Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Bi. Dorothy Semu, amesema kuwa chama chake kinaingia katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 kwa lengo kuu la kulinda thamani ya kura ya Mtanzania, kuhakikisha Chama Cha Mapinduzi (CCM) hakipitwi bila kupingwa na kutumia uchaguzi kama jukwaa la kusikiliza na kuzungumza masuala halisi yanayowagusa wananchi.
Akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika katika eneo la Sapiwi, Jimbo la Bariadi Vijijini, mkoani Simiyu, Julai 5, 2025, Semu amesisitiza kuwa uchaguzi huu si wa kawaida, bali ni fursa kwa Watanzania kudai heshima ya kura yao na kupaza sauti dhidi ya uonevu wa kisiasa unaotokana na matumizi mabaya ya vyombo vya dola.
Bi. Semu amewaonya maafisa wa vyombo vya dola kutotumika kama silaha za kuwanyamazisha wapinzani au kukandamiza harakati za kisiasa. Amesema kuwa taasisi hizo ni kwa ajili ya kulinda haki na amani ya wananchi wote bila kujali itikadi au chama chao.
Akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika katika eneo la Sapiwi, Jimbo la Bariadi Vijijini, mkoani Simiyu, Julai 5, 2025, Semu amesisitiza kuwa uchaguzi huu si wa kawaida, bali ni fursa kwa Watanzania kudai heshima ya kura yao na kupaza sauti dhidi ya uonevu wa kisiasa unaotokana na matumizi mabaya ya vyombo vya dola.
Bi. Semu amewaonya maafisa wa vyombo vya dola kutotumika kama silaha za kuwanyamazisha wapinzani au kukandamiza harakati za kisiasa. Amesema kuwa taasisi hizo ni kwa ajili ya kulinda haki na amani ya wananchi wote bila kujali itikadi au chama chao.