Trump: Iran sio wepesi, wanaijua Vita

Trump: Iran sio wepesi, wanaijua Vita

Mawele

JF-Expert Member
Joined
Jul 25, 2023
Posts
999
Reaction score
3,553
Rais wa Marekani Donald Trump amezungumzia hali ya mvutano na changamoto za kiusalama zinazohusisha Iran akisisitiza ugumu wa kuingia katika mifumo ya Nchi hiyo kutokana na uimara wake wa kijeshi na kiulinzi ambapo kauli hiyo imekuja katika muktadha wa tathmini yake kuhusu nguvu na uwezo wa Iran katika kukabiliana na Maadui zake.

Trump ameeleza hayo leo April 06, 2026, na kubainisha kuwa Iran imejijengea taswira ya Taifa lenye Wapiganaji hodari na Watu wenye msimamo mgumu hali inayofanya iwe vigumu kwa Mataifa mengine kuingilia au kushinda kirahisi.

Aidha, Rais amebainisha kuwa licha ya kuwepo kwa mabadiliko ya nguvu kwa kipindi cha hivi karibuni bado Nchi hiyo inaendelea kuwa tishio lenye uzito.

"Kuingia himaya ya Mtu inahitaji mapambano na sidhani kuna Nchi ngumu kama Iran maana inahitaji mapambano sana, ni Wapiganaji wazuri sana ni Watu wagumu sana” amesema Trump.
 
Ndio kajua leo baada kuona Vijana wake wanalejeshwa kwenye Masanduku!!!!!
 

Attachments

  • 1775527986747.jpg
    1775527986747.jpg
    417.4 KB · Views: 24
  • images (1) (13).jpeg
    images (1) (13).jpeg
    51.7 KB · Views: 18
  • 4cbvbb5fc697302p59i_800C450.jpg
    4cbvbb5fc697302p59i_800C450.jpg
    62.3 KB · Views: 17
  • 20260402_160858.jpg
    20260402_160858.jpg
    66.3 KB · Views: 17
  • 1774978362327.jpg
    1774978362327.jpg
    111.9 KB · Views: 21
Watasema tu muda bado wanao!!
 

Attachments

  • 4cbv7fe6ebc3ae2p2la_800C450.jpg
    4cbv7fe6ebc3ae2p2la_800C450.jpg
    64.7 KB · Views: 19
  • 1773266705287.jpg
    1773266705287.jpg
    51.1 KB · Views: 18

Similar Discussions

Back
Top Bottom