Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,436
- 5,234
Kiongozi wa ACT Wazalendo, Dorothy Semu, amesema chama chake kimeamua kushiriki Uchaguzi Mkuu wa Oktoba ili kutetea na kulinda demokrasia nchini, akisisitiza kuwa ni haki ya kila mwananchi kuchagua viongozi wanaoweza kuleta maendeleo.
Amebainisha haya Busega, mkoani Simiyu, Semu na kwamba haki ya kupiga kura imekuwa ikiporwa na kukandamizwa kwa miaka mingi, lakini sasa ni wakati wa wananchi kusimama kidete kuilinda.
Ameongeza kuwa licha ya changamoto nyingi katika mifumo ya uchaguzi, ACT Wazalendo haijasita kushiriki kwa sababu imedhamiria kuhakikisha sauti za wananchi zinasikika.
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Kauli hiyo ya Dorothy Semu ni mwendelezo wa msimamo wa ACT Wazalendo kujitokeza kwa nguvu katika uchaguzi wa mwaka huu, licha ya kuwepo kwa miito kutoka kwa baadhi ya vyama vya upinzani ya kususia uchaguzi huo.
Amebainisha haya Busega, mkoani Simiyu, Semu na kwamba haki ya kupiga kura imekuwa ikiporwa na kukandamizwa kwa miaka mingi, lakini sasa ni wakati wa wananchi kusimama kidete kuilinda.
Ameongeza kuwa licha ya changamoto nyingi katika mifumo ya uchaguzi, ACT Wazalendo haijasita kushiriki kwa sababu imedhamiria kuhakikisha sauti za wananchi zinasikika.
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Kauli hiyo ya Dorothy Semu ni mwendelezo wa msimamo wa ACT Wazalendo kujitokeza kwa nguvu katika uchaguzi wa mwaka huu, licha ya kuwepo kwa miito kutoka kwa baadhi ya vyama vya upinzani ya kususia uchaguzi huo.