PAYE
JF-Expert Member
- Jun 19, 2025
- 365
- 457
Rais wa 47 wa Taifa la Marekani, Donald John Trump (79) ameeleza mashaka yake ya kuingia mbinguni ambapo amesema hana hakika kama kuna kitu kinachoweza kumfanya aingie mbinguni ila ana uhakika amesaidia maisha ya watu wengi.
Trump alisema hayo akijibu swali la mwandishi wa habari aliyemuuliza kuhusu ratiba yake ya kusali na jinsi itakavyomsaidia kuingia mbinguni ndipo Trump akasema;
"Unajua mimi sidhani kama kuna kitu chochote kitakachonipeleka mbinguni. Kweli, sidhani. Huenda mimi si mtu wa kwenda mbinguni. Labda niko mbinguni sasa hivi, tunaposafiri kwa ndege ya Air Force One. Sina uhakika kama nitaweza kwenda mbinguni, lakini nimefanya maisha ya watu wengi kuwa bora zaidi."
Amesema Trump baada ya kauli yake Wiki kadhaa zilizopita kudai kutaka kuimaliza Vita ya Ukraine kwani itamsaidia kwenda Mbinguni.
Trump alisema hayo akijibu swali la mwandishi wa habari aliyemuuliza kuhusu ratiba yake ya kusali na jinsi itakavyomsaidia kuingia mbinguni ndipo Trump akasema;
"Unajua mimi sidhani kama kuna kitu chochote kitakachonipeleka mbinguni. Kweli, sidhani. Huenda mimi si mtu wa kwenda mbinguni. Labda niko mbinguni sasa hivi, tunaposafiri kwa ndege ya Air Force One. Sina uhakika kama nitaweza kwenda mbinguni, lakini nimefanya maisha ya watu wengi kuwa bora zaidi."
Amesema Trump baada ya kauli yake Wiki kadhaa zilizopita kudai kutaka kuimaliza Vita ya Ukraine kwani itamsaidia kwenda Mbinguni.