zabuni na kufanya naye majadiliano ya
16 Barua Kumb. Na. CBD.88/286/01 ya tarehe 12/04/06
17 Barua Kumb. Na. MD/010 ya tarehe 13Aprili, 2006
26
mkataba. Katika kutekeleza azma hiyo, Serikali ilikuwa tayari
imejiandaa na kamati zake zifuatazo: Kamati ya Makatibu Wakuu,
Kamati ya Watalaam na Kamati ya Serikali ya Majadiliano.
Kamati ya Makatibu Wakuu iliundwa katika kikao cha Baraza la
Mawaziri cha tarehe 10 Februari 2006, ikiwajumuisha Makatibu
Wakuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Wizara ya Fedha na
Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Kamati hii ilipewa jukumu la
kusimamia mchakato mzima wa zabuni. Ili kuharakisha zoezi hilo,
Serikali iliunda Kamati ya Wataalam (Team of Experts) ili kuisaidia
kwa karibu Kamati ya Makatibu Wakuu.18
Kamati Teule iligundua kuwa Kamati ya Wataalam ndiyo ilikuwa
yenye maamuzi katika mchakato huu na ndiyo iliyokuwa na
mawasiliano ya karibu na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na
Madini, kwani Kamati ya Makatibu Wakuu ilikutana mara moja tu
toka iundwe.19
Kazi ya kwanza ya Kamati ya Wataalam ilikuwa ni kupitia upya na
kuichambua tathmini iliyofanywa na TANESCO. Kazi ya pili ya
Kamati hiyo ilikuwa ni kumpata mzabuni ambaye angeweza
kutekeleza mradi huo wa umeme wa dharura kwa haraka. Kamati
hiyo ikatupilia mbali vigezo vya msingi vilivyotumika na Kamati ya
Tathmini ya TANESCO na kuweka vipya ambavyo, kwa maoni ya
18 Barua Kumb. Na CBD 214/324/01/13 ya tarehe 21/03/06
19 Taarifa Rasmi za Bunge, HANSARD ya tarehe 05/12/07 – Mahojiano na Ndugu Gray Mgonja.
27
Kamati Teule, vilifanana na vigezo vya mchezo wa watoto wa
sadakarawe: "mwenye kupata apate, mwenye kukosa akose".
Vigezo hivyo vilikuwa:
(i) Uwepo wa mitambo yenyewe pamoja na mitambo ya akiba,
(ii) Uunganishwaji wake kwenye gridi ya Taifa,
(iii) Hali ya usalama wa mitambo yenyewe kwa kulinganisha na
usalama wa gridi ya Taifa,
(iv) Muda wa kuleta mitambo, na
(v) Bei ya umeme.
Kwa maoni ya Kamati Teule, vigezo hivyo vilikuwa haviendani na
uzito na utaalam wa kazi iliyokusudiwa. Pia viliweza kutoa mwanya
hata kwa wazabuni dhaifu kupenyezwa.
Kamati ya Wataalamu ikawaalika wazabuni wote 8 kwa usaili wa
kuwapima kufuatana na vigezo hivyo vipya. Mzabuni mmoja kati ya
wazabuni wanane, M/S GAPCO (T) Ltd hakushiriki. Baada ya usaili
huo, Kamati hiyo ikapata wazabuni wanne ambao walionesha
kukidhi vigezo hivyo vipya. Wazabuni hao ni: Richmond
Development Company LLC, Renco SPA, Aggreko International
Projects Ltd na APGUM Co. Ltd.
Aggreko International Projects Ltd walidai kuwa na uwezo wa
kuzalisha umeme wa MW 40 kwa senti za Kimarekani 6.0/kWh;
Renco SPA walidai kuwa na uwezo wa kuzalisha umeme wa MW 60
28
kwa senti 10.0/kWh; Richmond Development Company LLC ilidai
kuwa na uwezo wa kuzalisha umeme wa MW 100 kwa senti
4.99/kWh; na APGUM Co. Ltd ilidai kuwa na uwezo kuzalisha umeme
wa MW 100 kwa senti za Kimarekani 5.4/kWh.
Kutokana na madai hayo yasiyo na uthibitisho Kamati ya Wataalamu
ikaipendekeza Richmond Development Company LLC kuingia kwenye
majadiliano ya mkataba na Serikali. Katika kuhalalisha ushindi huo
wa Richmond Development Company LLC wajumbe wote wa Kamati
hiyo ya wataalamu, Waziri wa Nishati na Madini aliyetangulia Mhe.
Dk. Ibrahim Msabaha (Mb), Waziri wa sasa wa Wizara hiyo, Mhe.
Nazir Karamagi (Mb), Katibu Mkuu wake, Ndugu Arthur Mwakapugi,
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Johnson Mwanyika, (Mb), Katibu
Mkuu wa Wizara ya Fedha, Ndugu Gray Mgonja na maafisa wote
waandamizi wa Serikali na TANESCO waliotoa ushahidi mbele ya
Kamati Teule, walitoa kauli zilizofanana mithili ya wimbo maarufu
kuhusu sifa za Richmond Development Company LLC zilizoifanya
ishinde kuwa: kwanza, bei yake ya umeme ilikuwa chini kupita
makampuni mengine; pili, kampuni hiyo ilikuwa na ubia na kampuni
kubwa na maarufu duniani ya Pratt & Whitney ya Marekani
inayotengeneza mitambo mbalimbali ya umeme; na tatu,
iliwasilisha pendekezo lake kama mwendelezaji miradi.20
Pamoja na wimbo huo kunoga, Kamati Teule ilishangazwa na
udhaifu mkubwa wa hoja hizo usiolingana hata kidogo na ujuzi na
20 Taarifa Rasmi za Bunge HANSARD za tarehe 28, 29, 30/11/07 na 3,4,5,6,7,10,19,21/12/07
29
uzoefu walionao watendaji wa TANESCO na Serikali hivyo kujenga
hisia kuwa Richmond Development Company LLC ilibebwa. Kwa
mfano, kwanza, Hoja ya bei iliyopendekezwa na Richmond
Development Company LLC kuwa ilikuwa ndogo haijitoshelezi. Je,
Kamati hiyo ililinganisha bei hiyo na nini? Kwani katika kuangalia
kumbukumbu za mchakato wa majadiliano, Kamati hiyo haikuwa na
kiwango chochote cha makadirio ya bei ya umeme wa kukodi
ambacho kingetumika kama kigezo cha kupima unafuu huo kama
upo badala ya kulinganisha na bei za makampuni ambayo yalikwisha
tubebesha mzigo mkubwa wa malipo hapo awali.
Aidha, Kamati Teule ilipata tetesi na baadaye ushahidi kuwa
Richmond Development Company LLC ilikuwa na wapambe ndani ya
Wizara ya Nishati na Madini na TANESCO waliokuwa wanaipa taarifa
(insider dealing). Mfano mdogo tu ni kama vile aliyekuwa
Mkurugenzi wa Usambazaji wa TANESCO Ndugu Mohamed Saleh,
aliyeshiriki kwenye Kamati ya Wataalam, na vile vile Kamati ya
Serikali ya Majadiliano, alipostaafu tu TANESCO akawa mmoja wa
wahandisi waandamizi wa DOWANS HOLDINGS S.A iliyochukua
majukumu ya Richmond Development Company LLC.21
Pili, ni hoja ya kwamba kampuni hiyo ilikuwa na ubia na kampuni
kubwa ya Pratt & Whitney. Katika mchakato wote wa zabuni ndani
ya TANESCO, moja ya masuala kadhaa yaliyoifanya Richmond
Development Company LLC isitiliwe maanani, ni ukosefu wa
21 Taarifa rasmi za Bunge HANSARD ya tarehe 04/12/06 - Mahojiano na Ndugu. Mohamed Saleh
30
ushahidi wa kisheria wa ubia (consortium agreement) kati yake na
Pratt & Whitney. Baada ya kubanwa na Kamati Teule kuhusu
ushahidi wa mahusiano wa kampuni hizo mbili, Wajumbe wa Kamati
ya Wataalamu waliwasilisha mbele ya Kamati Teule business card ya
mzungu mmoja Bwana John Perun22 aliyejiita mwakilishi wa Pratt &
Whitney, na kivuli cha mkataba wa kurasa nne kati ya Richmond
Development Company LLC na Pratt & Whitney wa kubadilishana
taarifa na siyo kuzalisha umeme, na uliokuwa haujathibitishwa na
wakili au shahidi yeyote wa kuaminika kuwa ushahidi wa ubia.23
Kamati Teule imesikitishwa na kushangazwa kwa kiwango cha chini
cha umakini kilichoonyeshwa na wataalam wetu hususan Ofisi ya
Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika kushughulikia suala hili.
Kamati Teule inaamini kuwa bila kujihusisha na Pratt & Whitney,
kampuni hiyo ya Richmond Development Company LLC isingeweza
kamwe kushinda zabuni hiyo. Hivyo ushahidi wa uhusiano wa
kisheria wa Kampuni hizo mbili, ilikuwa suala la msingi ambalo
wataalamu wetu waliwajibika kulipa uzito ili kulinda maslahi ya
nchi.
Katika tovuti yake (www.rdevco.com) Richmond Development
Company LLC ilikuwa inajitangaza kimataifa kuwa kampuni yenye
miradi mikubwa Tanzania ya ujenzi wa kiwanja cha kisasa cha
michezo, ujenzi wa bomba la mafuta la kilometa 1,150 na ukarabati
22 Business Card ya John Perun
23 Nakala ya Mkataba wa kubadilishana taarifa kati ya Richmond Development Company LLC na Pratt &
Whitney.
31
wa viwanja kadhaa vya ndege.24 Kamati Teule ilishindwa kuelewa
kwa nini Kamati ya Wataalam haikuihoji Richmond Development
Company LLC kuhusu uongo huo bayana ambao ulikuwa ushahidi wa
kutosha kuipotezea sifa.
Hoja ya tatu kwamba Richmond Development Company LLC ni
mwendelezaji miradi ilitakiwa vile vile ifanyiwe kazi badala ya
kuiamini tu. Wizara ya Nishati na Madini haiwezi kukwepa lawama
kwa kufumbia macho ukweli kuwa Richmond Development Company
LLC ilishawahi kuwa na Mkataba na Wizara hiyo uliosainiwa tarehe
30 Juni 2004, na kuvunjika mwezi Januari 2006 kwa kampuni hiyo ya
Kimarekani iliyojitambulisha kama mwendelezaji miradi kushindwa
kutekeleza sehemu yake ya mkataba. Wizara inaelewa fika kuwa
kampuni hiyo ilishindwa utekelezaji huo kutokana na kuyumba
kifedha. Mwendelezaji miradi gani ambaye anashindwa kumudu
hata fedha ya kununulia maafisa wake tiketi ya ndege kutoka Dares-
Salaam hadi Afrika Kusini na kurejea?25
Kama tulivyodokeza hapo awali baada ya Kamati ya Wataalam
kumaliza kazi yake na kuwasilisha taarifa Serikalini, Kamati ya
Serikali ya Majadiliano (Government Negotiation Team- GNT) ikiwa
na wajumbe kutoka TANESCO, Wizara ya Nishati na Madini, Wizara
ya Fedha, Benki Kuu na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali,
ikaanza mchakato wa majadiliano ya mkataba na mshindi wa
24 Nakala ya kipeperushi cha Richmond Development Company LLC na nakala ya company profile
25 Taarifa Rasmi ya Bunge HANSARD tarehe 19/12/07 – Mahojiano na Ndugu John Chaggama
32
zabuni. Kama ilivyotokea kwa Kamati ya Wataalam, Government
Negotiation Team vile vile haikufanya kazi ya kuridhisha japokuwa
ilikuwa na uwakilishi mpana. Kwa mfano, suala la kukosekana kwa
consortium agreement kati ya Richmond Development Company LLC
na Pratt & Whitney halikuwasumbua kabisa wajumbe wa Kamati ya
Serikali ya Majadiliano. Wajumbe hao, akiwemo mwakilishi wa
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, waliichukulia business card ya
Bwana John Perun na mkataba wa kubadilishana taarifa kati ya
kampuni hizo mbili kuwa ndio ushahidi wa ubia. GNT ilishindwa
hata kusisitiza kuwa ubia wa kampuni hizo uwekwe wazi katika
mkataba.
Aidha, kwa kuelewa kuwa Richmond Development Company LLC
haikufanyiwa uchunguzi wa awali (due diligence) GNT ilishindwa
kupendekeza kwa Serikali umuhimu wa kuifanyia Kampuni hiyo
uchunguzi baada ya kuiteua (post-qualification) kujua uwezo wake
kifedha, kiutendaji, kiutalaam na kiuzoefu. Katika mahojiano na
Wajumbe wa GNT, Kamati Teule iligundua kuwa walipitisha masuala
mengi kwa mazoea tu, baadhi yao wakiamini kuwa mikataba ya aina
hiyo inatoka Benki ya Dunia na vipengele vyake havibadiliki.26 GNT
ilifika mahali ikakubali bila vigezo vya kueleweka, faini ya
mzabuni/mkandarasi ya Dola 10,000 kwa siku kwa kuchelewesha
utekelezaji wa mradi.
26 Taarifa Rasmi za Bunge HANSARD ya tarehe 28 na 30/11/07 – mahojiano na Ndugu G.Makia
na Chidowu.
33
Tarehe 19 Juni, 2006, Bodi ya Zabuni ya TANESCO ilikutana na
kupitisha uamuzi rasmi wa kufuta zabuni waliyokuwa
wanashughulikia awali na kutangaza kuwa "TANESCO isihusishwe na
mkataba wowote utakaotokana na nyaraka za zabuni waliyoifuta".27
Siku hiyo hiyo ya tarehe 19 Juni 2006, Waziri wa Nishati na Madini
alimwandikia dokezo Waziri Mkuu Mhe. Edward Ngoyai Lowassa,
(Mb) kuwa majadiliano ya awali na Richmond Development Company
LLC yamekamilika hivyo Serikali iiteue Kampuni hiyo kwa lengo la
kuingia mkataba na TANESCO wa kuzalisha umeme wa dharura kwa
miaka miwili. Sehemu ya barua hiyo inasomeka:
"Kamati ya Serikali ya Majadiliano (GNT) inayojumuisha
wataalam kutoka Wizara Fedha, Wizara ya Nishati na
Madini, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Benki
Kuu na TANESCO ilifanya majadiliano na Richmond
Development Company LLC ya Houston, Marekani kutoka
tarehe 8 hadi 16 Juni 2006, kwa kuzingatia maelekezo
yako."28 (msisitizo tumeongezea)
Tarehe 21 Juni 2006, Katibu wa Waziri Mkuu Ndugu B. Olekuyan
aliiandikia Wizara ya Nishati na Madini kuitaarifu kuwa Mhe. Waziri
27 Kumbukumbu za kikao cha Bodi ya Zabuni ya TANESCO, tarehe19/06/06
28 Dokezo Na. CDB 286/397/01 la tarehe 17/06/06
34
Mkuu amekubali mapendekezo na ushauri wa Waziri wa Nishati na
Madini.29
Siku hiyo hiyo tarehe 21 Juni 2006, Waziri wa Nishati na Madini
akamwandikia dokezo Katibu Mkuu wake aiagize TANESCO iingie
mkataba mara moja na Richmond Development Company LLC baada
ya Waziri Mkuu kuidhinisha mapendekezo ya Wizara.30
Muda mfupi baadaye, kwa kutekeleza agizo la Waziri, Katibu Mkuu
wa Wizara ya Nishati na Madini akamwandikia barua Mwenyekiti wa
Bodi ya Wakurugenzi ya TANESCO Balozi Fulgence Kazaura
kumwagiza ahakikishe kuwa TANESCO inasaini mkataba na Richmond
Development Company LLC:
"Kwa barua hii Serikali inaiagiza TANESCO iingie
mkataba na Kampuni ya Richmond ili mitambo iletwe na
kuanza kuzalisha umeme haraka iwezekanavyo.
TANESCO inawajibika kuzingatia makubaliano
yaliyofikiwa kati ya Richmond na Kamati ya Majadiliano
ya Serikali (GNT)."31
Ijumaa ya tarehe 23 Juni 2006, Kaimu Mkurugenzi Mwendeshaji wa
TANESCO, Bwana Johannes .G. Lottering, aliitwa Wizara ya Nishati
na Madini na kuagizwa kusaini Mkataba huo kati ya TANESCO na
29 Barua Kumb. Na. 1/CEA 136/444/01 ya tarehe 21/06/06
30 Dokezo Na. CAB.286/397/01 la tarehe 21/06/06
31 Barua Kumb. Na. CBD.88/286/01 ya tarehe 21/06/06
35
Richmond Development Company LLC. Pamoja na kusita kwake,
hatimaye alisaini mkataba huo.32
Kamati Teule inaelewa hisia walizokuwa nazo viongozi wa ngazi
mbalimbali wa TANESCO kutokana na uongozi wa kiimla wa Wizara.
Tulichokiona hapo juu kwa maana ya mchakato wa Zabuni
kuchukuliwa na Wizara, ulikuwa ni ukiukwaji wa sheria na utaratibu
mzima wa uwajibikaji. Pamoja na dharura iliyokuwa inailikabili
Taifa, Serikali haiwezi kuwa kinara wa kuvunja sheria za nchi. Ni
maoni ya Kamati Teule kuwa Wizara ilikiuka siyo tu masharti ya
sheria na kanuni za ununuzi wa umma, bali vilevile maagizo
mbalimbali ya Baraza la Mawaziri. Kamati Teule isingelikerwa sana
na matukio haya kama Wizara ambayo ni taasisi ya ununuzi
(procurement entity) kama ilivyo TANESCO, ingemalizia mchakato
wake kwa kusaini mkataba huo yenyewe. Kuishinikiza TANESCO
kusaini mkataba ambao vyombo vyake halali vilikuwa havijaupitia,
ni udhalilishaji wa vyombo vya maamuzi ndani ya TANESCO na
upotoshaji wa hali ya juu wa taratibu za kazi na sheria. Inashangaza
kuwa baada ya kudhalilishwa na Wizara kwa kiwango hicho, chombo
kikuu cha maamuzi cha TANESCO, yaani Bodi ya Wakurugenzi,
haikuchukua hatua ya heshima ya kujiuzulu.
Kamati Teule ilishindwa kujua chanzo halisi cha ubabe, ujeuri na
kiburi cha Wizara ya Nishati na Madini kama tulivyoshuhudia, kiasi
cha kupindisha hata maamuzi ya Baraza la Mawaziri bila wasiwasi
32 Taarifa Rasmi za Bunge HANSARD ya tarehe 06/12/07 – mahojiano na Bwana J.G Lottering
36
wowote, kukaidi ushauri wa kitaalamu wa Mamlaka ya Udhibiti wa
Ununuzi wa Umma mara tatu mfululizo kinyume na maagizo ya
Baraza la Mawaziri lililotaka Sheria ya Ununuzi wa Umma
izingatiwe, kukiuka sheria kwa makusudi kwa kuingilia mchakato wa
zabuni wa taasisi nyingine ya ununuzi, kuvipuuza vyombo vya ndani
vya maamuzi vya TANESCO (Bodi ya Wakurugenzi, Bodi ya Zabuni
n.k), kuilazimisha Bodi ya Menejimenti ya TANESCO kuridhia
maamuzi yaliyofanywa na Wizara ya kuibeba Richmond
Development Company LLC kinyume cha sheria na taratibu, n.k.
Baadhi ya mashahidi, wakiwemo waandishi wa habari mashuhuri
nchini, waliinyooshea kidole Ofisi ya Waziri Mkuu kuwa msingi wa
ubabe uliokithiri wa Wizara ya Nishati na Madini katika kuibeba
Richmond.33 Aidha, baadhi ya nyaraka ambazo Kamati Teule
ilizipata katika uchunguzi wake zinaonesha kuwa maelekezo na
maamuzi mengi ya msingi yalikuwa yanafanywa na Waziri Mkuu
badala ya Wizara. Mfano ni barua kutoka Wizara ya Nishati na
Madini kwenda kwa Waziri Mkuu tuliyoinukuu ukurasa wa 33 wa
taarifa hii, ikitamka wazi kuwa GNT ilifanya majadiliano na
Richmond Development Company LLC tarehe 8 hadi 16 Juni 2006
"kwa kuzingatia maelekezo" ya Waziri Mkuu. Tarehe 13 Julai 2006
Waziri wa Nishati na Madini akamwandikia Katibu Mkuu wake kuwa,
"Nimezungumza tena na Mheshimiwa Waziri Mkuu leo juu ya bei ya
mitambo ya Aggreko. Msimamo ni ule ule niliokueleza awali na
33 Taarifa Rasmi za Bunge HANSARD ya tarehe 15/12/2007 – Mahojiano na Saed Kubenea. Vilevile
mazungumzo nje ya kiapo na waandishi wa habari Mbarak Islam na Zeno Mrina wa Ino Communication.
37
ameagiza tuulizie Richmond kama anaweza kutoa 40 MW kwa bei
isiyozidi ile ile ya 4.99 cents per kWh na kama tunaweza kuipata
basi achukuliwe Richmond".
Ushiriki huu wa karibu wa Waziri Mkuu katika kila hatua ya zabuni
ya umeme wa dharura, si lazima uwe ushahidi wa kwamba kiongozi
huyo wa kitaifa alihusika katika kuibeba Richmond. Unaweza pia
ukawa ushahidi wa staili ya kawaida kabisa ya Waziri Mkuu katika
kufuatilia masuala yote ya kitaifa kwa karibu sana tukizingatia
kwamba nchi wakati huo ilikuwa katika kipindi kigumu sana cha
ukosefu wa umeme. Watu pekee waliokuwa wanaujua ukweli
wenyewe, ukweli ambao ungeipa Kamati Teule msingi wa kumhoji
Waziri Mkuu kwa kiapo, walikuwa watatu: Waziri Dk. Msabaha (Mb),
Katibu Mkuu Mwakapugi na Mwenyekiti wa Bodi Balozi Kazaura.
Kamati Teule ikawaita kwa mara ya pili Mhe. Dk. Ibrahim Msabaha
(Mb) na Ndugu Arthur Mwakapugi kwa mahojiano zaidi. Wote
wawili, wakiwa ndani ya kiapo, walikataa katakata kupokea
maagizo kutoka kwa Waziri Mkuu ya kuipa Richmond upendeleo.
Lakini Mhe. Dk. Ibrahim Msabaha (Mb), baada ya mahojiano chini ya
kiapo, akaiuma sikio Kamati Teule kuwa katika suala hilo yeye
atakuwa kondoo wa kafara tu au, kwa maneno yake mwenyewe,
"Bangusilo" kwa lugha ya Kizaramo. Maelezo hayo ya ziada ya Mhe.
Waziri nje ya kiapo yalioana na maelezo aliyoyatoa Balozi Kazaura
nje ya kiapo tarehe 30 Novemba, 2007 ambapo mara baada ya
38
kumaliza mahojiano na Kamati Teule kwa kiapo, Balozi akatoa
maelezo ya ziada kuwa Richmond ilikuwa mradi wa "Bwana
Mkubwa" na "mshirika wake mkubwa kibiashara", akimaanisha Mhe.
Waziri Mkuu na Mhe. Rostam Aziz (Mb). Hii haikuwa mara ya kwanza
kwa Balozi Kazaura kuuhusisha uteuzi wa Richmond Development
Company LLC na mkono wa Waziri Mkuu. Mara ya kwanza ilikuwa
Januari 2007 mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na
Biashara.
Tumelazimika kueleza hata mambo tuliyoelezwa kwa siri kiungwana
(in confidence) kutokana na uzito wa suala lenyewe na dhamana
kubwa tuliyopewa na Bunge ya kuelezea kilichotokea kwa uwazi na
ukweli. Lakini ushahidi huu wa ziada na nje ya kiapo wa viongozi
hawa wawili, haukutoa msaada stahili kwa Kamati Teule kwa kuwa
msingi wa maamuzi yote ya Bunge si minong'ono au tetesi, bali
taarifa zenye uthibitisho halisi.
Ni dhahiri kuwa, kwa watumishi hao "waaminifu" wa Serikali,
isingelikuwa rahisi kumtaja Waziri Mkuu chini ya kiapo. Hatua hiyo
inahitaji ujasiri mkubwa na uzalendo wa hali ya juu. Pamoja na
woga uliokuwa dhahiri kwa watumishi hao, ushahidi wa maandishi,
wa mdomo na wa kimazingira ambao Kamati Teule iliupata kutoka
kwa mashahidi mbalimbali, unatosha kumuhusisha Waziri Mkuu
katika suala hili la Richmond na haumweki mahali pazuri kisiasa na
kimadaraka. Uvumi wa kuhusika kwa Waziri Mkuu mwenyewe moja
kwa moja na baadhi ya washirika wake wa karibu umeenea nchini
39
kwa kiwango cha kushangaza. Kamati Teule inaelewa kuwa uvumi
huo unaweza kuwa umechangiwa na mahasimu wake kisiasa, lakini
uharaka, urahisi na wepesi wa wananchi kuziamini tetesi hizo,
unazua maswali mengi kuhusu imani, heshima na staha aliyojijengea
yeye mwenyewe katika jamii.
40
3.0 MKATABA KATI YA TANESCO NA RICHMOND DEVELOPMENT
COMPANY LLC
3.1 Madhumuni, Muundo na Muda wa Mkataba
Kama tulivyoona awali, Mkataba kati ya TANESCO na Richmond
Development Company LLC hatimaye ulisainiwa na pande
zinazohusika Jijini Dar-es-Salaam tarehe 23 Juni 2006. Madhumuni
ya Mkataba yameainishwa wazi katika Utangulizi wa Mkataba kuwa
ni kusambaza umeme wa dharura kwa kutumia mitambo ya kukodi
ya kuzalisha umeme wa MW 105.6 kutokana na gesi.
Wanasheria waliokuwa kwenye GNT Ndugu Godson Makia na Ndugu
Donald Chidowu waliiambia Kamati Teule kuwa vifungu vya masharti
ya Mkataba huo vimenukuliwa kutoka kwenye Rasimu ya Mikataba
ya Benki ya Dunia.34 Taarifa hiyo haikuipendeza Kamati Teule kwani
matarajio ya Taifa kwa wataalam wetu wanaposhiriki kwenye
majadiliano ya aina hiyo siyo tu kuhamisha vifungu kutoka kwenye
tovuti za taasisi za kimataifa bila kujali na kutafakari masharti ya
mikataba hiyo kwa kuzingatia hali halisi ya mazingira yalivyo kwa
manufaa ya Taifa.
Kamati Teule imebaini kuwa upo udhaifu, ukosefu wa mbinu na
uzoefu katika kujadili mikataba (contract negotiation skills).
34 Majadiliano rasmi ya Bunge HANSARD ya tarehe 28 – 29/11/07
41
Aidha, Kamati Teule imeshangazwa na msimamo
 
Aidha, Kamati Teule imeshangazwa na msimamo wa wataalam wetu
wa kuheshimu maelekezo ya taasisi za kimataifa wakati kanuni za
ununuzi (Public Procurement Regulations GN. 97) zilizotungwa chini
ya sheria za ununuzi wa umma zinaelekeza kufuata mifumo ya
mikataba iliyoandaliwa na PPRA. Kanuni ya 115 inatamka kwamba
kila juhudi itafanywa kuhakikisha kuwa sampuli za mikataba ya
ununuzi zilizoandaliwa na mamlaka zinatumika na pale ambapo
rasimu zingine za mikataba nje ya mamlaka zinatakiwa kutumika,
basi idhini ya Mamlaka na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali
itahitajika.
Pamoja na kwamba madhumuni ya msingi ya Mkataba huu ni
kuzalisha na kusambaza umeme wa dharura (emergency power
supply) muda wa mkataba huo ni miezi ishirini na minne (24)!
Tukirejea kwenye tangazo la zabuni la TANESCO, muda wa kukodi
mitambo hiyo ilikuwa ni miezi kumi na mbili tu na muda huo
ungeweza kuongezwa kutegemea hali ya uzalishaji umeme nchini.
Hata hivyo, muda huo uliongezwa na GNT na kuwa miezi ishirini na
nne. Swali linalojitokeza ni kwamba, GNT ilikuwa inakimbilia wapi
kuongeza muda wa kukodi mitambo hiyo kutoka miezi kumi na mbili
mpaka ishirini na nne wakati kulikuwa na fursa ya kuongeza muda
pale inapobidi?
Kwa kuwa madhumuni ya Mkataba huu ilikuwa ni kuzalisha umeme
wa dharura, Serikali ilipaswa kutilia maanani hali ya kuongezeka
42
kwa maji katika mabwawa yaliyoko nchini ili kuona umuhimu wa
kuongeza au kutoongeza muda wakati wa ukomo wake. Uamuzi wa
kuongeza muda kabla ya kutathmini hali ya uzalishaji umeme kwa
njia ya maji zaidi ya kipindi cha mwaka mmoja kilichokusudiwa
awali, unatia mashaka. Ukweli ni kwamba maji katika mabwawa
nchini yalikuwa yameshajaa mapema Januari, 2007 na muda wa
awali wa kuisha Mkataba ungekuwa tarehe 11/9/2008; hivyo
ingekuwepo nafasi ya kutosha kuamua kuongeza au kutoongeza
muda wa mkataba.
Kamati Teule inasisitiza kuwa, udharura wa mradi huu ulimalizika
pale mabwawa yetu yalipojaa maji mapema mwezi Februari 2007,
hivyo kitendo cha TANESCO kukubali mkataba kuhaulishwa bila
marekebisho kimewashangaza hata hao waliohaulishiwa mkataba
huo.35 Hii pia inaonyesha udhaifu kwa watendaji wetu kushindwa
kuona fursa iliyokuwa wazi katika kifungu 12.3 cha mkataba
ambacho kingeiwezesha TANESCO kuvunja mkataba bila ya kupata
hasara. Matokeo yake TANESCO imeingia kwenye gharama kubwa ya
kulipa capacity charge na gharama nyinginezo, wakati huo huo
ikizingatiwa kuwa mitambo hiyo inatumika chini ya kiwango
kilichokusudiwa au kutotumika kabisa (under utilization) kutokana
na mabwawa yetu kuzalisha umeme wa bei nafuu ukilinganisha na
bei ya umeme huo wa kukodi.
35 Majadiliano rasmi ya Bunge HANSARD ya tarehe 27/12/07 – mahojiano na Mkurugenzi Mwendeshaji
wa Dowans Holdings S.A Bwana Gui Picard
43
Kwa ujumla muda wa kumalizika kwa mkataba huu una utata
mkubwa. Utata wenyewe unatokana na ukweli kwamba kwa mujibu
wa kifungu cha 15.18 mkataba unaanza siku moja baada ya
kufunguliwa Barua ya Dhamana ya Benki (Letter of Credit - LC)
ambayo ni tarehe 12/09/2006 hivyo mkataba huu ungeisha muda
wake tarehe 11/09/2008. Iwapo tarehe ya awali ya kuzindua
mitambo hiyo (Commercial Operational Date - COD) yaani tarehe
2/2/2007 ingekuwa ndio msingi wa kuanza mkataba huu, basi
mkataba huu ungeisha tarehe 2/2/2009. Aidha, kwa kufuata tarehe
ya sasa ya COD yaani tarehe 4/10/2007 mkataba huo utaishia tarehe
4/10/2009. Kutokana na hali hiyo, kutakuwa na ongezeko la muda
wa mkataba kwa miezi 13 ikizingatiwa mkataba ungeanza tarehe
12/09/2006. Kamati Teule imebaini kuwa ongezeko hilo
linaliongezea Taifa mzigo wa kiasi cha Dola za Kimarekani 47.5
millioni au Tsh. 59.375 bilioni kutokana na malipo ya capacity
charge.
3.2 Malipo ya Kodi
Kwa mujibu wa Kifungu cha 3.4 cha Mkataba, TANESCO inawajibika
kulipia kodi zote zinazotakiwa kulipwa na Richmond Development
Company LLC kwa mujibu wa Sheria, pamoja na malipo mengine
yanayohusiana na uingizaji nchini na utoaji nje ya nchi mitambo
husika, ikiwa ni pamoja na vifaa, vipuri n.k. vya mitambo hii.
Kifungu hicho kinasomeka kama ifuatavyo:
44
"All taxes and charges arising in relation to the
importation and exportation of the plant, equipment,
tools, spare parts, consumables, testing and
monitoring equipment or in connection with the
supplier's performance of its obligations under this
Agreement generally that become due in accordance
with the laws of Tanzania shall be paid for by
TANESCO at its sole cost and expense".
Tafsiri ya Kifungu hiki cha mkataba ni kwamba, Richmond
Development Company LLC inalipiwa kodi zote zinazohusiana na
utekelezaji wa wajibu wake chini ya Mkataba huo, hata pale
ambapo itaamua kuihamishia mitambo yake nchi nyingine.
Kwa maoni ya Kamati Teule kifungu hiki cha Mkataba kinatoa
unafuu usiostahili katika hali ya kawaida, au kwa namna yoyote ile,
kwa Richmond Development Company LLC na kuibebesha TANESCO
mzigo wa kulipia kodi isizostahili.
Vilevile, masharti ya Kifungu hiki yanaifanya TANESCO ibebe mzigo
wa kulipia kodi zinazohusika na uendeshaji (operations) na
matengenezo (maintenance) ya mitambo ya Richmond Development
Company LLC kutokana na hoja kwamba, uendeshaji na
matengenezo ya mitambo vimetafsiriwa kama shughuli ambazo
zinahusiana na utekelezaji wa majukumu ya Richmond Development
45
Company LLC chini ya Mkataba (in connection with the supplier's
performance of its obligations under the Agreement).
Kwa wigo wa tafsiri ya majukumu haya, TANESCO inawajibika kulipa
hata gharama za Bima, ada za mawakili wa wawekezaji hawa,
gharama ambazo TANESCO haina uwezo wa kuzisimamia wala
kuzipunguza.
3.3 Malipo mengine
Kwa mujibu wa Mkataba, TANESCO ina wajibu wa kufanya malipo
yafuatayo kwa Richmond Development Company LLC kuanzia tarehe
ya kuanza uzalishaji (COD):
(i) Malipo ya umeme unaotumiwa (energy purchase price) – Dola
za Kimarekani 0.0499 kwa kWh.36 au Shilingi za Kitanzania
62.375 kwa kWh, na
(ii) Gharama za kudumu za uwezo wa mitambo (capacity charge)
Dola za Marekani 34.60565 kwa kW kwa mwezi au Shilingi za
Kitanzania 43,257.063 kwa kW. Malipo haya yanafanywa hata
pale ambapo mitambo ya Richmond Development Company
LLC haizalishi umeme.37
36 Tafsiri ya Interim Energy Purchase Price ukurasa wa 3 wa Mkataba
37 Kifungu 4.2 na Nyongeza C ya Mkataba
46
3.4 Kuhaulisha Mkataba
Mkataba huu una kifungu cha 15.12 kinachoruhusu wahusika wa
Mkataba huu kuhaulisha haki na majukumu yao chini ya Mkataba
kwa chombo kingine chochote walichokiteua lakini kwa makubaliano
ya pande zote mbili.
Kitendo cha kuweka kipengele cha kuhaulisha Mkataba,
kinadhihirisha moja kwa moja woga wa Wizara ilioujadili na
kuuidhinisha mkataba huu wa kutokuwa na uhakika na utendaji wa
wazabuni inaowachagua. Vilevile kinaruhusu biashara ndani ya
mkataba, biashara ambayo Serikali haina udhibiti nayo kwa maana
ya kujua hulka na usalama wa mrithi wa mzabuni. Kamati Teule
haioni mantiki ya kuhaulisha mkataba wakati mtoa huduma
ameshindwa kutekeleza masharti ya mkataba.
3.5 Fidia kwa Kuchelewa kutekeleza Mkataba
Kwa mujibu wa Kifungu cha 4.4 cha Mkataba, Richmond
Development Company LLC inawajibika kuilipa TANESCO Dola za
Kimarekani 10,000 (Tsh.12.5 milioni) kwa siku kwa ucheleweshaji
wa kuanza kuzalisha umeme kulingana na tarehe iliyowekwa katika
Mkataba.
Wataalam walipotakiwa kueleza jinsi walivyofikia kiwango hicho,
walitoa maelezo kuwa walifuata viwango vya kimataifa kutoka kwa
47
wataalam wao (Consultants) bila kutumia vigezo vyovyote
vinavyohalalisha kiwango hicho.38
Kamati Teule imebaini kuwa malipo ya Dola za Kimarekani 10,000
kwa siku ni kidogo sana ukilinganisha na capacity charge ambayo
TANESCO inalipa kwa siku kwa mwekezaji huyo. TANESCO ingeweza
kurejesha kiwango kile kile ambacho Richmond Development
Company LLC inalipwa inapokuwa haizalishi umeme, au kiwango
ambacho TANESCO ingepata kutokana na mauzo ya umeme
unaozalishwa kwa siku kwa bei ya TANESCO, au wangeweza kutumia
formula ya haki (fair deal) ya wastani wa bei zao kwa siku.
Kwa mfano, Richmond Development Company LLC imechelewesha
mradi kwa siku 243 kuanzia tarehe 2/2/07 hadi tarehe 2/10/2007.
Fidia tunayodai kufuatana na mkataba ni Dola za Kimarekani 10,000
x 243 = 2,430,000 ambazo ni sawa na Tsh.3.037 bilioni tu. Endapo
mradi huo ungecheleweshwa kwa miaka miwili wangetakiwa kulipa
Dola za Kimarekani 10,000 x siku 365 x miaka 2 = Dola za
Kimarekani 7.3 milioni (Tsh 9.125 bilioni tu).
Kwa mujibu wa mkataba, Richmond Development Company LLC
inalipwa Dola za Kimarekani 121,811 (Tsh 152.264 milioni) kwa siku
kama gharama za kudumu za uwezo wa mitambo yao (capacity
charge). Fedha hizi zinalipwa kila siku bila kujali kama Richmond
Development Company LLC imezalisha umeme au la. Kwa msisitizo
38 Taarifa rasmi za Bunge HANSARD ya tarehe 23/11, 30/11, 3/12/07
48
ni kwamba wakati sisi tunawalipa shilingi milioni 152.264 kwa siku,
wao wanatulipa Tsh. milioni 12.5 kwa siku pale wanapotupa hasara
kwa kutokuzalisha umeme kwa wakati. Hasara ambayo TANESCO
ilipata kwa kukosa umeme inaweza kutambuliwa kwa kuangalia
wastani wa bei inayowauzia wateja wake ambayo ni sawa na Dola za
Kimarekani 0.07 au Tsh 87.5. Hivyo, ingekuwa halali kabisa kwa
TANESCO kuidai Richmond Development Company LLC Tsh. milioni
228.657 kwa siku. Kamati Teule inaona tatizo kuu linalotukabili ni
ukosefu wa mbinu za kibiashara, kutojiamini, kukosa umakini wa
kitaaluma na ubinafsi upande wa maafisa wetu wanaojadili
mikataba kwa niaba yetu.
3.6 Ulinganisho na Mikataba Mingine
Mzigo mkubwa ambao TANESCO inabeba chini ya mkataba wake na
Richmond Development Company LLC unajirudia katika mikataba
mingine kati ya TANESCO na makampuni mengine ya umeme kama
vile IPTL, AGGREKO, ALSTOM na SONGAS.
Katika kuchambua mikataba mbalimbali ya kuzalisha umeme wa
dharura wa muda mfupi na ile ya muda mrefu, Kamati Teule
imebaini kuwa baadhi ya miradi imeigharimu Serikali pesa nyingi
mno kulinganisha na mradi wenye uwezo sawa inayotumia nishati ya
aina nyingine. Mfano halisi ni mradi wa Alstom Power Rentals na
Aggreko International Project Ltd, hii yote inazalisha umeme wa MW
49
40 lakini inatofautiana kwa aina ya nishati ya uzalishaji (Angalia
Jedwali II).
Mradi wa Alstom Power Rentals wenye capacity charge ya Dola za
Kimarekani milioni 21.9 (Tsh. 27.375 bilioni) umegharimu Serikali
jumla ya Dola za Kimarekani milioni 130.181 (Tsh. 162.726 bilioni)
kwa mwaka mmoja. Hii ni pamoja na gharama za dizeli kwa
uendeshaji wa mtambo huo. Mradi wa AGGREKO wenye capacity
charge ya Dola za Kimarekani milioni 17.437 (Tsh.21.796 bilioni)
umeigharimu Serikali jumla ya Dola za Kimarekani milioni 28.860
(Tsh. 36.075 bilioni) pamoja na gharama ya gesi kwa mwaka mmoja.
Kwa kubaini mzigo mkubwa wa gharama hizo uliosababishwa hasa
na nishati ya diesel na kwa kuzingatia utajiri wa nishati ya gesi
tuliyobarikiwa kuwa nao, Kamati Teule inashauri njia mbadala
ambayo inaweza kutumika ili kuokoa gharama hizo za dizeli hasa
kwa vile sehemu nyingi za pembezoni mwa Tanzania zinatumia
mitambo ya mafuta na haijaunganishwa na Gridi Kuu ya Taifa
(Msongo Mkuu wa Umeme).
Kamati Teule imeshuhudia matumizi ya gesi asilia inayohifadhiwa
katika visima vya gesi (gas wells). Gesi hiyo husafirishwa mahali
husika kwa kutumia trailers maalum. (Angalia Jedwali Na I).
Kutokana na takwimu tulizozipata, mradi wa Mwanza wa Alstom
endapo ungetumia gesi tungeweza kunusuru jumla ya Dola za
50
Kimarekani 68.294 (Tsh. Bilioni 85.4) kwa mwaka wa kwanza na
tungeepukana na gharama za capacity charge ya kila mwezi. Wakati
huo huo mitambo hiyo itabaki kuwa mali yetu. (Angalia uchambuzi
wa kimahesabu baada ya Jedwali Na. I & II).
JEDWALI Na. I
MAELEZO KIPIMO BEI (US
 
NAOMBA MNIRUHUSU NIWEKE RIPOTI YA BUNGE HAPA NA HUKUMU YA ICC NA MKATABA WA TANESCO NA DOWNS ILI TUJADILI VIZURI

tafadhali
 
nafikiri wengine wanapata shida kwenye attachment wacha niweke hivi kila mtu asome na tuchangie kwa umoja au unaonaje mkuu

Kama ni lazima sana kuiweka kama unavyotaka, basi anagalau jaribu ku-format kido ili idadi ya mistari ipungue. Vinginevyo lengo lako haliwezi kutimia!
 
Kama ni lazima sana kuiweka kama unavyotaka, basi anagalau jaribu ku-format kido ili idadi ya mistari ipungue. Vinginevyo lengo lako haliwezi kutimia!


ok thanks
 
SASA MBONA HUKUMALIZIA HIYO RIPOTI YA mwakyembe au niimalizie mimi maana ninayo hapa???
 
Wamelipwa. Tumelipa.
P
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…